TBS YATOA ELIMU MAONESHO YA SABA YA MIFUKO NA PROGRAMU ZA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI SINGIDA

 



Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kutoa elimu muhimu kuhusu ubora wa bidhaa katika Maonesho ya Saba ya Mifuko na Programu za Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi yaliyofanyika katika viwanja vya Bombadier, mkoani Singida. 

Maonesho haya yaliyoanza Septemba 8, 2024, na kumalizika Septemba 14, 2024, yalikuwa na lengo la kuimarisha uelewa wa wajasiriamali na wananchi kuhusu ubora wa bidhaa na ushiriki wa TBS.

Afisa Mtoa Elimu wa TBS, Sileja Lushibika, alieleza kuwa shirika hilo limejitolea kutoa elimu kwa wajasiriamali na wageni waliotembelea banda la TBS. Alisisitiza umuhimu wa kuwa na alama ya ubora ya TBS katika bidhaa, akionyesha jinsi alama hii inavyosaidia kuboresha viwango vya bidhaa na kukuza imani ya watumiaji.

Ushiriki wa TBS katika maonesho haya ulionyesha dhamira yake ya kuunga mkono juhudi za kiuchumi za wananchi, huku ukitoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya sekta ya viwanda na biashara nchini Tanzania.

Comments