Saturday, April 22, 2017

WAZIRI KAIRUKI AZINDUA MAFUNZO YA UONGOZI KWA MAOFISA WA POLISI


 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala bora Mhe.Angelah Kairuki akizindua Programu ya Mafunzo ya Uongozi kwa Maofisa wa wa Jeshi la Polisi Mjini Dodoma yanayoendeshwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Chuo cha Aalto cha nchini Finland.Kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu na kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Prof. Joseph Semboja.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala bora Mhe.Angelah Kairuki (katikati), Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba (kushoto) na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu wakionyesha Vitabu vyenye Programu ya Mafunzo ya Uongozi kwa Maofisa wa Jeshi la Polisi yanayoendeshwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Chuo cha Aalto cha nchini Finland mjini Dodoma leo.Mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo Maofisa wa Polisi katika Uongozi.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Programu ya Mafunzo ya Uongozi kwa Maofisa wa Jeshi la Polisi Mjini Dodoma.Mafunzo hayo yanaendeshwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Chuo cha Aalto cha nchini Finland.Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala bora Mhe.Angelah Kairuki na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Prof. Joseph Semboja.
 Baadhi ya Maofisa wa Jeshi la Polisi waliopo katika Mafunzo ya Uongozi yanayoendeshwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Chuo cha Aalto cha nchini Finland.Mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo Maofisa wa Polisi katika Uongozi ambapo baada ya kuhitimu watatunukiwa “Post-Graduate Diploma in Leadership”.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala bora Mhe.Angelah Kairuki, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba na Viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na  Maofisa wa Jeshi la Polisi waliopo katika Mafunzo ya Uongozi yanayoendeshwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Chuo cha Aalto cha nchini Finland.Mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo Maofisa wa Polisi katika Uongozi ambapo baada ya kuhitimu watatunukiwa “Post-Graduate Diploma in Leadership”. Picha zote na Frank Geofray-Jeshi la Polisi

No comments: