
Akimkaribisha, Mhe. Waziri Mkuu kuzungumza na kuzindua NBC Kiganjani App, Mhe. Dkt. Nchemba aliipongeza NBC kwa ubunifu walioufanya na kwamba hatua hiyo si tu kwamba inaimarisha maendeleo ya sekta ya benki, bali pia inaendana na dhamira ya serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kujenga uchumi jumuishi unaowezesha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wananchi wote.
Aidha, Mhe. Dkt. Nchemba, aliipongeza Benki hiyo kwa kudhamini Ligi Kuu ya Tanzania Bara (NBCPL) ambayo kupitia udhamini wao imekuwa na msisimko mkubwa na kuiwezesha Tanzania kupanda viwango na kuwa ligi namba 4 kwa Ubora baranı Afrika.
No comments:
Post a Comment