Tuesday, August 21, 2007

Afrika Mashariki sarafu moja 2012



MARAIS wa nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) jana walikubaliana kuwa na sarafu moja na soko la pamoja kwa nchi za jumuiya hiyo ifikapo mwaka 2012.

Sambamba na uamuzi huo marais hao pia wamesogeza mbele uamuzi wa uharakishwaji wa kuanzishwa kwa Shirikisho la Afrika ya Mashariki.

Akisoma taarifa ya pamoja ya Marais hao mara baada ya kumalizika kwa mkutano wao katika Hoteli ya Ngurdoto jana, Katibu Mkuu EAC, Balozi Juma Mwapachu alisema wakuu hao wamefikia maamuzi hayo kutokana na maoni yaliyotolewa na wananchi wa nchi hizo na pia kuingizwa kwa Rwanda na Burundi kwenye jumuiya hiyo. Bonyeza hapa usome habari hii kwa kina katika gazeti letu la Mwananchi

No comments:

RAIS SAMIA AFUNGUA DARAJA LA J.P MAGUFULI: MLANGO WA MAENDELEO, HISTORIA MPYA YA KIGONGO–BUSISI

Misungwi, Mwanza – 19 Juni 2025 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan leo amefungua rasmi Daraja la ...