WAFANYAKAZI wa Benki ya NMB jana walirejea kazini na kuendelea kutoa huduma baada ya kubatilishwa kwa mgomo ulioanza Jumatatu wiki hii, huku kukiwa na kasoro kadhaa katika huduma ambazo zililalamikiwa na wateja wa benki hiyo.Katika tawi la Bank House kulikuwa na msururu mrefu wa wateja walio kuwa wamejipanga kwenye mstari wakisubiri kupatiwa huduma ambayo ilisitishwa tangu Jumatatu, huku mashine za kutolea fedha 'ATM' zikiwa hazifanyi kazi.Kwa mujibu wa wateja waliokuwapo maeneo hayo, mashine hizo zilikuwa hazifanyi kazi tangu walipofika asubuhi na kwamba, walipowasiliana na uongozi waliwaambia hawajui tatizo litatatuliwa saa ngapi.Lakini ilipofika saa 4:00 asubuhi baadhi ya ATM za makao makuu ya benki hiyo, zilianza kufanya kazi kwa kusuasua na baada ya muda zilirejea katika hali yake ya kawaida na watu wakaanza kuchukua fedha.Habari Kwa Hisani Ya Mzee Wa Sumo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
RAIS SAMIA AFUNGUA DARAJA LA J.P MAGUFULI: MLANGO WA MAENDELEO, HISTORIA MPYA YA KIGONGO–BUSISI
Misungwi, Mwanza – 19 Juni 2025 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan leo amefungua rasmi Daraja la ...
.jpeg)
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
(Picha na Yahya Charahani) Katika kijiji cha Mwanjoro, wilayani Meatu – Shinyanga, maisha bado yanapumulia kwenye nyumba za udongo na mapaa...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment