Na Mwandishi Wetu,Ruvuma
WAKULIMA wa zao la kahawa wanaohudumiwa na Chama cha Msingi cha
Ushirika KImuli Amcos kata ya Utiri Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma,
wamefanikiwa kuzalisha tani 105,986.95 za kahawa zilizowaingizia zaidi
ya Sh.bilioni 14,022,174,698.40 kuanzia Msimu wa kilimo 2021/2022 hadi
2024/2025.
Katibu wa
Chama hicho Aron Komba amesema,katika msimu 2021/2022 wakulima
walizalisha tani 548,551 zenye thamani ya Sh.bilioni
3,299,453,120,msimu wa kilimo 2022-2023 walizalisha tani 455,643 ambazo
ziliwaingizia Sh.bilioni 3,065,405,776.40.
Aidha alisema,msimu wa 2023/2024 Wakulima ambao ni Wanachama wa Kimuli
Amcos walizalisha jumla ya kilo 585,288 zenye thamani ya Sh.bilioni
2,929,893,908 na msimu 2024/2025 walizalisha kilo 530,253 ambazo
waliuza Sh.bilioni 4,727,421,894 kupitia njia ya minada.
“Pia kwa muda wa miaka minne ya Uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu
Hassan,tumetoa mikopo ya pembejeo yenye thamani ya Sh.bilioni
3,056,783,867 kwa Wakulima 7,005 wanaojishughulisha na kilimo cha kahawa
na mazao mengine ya chakula na biashara”alisema Komba.
Kwa mujibu wa Komba,msimu wa kilimo 2022/2023 wametoa mikopo ya
pembejeo ya Sh.957,343,812 kwa wanachama 2,137 mwaka 2023/2024
Sh.917,834,200 kwa Wanachama 2,381 na mwaka 2024/2025 wametoa mikopo
yenye thamani ya Sh.1,181,605,855 iliyokwenda kwa Wananchama 2,487.
Alisema,mikopo hiyo imewasaidia Wanachama kulima kwa tija na kuongeza
uzalishaji kwani hapo awali walikuwa wanaangaika kutafuta pembejeo
ambazo ziliuzwa kwa bei kubwa kati ya Sh.165,000 hadi 170,000 kwa mfuko
mmoja wa kilo 25.
Alisema,hali hiyo ilipelekea baadhi ya wakulima kukata tamaa na
kutoendelea na shughuli zao za kilimo kutokana na kushindwa kumudu
gharama ya pembejeo ambapo, amempongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan,kwa
kuanza utaratibu wa kutoa pembejeo za ruzuku kwa zao la kahawa.
Komba,ameiomba Serikali kuendelea kutoa pembejeo za ruzuku kwa zao la
kahawa ili kuwapunguzia wakulima mzigo mkubwa wa kununua pembejeo kwa
bei ya juu na kuongeza upatikanaji wa pembejeo za ruzuku ili wakulima
waweze kuzalisha kwa wingi.
“Naishauri Serikali kama inataka kufanikisha mpango wake wa kutouza
kahawa ghafi basi ituwezeshe kwa kutujengea miundombinu ili tuweze
kukaanga kahawa tunayozalisha kwa ajili ya matumizi ya sisi wenyewe na
watu wengine na nyingine tuuze kwenye soko la nje"alise
ma Komba.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Amcos ya Kimuli Yordan Komba
alisema,katika kipindi cha miaka minne Chama hicho kimepiga hatua kubwa
kwa kuongeza Wanachama kutoka 364 tangu kilipoanzishwa mwaka 1993 hadi
1,700 mwaka 2024.
Aidha,ameiomba Serikali kupitia maafisa Ugani kwenda kwa wakulima
kuwapa utaalam na mbinu za kilimo cha kisasa zitakazo wasaidia kuongeze
uzalishaji na kupata mavuno mengi.
Mkulima na Mwanachama wa Chama hicho Gisat Komba alisema,kwa muda wa
miaka minne uzalishaji wa kahawa umeongezeka na hali hiyo imetokana na
upatikanaji wa pembejeo za ruzuku zinazotolewa na Serikali ambazo
zimehamasisha watu wengi hasa vijana kujikita kwenye kilimo cha zao
hilo.
Hata hivyo
alisema,changamoto kubwa ni soko la uhakika kwani wanunuzi wana tabia ya
kujipangia bei ya kahawa bila kuwashirikisha wakulima jambo
linalowaumiza sana kwa sababu wanatumia gharama kubwa katika uzalishaji
wake.
Kwa upande
wake Afisa Mtendaji wa kata ya Utiri Libaba Gervas Libaba alisema,kata
hiyo ni maarufu kwa kilimo cha zao la kahawa na Wananchi wanajitahidi
sana kulima,lakini changamoto iliyopo ni upatikanaji wa pembejeo za
ruzuku.
Ametoa ombi
kwa Serikali kupitia Wakala wa Barabara za mijini na vijijini(Tarura)
Wilaya ya Mbinga,kukamilisha ujenzi wa Barabara ya lami ya Utiri-Mahende
kwa kiwango cha lami ili iweze kusaidia wakulima kusafirisha mazao
kupeleka sokoni kwa haraka kwani barabara hiyo inapita kwenye maeneo
yenye uzalishaji mkubwa wa kahawa.
Monday, March 03, 2025
WAKULIMA WANEEMEKEA NA ZAO LA KAHAWA,WASEMA MIKOPO YA PEMBEJEO IMEWASAIDIA KULIMA KWA TIJA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
MAKAMU WA RAIS DKT. PHILIP MPANGO AWATAKA WATANZANIA KUKEMEA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawak...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
(Picha na Yahya Charahani) Kwa wale waliokulia maeneo haya, hili ni jambo la kawaida ukitoka mjini, shambani sijui hadi wapi kote ni haya h...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment