Tuesday, August 24, 2010

CUF yapata pigo wagombea wawili wafa


Wagombea wawili wa Chama cha Wananchi (CUF) wamefariki dunia jana visiwani Zanzibar katika matukio tofauti.Waliofariki dunia ni alikuwa Mwakilishi wa Jimbo la Kojani (CUF), Omar Ali Jadi (55) Mkoa wa Kaskazini Pemba na Mwalimu Shani Hamada Shani ambaye ni mgombea wa udiwani wa chama hicho katika Jimbo la Kikwajuni. Jadi alikuwa akiugua ugonjwa wa kisukari na kwamba alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya figo. Shani alifariki dunia baada ya kugongwa na gari wakati akielekea kuchukua fomu katika Tume ya Uchaguzi Zanzibar(ZEC), eneo la Maisara.Habari ya Salma Said, Zanzibar. SOURCE: CUF

No comments:

RAIS SAMIA ALETA FURAHA NA MATUMAINI BUSEGA, AFUNGUA MRADI MKUBWA WA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

Shamrashamra za ufunguzi wa mradi wa Maji na Usafi wa Mazingira wa Lamadi, Wilayani Busega mkoani Simiyu tarehe 19 Juni, 2025 Rais wa Jamhur...