Monday, July 23, 2007

Kupima tumepima Ukimwi, enhee nini kinafuata?

LAZIMA unapoanza kitu kuwe na sehemu ya kuanzia. Hilo halipingiki, unaweza kuanzia mwanzo ukaenda mwisho na pia unaweza kuanzia katikati na kisha kumalizia mwishoni, pia waweza kuanzia mwisho. Inawezekana.

Serikali yetu imeanzia sehemu fulani na sasa inasonga mbele, ndiyo maana imetangaza kampeni ya nchi nzima kupima virusi vya Ukimwi, akajitokeza shupavu huyu kwa mifano yake, Rais Jakaya Kikwete , akapima akatangaza, matokeo akaondoka.

Wakaja wengine wakapima wakaondoka. Wabunge nao wakajitutumua kupima jana, japo wengine kwa shingo upande wamekwenda, wengine nao wanaenda kupima sababu tu wenzao wamepima na kisha wanaingia mitini.

Nafurahi kwamba na sisi wavuja jasho tulikuwapo katika foleni ndefu tukionyesha kujali afya zetu, tumepima na tumeondoka, majibu yetu tunayajua wenyewe. Bonyeza hapaupate taarifa kwa kina zaidi.

No comments: