Saturday, January 31, 2026

DKT. MWIGULU KUMUWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA KWENYE HAFLA YA UTOAJI TUZO ZA UHIFADHI NA UTALII

 







WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 31, 2026 amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) ambapo anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika hafla ya Utoaji wa Tuzo za kitaifa za Uhifadhi na Utalii (The Serengeti Awards).

Pia, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu atatembelea Hifadhi ya Taifa ya Arusha ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais Dkt. Samia katika kukuza Utalii nchini.

No comments:

RAIS SAMIA AJUMUIKA NA WANANCHI WETE KWENYE FUTARI YA RAMADHANI PEMBA

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akijumuika na makundi mbalimbali ya Wananchi wa Wete kwenye F...