Saturday, April 09, 2016

MWANAMUZIKI NDANDA KOSOVO AFARIKI DUNIA


Globu ya jamii imepokea taarifa za Mwanamuziki mkongwe aliyewahi kujizolea sifa kem kem katika miondoko ya dansi hapa  nchini wakati akiwa na bendi ya FM miaka ya nyuma kabla ya kujiengua na kuunda kundi lake lililojulikana kwa jina la Stono Musica a.k.a Wajela Jela Gwaa, Ndanda Cosovo ‘Kichaa’ amefariki Dunia leo asubuhi,baada ya kuugua kwa siku chache

Taarifa kutoka kwa mtu wake wa Karibu ambaye pia ni Mwanamuziki wa dansi,Kardinal Gento amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na ameongeza kuwa Ndanda Kosovo amefariki dunia leo asubuhi katika hospitali ya Muhimbili alikokuwa amelazwa tangu juzi kutokana na matatizo ya tumbo.
*Tutazidi kupeana taarifa zaidi hapa hapa kadiri zitakavyokuwa zikiingia*
Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi-AMIN

No comments:

MAJALIWA: FANYENI TAFITI ZENYE TIJA KWA WANANCHI

Dar es Salaam, 18 Juni 2025 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, ametoa wito kwa watafiti na wapangaji wa s...