Wednesday, January 07, 2009

Kilimanjaro Stars yatisha Kampala


IKICHEZA soka safi na la kujiamini lililowalazimisha Waganda kuishangilia, Kilimanjaro Stars ilitandika bila huruma Rwanda kwa mabao 2-0 na kujisafishia njia, wakati wapinzani wa Uganda wakisambaratisha Somalia 4-0.
Ushindi huo umeifanya Stars kufikisha pointi sita na kuongoza kundi kwa muda, huku kiungo wake, Athuman Idd akinyemelea ufungaji bora kwa mabao mawili aliyonayo.
Stars ambayo ilianza mchezo huo kwa kushambulia kwa nguvu, iliandika bao la kwanza dakika ya nane kupitia kwa winga wake Mrisho Ngassa ambaye alipiga 'tiktak' iliyogonga besela na kutinga wavuni.
Rwanda ambayo ilicheza soka la pasi nyingi fupi fupi na kushambulia kwa kushtukiza, ilijipanga na kupandisha shambulizi kali dakika ya 10 na kupangua ukuta wa Stars, lakini Lomani Jean akachachawa na kupaisha.
Washambuliaji wa Stars walizidi kuishambulia Rwanda, ambapo dakika 23 Henry Joseph alipiga shuti kipa akatema, lakini Mrisho Ngassa akaichelewa kumalizia.
Stars ambayo wachezaji wake walikuwa wakikaba kwa nguvu, kwa kujiamini na kutowapa nafasi Rwandakukaa na mpira, ilizidi kushambulia huku wachezajiwake wakionana vizuri na kuandika bao la pili dakika ya37 kupitia kwa Athuman Iddi 'chuji'.Taarifa ya Michael Momburi.

No comments:

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la...