Tuesday, April 08, 2025

Dkt. Samia Aandika Historia Mpya Angola, Alihutubia Bunge la Taifa kwa Heshima ya Juu






 Luanda, Angola – Aprili 8, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweka alama muhimu katika uwanja wa diplomasia ya kikanda baada ya kulihutubia rasmi Bunge la Jamhuri ya Angola jijini Luanda, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kiserikali nchini humo.

Katika hotuba yake, Mhe. Rais Dkt. Samia alisisitiza juu ya umuhimu wa mshikamano wa Afrika katika kuimarisha uchumi, kukuza biashara ya ndani ya bara, na kuhimiza amani na ushirikiano kati ya mataifa. Aligusia pia ushirikiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Angola, hususan katika nyanja za elimu, afya, nishati, na uwekezaji.

“Ni wakati wetu sasa, kama mataifa ya Afrika, kusimama pamoja na kujenga mustakabali imara kwa vizazi vijavyo,” alieleza Mhe. Rais Samia mbele ya wabunge na viongozi waandamizi wa Serikali ya Angola.

Ziara hiyo inatarajiwa kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kuibua fursa mpya za kiuchumi na kijamii baina ya mataifa haya mawili marafiki.

No comments:

TRENI YA MWENDOKASI KUFIKA MWANZA 2028

  Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kutoka kulia),akizungumza baada ya kukagua daraja la kupitisha magari chn ya reli, l...