Friday, October 05, 2012

KESI YA ELIZABETH 'LULU' MICHAEL YAGONGA MWAMBA MAHAKAMA YA RUFAA, YARUDISHWA MAHAKAMA YA KISUTU KUANZA UPYA...!!!


KESI ya mauaji inayomkabili msanii wa filamu za maigizo nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’ anayedaiwa kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba ‘The Great’ ambayo leo ilitakiwa kutolewa maamuzi ya umri na Mahakama ya Rufaa imerudishwa mahakama ya Kisutu kuanza upya. 

Akitoa maamuzi hayo Naibu Msajili wa Mahakama hiyo yenye maamuzi ya mwisho hapa nchini, Zahra Marume amesema utaratibu uliotumika kuifikisha kesi hiyo mahakamani hapo ulikuwa na makosa hivyo kuamuru kesi hiyo kurudi mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam.

No comments:

TRENI YA MWENDOKASI KUFIKA MWANZA 2028

  Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kutoka kulia),akizungumza baada ya kukagua daraja la kupitisha magari chn ya reli, l...