Mkurugenzi Mkuu TAWIRI Dkt. Eblate Mjingo ni miongoni mwa Wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii wanaoshiriki mkutano wa kimkakati unaowajumuisha watendaji wote wa Wizara hiyo kujadili namna bora ya kuboresha utendaji ili kufikia malengo tarajiwa hususani ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.
Akifungua mkutano huo, Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) ameitaka Menejimenti ya Wizara na Wakuu wa Taasisi za Wizara hiyo kuongeza ubunifu sambamba na kuzigeuza changamoto za kiutendaji kuwa fursa za matokeo chanya kwa wananchi.
Amefafanua kuwa sekta ya Maliasili na Utalii ni moja ya sekta za mageuzi hapa nchini kutokana na mchango wake katika kuchochea ukuaji wa uchumi, kuongeza ajira, mapato ya fedha za kigeni na maendeleo ya jamii kwa ujumla.
“ Utendaji katika sekta hii ni lazima uwe wa kimkakati na unaozingatia utu kwa kuwa unagusa sehemu kubwa ya maisha ya wananchi,” amehimiza Dkt. Kijaji
Mkutano huo unaoendelea kwa siku nne katika Hifadhi ya Taifa ya Nyerere ni fursa kwa Menejimenti na viongozi wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kubadilishana uzoefu na kujifunza mbinu bora za kuendeleza uhifadhi na utalii.
TAWIRI ni injini katika sekta ya Uhifadhi na Utalii





No comments:
Post a Comment