Sunday, March 09, 2008

Mufti Simba mgonjwa

Na Muhibu Said wa Mwananchi

MUFTI wa Tanzania, Sheikh Mkuu, Issa bin Shaaban Simba, amelazwa hospitali mkoani Arusha kwa takriban wiki mbii sasa, akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa kisukari.

Habari zilizopatikana jijini Dar es Salaam jana, zinaeleza kuwa, Mufti Simba amelazwa katika Hospitali ya Dk Mhando iliyoko mjini Arusha tangu Machi 2, mwaka huu.

Katibu wa Mufti, Sheikh Abdushakur Omar, alilithibitishia gazeti hili juzi na jana kuhusiana na kulazwa kwa Mufti Simba katika hospitali hiyo.Kwa kina zaidi soma Mwananchi la Kesho.

No comments: