Friday, December 29, 2006

Richmond mpya ni kanzu mpya, sheikh wa zamani?

KILA kona ulikuwa ukipita rat a tat!! hiyo si mitaa ya mijini, peke yake bali nchi nzima. Tatizo mgawo wa umeme au kiufupi tuseme ukosefu wa umeme umekuwa Kero!

Kero kwa sababu umesababisha wengi kukosa ajira, kiwango cha uhalifu kuongezeka, umasikini, wizi, uchumi kushuka na kila kitu kibaya unachokijua msomaji.

Wiki hii Shirika la Umeme likatangaza kuwa mgawo sasa basi, sababu kubwa la kufa kimya kimya kwa mgawo huu ni kujaa kwa mabwawa ya Mtera na Kidatu. Inasikitisha!

Inanisikitisha siyo kwa sababu maji yamejaa au kwa kuwa, eti siwatakii watanzania maisha bora na mema, bali ni kutokana na kuwa katika kiwango cha chini cha maendeleo cha kutegemea nature, wakati uwezo tunao wa kutotegemea nature. Unaweza kuendelea zaidi hapakwa kubonya hapa