Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ameishukuru Wizara ya ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi chini ya Waziri wake Mhe. Deogratius Ndejembi, kwa kusimamia na kuratibu vyema maandalizi ya sera ya ardhi, akiipongeza pia kwa kubadilika kiutendaji na kuwa kinara katika utatuzi wa changamoto za ardhi na maendeleo ya watu.
Rais Samia ametoa pongezi hizo mapema leo Jumatatu Machi 17, 2025 Jijini Dodoma, wakati akizindua sera ya ardhi ya mwaka 1995 toleo la mwaka 2023, sera ambayo inatajwa kuwa muarobaini wa changamoto mbalimbali za ardhi pamoja na silaha muhimu katika uongezaji wa thamani ya ardhi kwa maendeleo ya watanzania.
No comments:
Post a Comment