Monday, July 16, 2007
Tanzania bila Ukimwi Inawezekana
Mwishoni mwa wiki, Rais Kikwete aliongoza wananchi na viongozi wenzake wa serikali na wa vyama vya kisiasa katika kampeni zilizoanza za kupima Virusi vya Ukimwi. Kitendo cha Rais Kikwete na mkewe (Pichani) na viongozi wengine wote ni kitendo cha kijasiri ambacho hakina budi kupongezwa na kuungwa mkono. Ingawa ni kitendo kilichochelewa lakini kufanyika kwake kumekuja wakati muafaka katika kukoleza mapambano dhidi ya ugojwa huu unaoangamiza jamii yetu na kuweka hatima ya baadaye ya taifa letu mashakani.
Ingawa pia haitoshi kwa viongozi kupima tu bali pia kutangaza matokeo ya vipimo hivyo hadharani ili wawe watakaogundulika wameambukizwa siyo tu wawe mfano wa kupima tu bali pia wawe mfano wa watu wanaoishi kwa matumaini na kuendelea na majukumu yao badala ya kuonekana kuwa kugundulika kuwa na VVU ni leseni ya kifo.
Hata hivyo, katika upande wa kauli mbiu ya 'Tanzania Bila Ukimwi Inawezekana' kunaonekana kuwapo utata wa aina fulani. Moja sababu Ukimwi upo na kwa maana hiyo haujapatiwa dawa na kwa maana hiyo wenye ukimwi wapo. Kwa maana hiyo kusema tanzania bila ukimwi inawezekana ni kuwanyanyapaa wenye virusi. Je wanapopatikana na ukimwi ina maana serikali itafanyaje?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
SAMIA AZINDUA MKUTANO WA KIMATAIFA WA WFNS, ATEMBELEA MAONESHO YA SEKTA YA AFYA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akitembelea mabanda ya maonesho ya wadau wa Sekta ya Afya kabla ya k...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Pascal Mayalla akiwa katika chumba cha wagonjwa Daraja la kwanza katika hospitali ya mkoa wa Dodoma ambako amelazwa kwa matibabu baada ya ku...
No comments:
Post a Comment