Sunday, May 16, 2010

Harambaee ya kuichangia CCM mkoa wa Kilimanjaro yafana


Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro Mama Vicky Nsilo Swai akimzawadia Rais Kikwete Ramani ya Afrika yenye kuwaonyesha wanyama watano wakubwa(the big five) Simba,Tembo,Faru, Nyati na Chui muda mfupi baada ya kumalizika hafla ya kuchangia fedha kwaajili ya Uchaguzi Mkuu CCM mkoa wa Kilimanjaro jana jioni katika hoteli ya Golden Tulip jijii Dar es salaam.Katika hafla hiyo Zaidi ya shilingi milioni mia mbili zilipatikana ikiwemi ahadi na fedha taslimu.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro Mama Vicky Nsilo Swai akimzawadia Rais Kikwete Ramani ya Afrika yenye kuwaonyesha wanyama watano wakubwa(the big five) Simba,Tembo,Faru, Nyati na Chui muda mfupi baada ya kumalizika hafla ya kuchangia fedha kwaajili ya Uchaguzi Mkuu CCM mkoa wa Kilimanjaro jana jioni katika hoteli ya Golden Tulip jijii Dar es salaam.Katika hafla hiyo Zaidi ya shilingi milioni mia mbili zilipatikana ikiwemi ahadi na fedha taslimu.

Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua harambee ya kuchangia fedha uchaguzi mkuu CCM mkoa wa Kilimanjaro iliyofanyika katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam jana jioni.Picha kwa hisani ya Freddy Maro.

Saturday, May 15, 2010

Kili Music awards

Sean-Kingston performance Sat May 15, 2010 at Diamond Jubilee, Dar es Salaam.

Mrisho mpoto akionesha tuzo yake ya wimbo bora wenye asili ya Kitanzania uitwao nikipata Nauli

Mdau mkubwa wa timu ya Yanga,Bw. Madega akikamkabidhi Diamond tuzo yake ya wimbo bora wa R&B uitwao Kamwambie

Mzee Yusuf akionyesha tuzo yake ya Mtunzi bora wa nyimbo, na pia kundi lake la Jahazi lilinyakua tuzo ya albamu bora ya taarabu iliyoitwa Daktari wa Mapenzi

Gadner Habash akimpongeza mkewe Lady Jay Dee kwa kupata tuzo ya Female Artist of the Year ambayo alipokea kwa niaba.

Thursday, May 13, 2010

Ajali ya ndege yaua 104 Libya


Mabaki ya ndege aina ya Air Bus 330, iliyopata ajali

Maafisa nchini Libya wameripoti kuwa, ndege ya abiria imeanguka katika uwanja wa ndege mjini Tripoli na kuua takriban watu 104.

Ndege hiyo inayomilikiwa na shirika la ndege la Afriqiyah ilikuwa safarini kutoka mjini Johannesburg, Afrika Kusini.

Maafisa wamesema ilianguka wakati ikjaribu kutua karibu na uwanja huo.Takriban abiria 93 walikuwa ndani ya ndege hiyo pamoja na wafanyakazi kadhaa wa ndege hiyo aina ya Air Bus 330.

Watu hao wanaaminika kutoka mataifa mbalimbali zikiwemo nchi za Uingereza na Afrika Kusini.Wafanyikazi 11 wa ndege hiyo wameripotiwa kuwa raia wa Libya.

Ndege hiyo ilitarajiwa kuelekea kwenye uwanja wa ndege wa Gatwick mjini London baada ya kusimama kwa muda mjini Tripoli.

Magari ya kuwabebea wagonjwa yameonekana kuelekea kwenye uwanja huo. Shirika la ndege la Afriqiyah lilianzishwa nchini Lybia mwaka wa 2001.

CHANZO: bbcswahili.com

Wednesday, May 12, 2010

Sanamu iliyoibwa Bongo na Waswiss yarejeshwa


Sanamu ya Makonde ambacho kiliibiwa kutoka Makumbusha ya Taifa Dar es Salaam, ilibwa kati ya mwaka 1984-1986 pamoja na baadhi ya mikusanyo ya mila na Sanamu hiyo kilikamatwa nchini Uswisi na hatimaye kurejeshwa hapa nchini.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga akipokea Sanamu hiyo kutoka kwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo Dk.Ladislaus Komba.Kinyago hicho kilikutwa katika makumbusho ya Barbier Murller nchini Switzerland. Sanamu hii ilikabidhiwa nchini Mei 9 2010 na uongozi wa Makumbusho hiyo ya Switzerland

Rais Kikwete mgeni rasmi harambee ya CCM


MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA KILIMANJARO, MAMA NSILO SWAI AKIONGEA KUHUSU HARAMBEE YA KUCHANGIA CHAMA HICHO MKOANI KILIMANJARO ITAKAYAYOFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM (PICHA NA MPIGA PICHA WETU)

********************************************************************************

RAIS Jakaya Kikwete atakuwa mgeni rasmi kwenye chakula cha hisani kuchangia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kilimanjaro itakayofanyika jijini Dar es Salaam kesho.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro Nsilo Swai alisema kuwa harambee hiyo ina lengo la kuchangisha fedha za kugharamia shughuli za uchaguzi mkuu mwaka huu na kuendeleza chama.

Harambee hiyo itafanyika kwenye hoteli ya Golden Tulip ambapo viongozi wa juu wa chama na serikali, wawakilishi wa mashirika wabunge wote wa CCM wa Mkoa wa Kilimanjaro, wakereketwa wa CCM, pamoja na wafanyabiashara wadogo na wakubwa kutoka mkoa wa Kilimanjaro watahudhuria.

Mama Nsilo Swai alisema kuwa harambee hiyo itaanza saa moja usiku ambapo kiingilio itakuwa ni Sh 50,000 kwa mtu mmoja na Sh 60,000 kwa Bibi na Bwana.

“Nawaomba wanaKilimanjaro walioko Dar es salaam na wakereketwa wa Chama Cha Mapinduzi wote kwa ujumla kuhudhuria na kuchangia chama chao”, alisema.

Swai aliongeza kuwa mbali na uchangiaji fedha taslimu pia kutakuwa na mnada wa vitu mbalimbali kama sehemu ya uchangiaji katika shughuli hiyo. Harambee hiyo itapambwa na burudani kutoka kwa bendi ya Msondo Ngoma ya jijini Dar es Salaam.

Two Tanzanians Participate in FORTUNE/U.S. State Department Women's Mentoring Partnership Program

Irene Kiwia, Managing Director of Frontline Management Company, a communication company that deals with public relations, event management and corporate communication and Modesta Mahiga, Managing Director, Professional Approach Limited, a company that deals with human resource capacity building consultancy firm, are in the United States to participate in a four-week FORTUNE/U.S. State Department Global Women's Mentoring Partnership. This program draws on the knowledge and expertise of America’s most accomplished leaders to empower aspiring women professionals across the globe. From left Ms. Mahiga, Ms. Kiwia and Ms. Karen Grissette, U.S. Embassy Deputy Public Affairs Officer at the chancery before their departure. (Photo courtesy of the American Embassy)

Daraja la Umoja lazinduliwa



Rais Jakaya Kikwete na Rais Guebuza wa Msumbiji wakisalimia wanachi katika daraja la Umoja linalounganisha Tanzania na Msumbiji kijiji cha Mtambaswala mkoani Mtwara wakati wa uzinduzi wa daraja hilo mapema leo





Leo marais Jakaya Kikwete na mwenzake Armando Guebuza wa Msumbiji, wamezindua Daraja la Umoja linaloziunganisha nchi hizi mbili kama ishara ya mshikamano na udugu wa kihistoria uliopo baina ya watu wa nchi hizo.

Daraja hilo lenye urefu wa meta 720 na upana wa meta 13.5 ni kiunganishi kizuri kwa nchi hizi na tunatarajia litatumiwa kwa maslahi ya watu wa Tanzania na Msumbiji, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikabiliwa na matatizo ya barabara. Ni ukombozi kwao.

Wazo hilo lililotolewa na marais waasisi; marehemu Julius Nyerere wa Tanzania na Samora Machel wa Msumbiji mwaka 1975 na kutekelezwa na viongozi waliofuata na kukamilishwa na waliopo sasa.

Wazo limesimamiwa na mkandarasi M/s China Geo- Engineering ambaye alisimamiwa na Mhandisi Mshauri NorConsult kutoka Norway, kwa uvumilivu wao na juhudi kubwa za kukamilisha daraja hilo, ambalo litabaki kuwa alama ya uhusiano mzuri na wa kihistoria wa nchi hizi.

Ili kuenzi wazo hili na kuheshimu uamuzi wa kulijenga, ni vizuri sasa wananchi wakawa walinzi wa wenzao, dhidi ya hujuma yoyote itakayofanywa kwenye daraja hilo, hasa hii ya ukataji vyuma kwa ajili ya tamaa ya kujipatia kipato cha haraka haraka.

NANENANE 2026: RAIS SAMIA ASISITIZA KILIMO CHA TIJA, MASOKO NA TEKNOLOJIA KUELEKEA DIRA 2050

  Dodoma, Agosti 8, 2026 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameongoza kilele cha Maadhimisho ya Nanena...