Tuesday, December 05, 2006

Huku ni kijijini Usiulize, Meatu



Maisha haya unayakumbuka?

Kunakopikwa masuala yote duniani hapa



Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa

Balozi Mahiga

Balozi wa Tanzania UN, Dk Augustine Mahiga

BALOZI DK. MAHIGA AKITOA MUHTASARI WA MKUTANO WA UN

Jopo la waandishi wa habari waliopo jijini New York wakimsikiliza Balozi wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa, Dk Augustine Mahiga.

Balozi Mahiga Mkutanoni



Jana Balozi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Dk Augustino Mahiga alilihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, kubwa likiwa kupiga vita biashara haramu ya almasi za damu. (Picha imepigwa na Athmani Hamisi)

Ndani ya kikao cha Baraza Kuu la Usalama la UN



Balozi Augustine Mahiga (aliyeketi) akizungumza jambo na Wasaidizi wake baada ya kumaliza kikao cha jana kilichozungumzia masuala ya ukomeshaji silah ndogo ndogo.

Saturday, December 02, 2006

Mkutano wa TED Global kufanyika Tanzania




























MKUTANO mkubwa duniani wa kila mwaka wa masuala ya teknolojia, (technology, entertaiment, design) unaowashirikisha watu maarufu duniani wanaozidi 1000, utafanyika Tanzania kwa mara ya kwanza.

Akitangaza rasmi jana jijini hapa New York, Mkurugenzi wa Programu wa TED, Emeka Okafor (pichani kushoto), Emeka unaweza kumfikia kwa kubonya hapaalisema mkutano huo umeamuliwa kufanyika rasmi Tanzania kutokana na mafanikio makubwa iliyoyapata Tanzania katika nyanja mbalimbali ikiwamo uchumi na siasa.

“Hatujaichhagua Tanzania kwa bahati mbaya au kwa upendeleo tu, au eti tunataka kutazama wanyama wa mbugani, la hasha , bali ni kwasababu ya mafanikio makubwa nchi hiyo iliyoyapata kiuchumi na kisiasa,”alisema Okafor.

Kama wewe unajihusisha na masuala ya teknolojia na biashara, tuma maombi yako ili uweze kuhudhuria mkutano huu. Watu utakaokutana nao ana na mada zinazojadiliwa kwenye mikutano ya TED, utasuuzika nafsi yako.

MTUHUMIWA WA “KUFUTA MADENI” YA MIKOPO AKIRI KOSA, AHUKUMIWA KIGOMA

KIGOMA, Septemba 4, 2026 — Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kigoma imemhukumu Nicholaus Komba Mahitana maarufu kama Abdallah Mahimbo baad...