Wednesday, May 19, 2010

Simba kubwa lamezwa na paka 1-0


Mabingwa wa soka Tanzania timu ya Simba leo imechapwa goli moja na timu ya Sofapaka mabingwa wa soka kutoka nchini Kenya katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Nyamirambo Kigali nchini Rwanda kuanzia saa tisa na nusu kwa saa za Tanzania katika mashindano ya vilabu bingwa Afrika Mashariki na Kati yanaoandaliwa na SECAFA.

Mjumbe wa kamati ya Utendaji na msemaji wa klabu hiyo aliyeshuhudia mchezo huo alijibu kwa kifupi katika simu kwamba tumefungwa goli moja, lakini habari zaidi zinasema mchezaji wa Sofapaka John Baraza ndiye aliyefunga goli hilo katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo.

Katika mchezo wa kwanza Simba iliifunga Timu ya Atraco magoli mawili kwa moja na sasa imebakiza mchezo mmoja ambao utaamua majaliwa ya timu hiyo kama itatinga kwenye robo fainali ama itaaga michuano hiyo

No comments:

MHE. NDEJEMBI AITAKA PURA KUWAJENGEA UWEZO WATANZANIA KUSHIRIKI MRADI WA LNG

Na Mwandishi Wetu, Morogoro Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratous Ndejembi, ameitaka Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) kuimar...