Rais Jakaya Mrisho Kikwete alikagua barabara ya Lindi – Kibiti hadi Mingoyo pamoja na Daraja la Mbwemkuru, wakati akitoka Lindi kwenda Kilwa.
Kabla ya ukaguzi huo, Rais alipata taarifa ya maendeleo ya barabara hii muhimu kwa mikoa ya kusini na Daraja la Umoja (ambalo hakulikagua) kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Bw. Omar A. Chambo; ambaye amemueleza Rais kuhusu hatua mbalimbali zilizofikiwa katika ujenzi wa barabara hiyo. Ujenzi wa barabara ambao unafanyika kwa awamu, utakamilika mwishoni mwa mwaka huu wakati Daraja la Umoja linatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2008.
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari Msaidizi wa Rais,
20 Nov, 07.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
TRC KUONGEZA SAFARI ZA SGR DAR ES SALAAM–DODOMA 🚆🇹🇿
Habari njema kwa wasafiri! Shirika la Reli Tanzania (TRC) limetangaza kuongeza safari za treni ya SGR kati ya Dar es Salaam na Dodoma kua...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Nadhani mtakumbuka kibwagizo maarufu katika TV ambacho kinaimbwa perupe pepero perupe pepero hawa ni vijana wa Sisi Tambala waliokuwapo kati...
-
Mdau Julius Samwel hivi karibuni alikuwa huko Mwanza na hizi ndizo alizofanikiwa kutumegea, wadau hebu someni hicho kibao mniambie kuna nini...
No comments:
Post a Comment