Wednesday, May 19, 2010

Simba kubwa lamezwa na paka 1-0


Mabingwa wa soka Tanzania timu ya Simba leo imechapwa goli moja na timu ya Sofapaka mabingwa wa soka kutoka nchini Kenya katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Nyamirambo Kigali nchini Rwanda kuanzia saa tisa na nusu kwa saa za Tanzania katika mashindano ya vilabu bingwa Afrika Mashariki na Kati yanaoandaliwa na SECAFA.

Mjumbe wa kamati ya Utendaji na msemaji wa klabu hiyo aliyeshuhudia mchezo huo alijibu kwa kifupi katika simu kwamba tumefungwa goli moja, lakini habari zaidi zinasema mchezaji wa Sofapaka John Baraza ndiye aliyefunga goli hilo katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo.

Katika mchezo wa kwanza Simba iliifunga Timu ya Atraco magoli mawili kwa moja na sasa imebakiza mchezo mmoja ambao utaamua majaliwa ya timu hiyo kama itatinga kwenye robo fainali ama itaaga michuano hiyo

PROGRAMU YA MAFUNZO YA UONGOZI KWA JESHI LA POLISI




The IGP and the British High Commissioner, Diane Corner; Picture named (Round-table discussion) shows the British High Commissioner, Diane Corner (right) listening to the IGP and left is an official from DFID.

***************************************************************************************
Wiki hii Balozi wa Uingereza hapa nchini, Diane Corner, pamoja na Inspecta Generali wa Polisi, (IGP) Saidi Mwema wamezindua programu ya mafunzo ya uongozi kwa Jeshi la Polisi la Tanzania inayodhaminiwa na Serikali ya Uingereza. Mafunzo hayo, ambayo yataendeshwa na Mamlaka ya Kitaifa ya Kuboresha Idara ya Polisi ya Uingereza (NPIA) pamoja na ile ya Hampshire kwa muda wa miezi tisa (kuanzia mwezi ujao), yatakuwa na lengo la kubadilishana uzoefu na mbinu bora - kwa kujikita zaidi katika masuala ya kiuongozi na kimenejimenti.

“Mafunzo hayo ni muhimu sana kwetu hasa kwa kipindi hiki cha maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao, lakini pia ni muhimu zaidi katika jukumu zima la kudumisha amani hapa nchini,” alishukuru IGP Saidi Mwema.

Ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mafunzo hayo, hivi karibuni Ubalozi wa Uingereza uliwapeleka kuhudhuria mafunzo huko NPIA na Hampshire nchini Uingereza IGP Saidi Mwema pamoja na maafisa wengine wa Jeshi la Polisi la Tanzania, ambao ni Kamishna wa Polisi anayeshughulikia Utawala na Rasilimali, Clodwig Mtweve, Mkuu wa Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Abdulrahman Kaniki na Kamanda wa Chuo cha Polisi Dar es Salaam, Elice Mapunda.

Ujumbe huo ulipata mafunzo huko NPIA katika masuala ya utekelezaji oparesheni za kipolisi kwa kuzingatia haki za binaadamu, utoaji huduma za kipolisi, uchunguzi, utafiti na masuala mbalimbali ya kiutawala. Pia walipata fursa ya kujiunga na jeshi la Polisi Hampshire na kufanya doria, pamoja na kujenga ujirani mwema na jamii zinazozunguka. Uzoefu huu umewezesha kujenga ushirikiano wa karibu zaidi kati ya Jeshi la Polisi la Tanzania na Hampshire, na hivyo kupanua wigo wa kujifunza kutoka pande zote mbili.

"Ninayo furaha kubwa kuzindua programu hii ya Polisi. Mafunzo haya ni mchango mkubwa katika maboresho ya sekta ya sheria, ambayo sisi pamoja na Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DFID) tunafadhili. Ninatumaini ya kuwa mafunzo haya yatakuza ushirikiano baina ya Jeshi la Polisi la Tanzania na lile la Uingereza ambao kila upande utakuwa na mengi ya kujifunza kutoka kwa mwenzake,” alisema Balozi Corner.
___________________________________________________________________________

Tuesday, May 18, 2010

Uchuuzi wa samaki


Akina mama wachuuzi wa samaki katika ziwa Ndori wilayani Babati, akina mama hawa wanauza samaki mmoja shillingi 100 na wamekuwa wakisubiri ziwani samaki hao mara baada ya kuvuliwa. Picha na Mussa Juma

Monday, May 17, 2010

U.S. and Tanzania Launch Medication Assisted Therapy Program for Drug Users


From right: U.S. Ambassador Alfonso E. Lenhardt, Phillip Marmo, Minister of State in Tanzania's Prime Minister's Office - Coordination & Parliamentary Affairs and U.S. Global AIDS Coordinator Ambassador Eric Goosby - announced the establishment of the first Medication Assisted Therapy (MAT) program for drug users in sub-Saharan Africa. Services will be initiated shortly at a site in Dar es Salaam to be followed by two more sites in Zanzibar and Dar es Salaam. These services are a crucial part of HIV and health services because MAT allows drug users to return to a regular, productive and healthier life. (Photo courtesy of the American Embassy)

Mdau Ernest alamba Nondozzz ya master of IT Project Management


Vincent Ernest akiwa na washikaji zake Stephen Kassambo kushoto na Godwin Meghji wa kulia baada ya kula Nondo zake University of Maryland huko Maryland. Kalamba master of IT Project Management. Jamaa wanakata nondozzz si mchezo hawa Blogu ya Charaz blogspot na timu yake wanamtakia kila la kheri Ernest kwa kula nondozzzz

Rais Kikwete azindua Benjamin William Mkapa Special Economic Zone


Rais Jakaya Kikwete akiwa na Rais mstaafu awamu ya tatu Benjamin William Mkapa wakitembelea baadhi ya maeneo ya ukanda maalumu wa uwekezaji kwaajili ya kuuza nje lijulianalo kama (Benjamin William mkapa Special Economic Zone) huko Mabibi,Ubungo jijini Dar es Salaam, leo asubuhi. Rais Kikwete alifungua rasmi ukanda huo mpya wa uwekezaji (Picha na Freddy Maro)

Sunday, May 16, 2010

Flora Martine ndiye miss IFM 2010


Washiriki wa miss IFM wakijimwaya mwaya jukwaani

Miss IFM 2010,Flora Martin kati na mshindi wa pili Judith Osima (shoto) na wa tatu ni Esther Emmanuel wakiwa wampozi mara baada ya kuibuka kidedea kwenye kinyang'anyiro cha shindano hilo lililokuwa na ushindani mkubwa miongoni mwa washiriki hao.Picha za Silvan Kiwale.

NANENANE 2026: RAIS SAMIA ASISITIZA KILIMO CHA TIJA, MASOKO NA TEKNOLOJIA KUELEKEA DIRA 2050

  Dodoma, Agosti 8, 2026 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameongoza kilele cha Maadhimisho ya Nanena...