Friday, January 02, 2009

masikini chadema

VIONGOZI na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana waliachwa wakitafakari cha kufanya baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutupilia mbali rufaa ya mgombea wao kupinga kuenguliwa kwenye kinyang'anyiro cha ubunge wa Mbeya Vijijini.
Mgombea wa Chadema, Sambwee Shitambala alienguliwa na Tume ya Uchaguzi ya Mbeya Vijijini baada ya vyama vya CCM na CUF kuwasilisha pingamizi, vikidai kuwa alikiuka Sheria ya Uchaguzi kwa kuapa kwa wakili badala ya kwa hakimu. Mgombea huyo hakukubaliana na uamuzi huo na kukata rufaa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Lakini jana, mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Lewis Makame aliwaambia waandishi wa habari kwenye hoteli ya Mount Livingstone kuwa baada ya kutafakari mambo makuu manne, tume yake imetupilia mbali rufaa hiyo.
"Siwezi kueleza chochote kwa sasa kwa sababu tunahitaji kufanya consultations (mashauriano)," alisema mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alipotakiwa kuzungumzia hatua inayofuata baada ya Jaji Makame kutangaza uamuzi huo, habari hizi katupasha Brandy Nelson kutoka Mbeya.



No comments:

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la...