Wednesday, November 12, 2008

Chuo Kikuu watimuliwa









UONGOZI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kampasi ya Mlimani umewasimamisha masomo wanafunzi wa shahada za kwanza kwa muda usiojulikana.

Hatua hiyo imekuja baada ya wanafunzi hao kukaidi amri ya chuo pamoja na ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Prof Jumanne Maghembe, iliyowataka kusitisha mgomo na kurudi madarasani wakati wizara ikishughulikia madai yao.

Kufuatia hatua hiyo, Rais wa Serikali ya wanafunzi wa chuo hicho, Anthony Machibya, aliwatangazia wanafunzi wenzake juu ya kusimamishwa huko na kusisitiza kuwa, pamoja na kufukuzwa chuoni hapo, lakini watakaporudi wataendeleza harakati za kudai haki yao mpaka watakapoipata.

No comments:

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la...