Wednesday, April 22, 2009

Afrika kusini wapiga kura leo



Wastahiki milioni 23 nchini Afrika Kusini leo wanapiga kura katika uchaguzi mkuu wa nne, ambapo chama kinachotawala ANC kinatarajiwa kushinda tena kwa kura nyingi.

Chama cha ANC kitakabiliwa na changamoto kubwa kutoka kwa vyama vya upinzani.Uchaguzi wa leo pia unatarajiwa kumpitisha rais wa chama hicho Jacob Zuma kuwa rais wa nchi vilevile.

Chama cha ANC kinatarajiwa kushinda katika uchaguzi huo mkuu na mgombe urais wa chama hicho Jacob Zuma pia anatazamiwa kupita kwa kura nyingi.

Watu walianza kupiga kura nchinini kote saa moja asubuhi kwenye vituo vya kupigia karibu alfu 20 katika zoezi litakalochukua muda wa saa 14.

No comments: