Monday, January 19, 2009

Mambo magumu chuo kikuu



JESHI la polisi limelazimika kuvunja maandamano ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, yaliyokuwa yameandaliwa na serikali ya wanafunzi iliyoripotiwa kutotambuliwa chuoni hapo (DARUSO).

Maandamano hayo yaliandaliwa kwa lengo la kupinga utaratibu wa udahili unaoendelea kwa kuwarudisha wanafunzi ambao wamekamilisha malipo yao yote.

Mwananchi ilishuhudia wanafunzi wakiwa nje ya chuo wakijiandaa kuandamana huku wakiwa wameshika mabango yanayochochea maandamano, huku wengine wakiwa wanaendelea na udahili kama kawaida.

"Tumeamua kuandamana leo uongozi uone wenyewe kwamba unachokifanya sio halali kwani kumrudisha kuendelea na masomo mwanafunzi mwenye uwezo na kumuacha asiye na uwezo ni sawa na ukandamizaji,"walisikika wanafunzi hao wakiwa wameshikilia mabango tayari kwa maandaamano." Habari ya Hussein Issa na Picha ya Emmanuel Herman.

No comments:

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la...