Wednesday, April 16, 2025

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIUNDOMBINU YA BARABARA YA DAR ES SALAAM – LINDI






Waziri Mkuu wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa, amefanya ziara ya kukagua miundombinu ya barabara kuu ya Dar es Salaam – Lindi, iliyoharibiwa kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Waziri Mkuu ameambatana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stegomena Tax, na Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, ambapo walijionea hali halisi ya barabara hiyo na hatua zinazochukuliwa ili kurekebisha na kuimarisha miundombinu hiyo muhimu.

Ziara hii ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita kuhakikisha miundombinu ya barabara inaboreshwa na kudumishwa ili kuwezesha usafirishaji salama na wa haraka kwa wananchi na bidhaa muhimu.

#Tanzania #Miundombinu #WaziriMkuu #Somanga #Ujenzi #SerikaliYaAwamuYaSita #Barabara

No comments:

RAIS SAMIA AKUTANA NA MJUMBE MAALUM WA JUMUIYA YA MADOLA IKULU DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 15 Aprili 2026, amekutana na kufanya mazungumzo na Mjumbe...