Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limezindua rasmi mauzo ya nyumba katika miradi mikubwa ya kisasa jijini Dar es Salaam na mikoa ya Tanga na Tabora.
Uzinduzi huo umefanyika Makao Makuu ya NHC, Kambarage House,
ukiongozwa na Meneja Mauzo na Masoko, Deogratius Batakanwa, ambaye
amesema hatua hii inalenga kuhakikisha Watanzania wanapata makazi bora,
ya kisasa na yenye thamani ya kudumu.
Amesema kuwa Jijini Dar es Salaam, NHC imezindua mauzo ya nyumba
kwenye mradi wa Boulevard Residence yenye nyumba za chumba kimoja (37.7
sqm), vyumba viwili (103.5 sqm) na vyumba vitatu (124.2 sqm), Katika
mradi huu mauzo yanaanzia shilingi milioni 248 yakiwa na VAT.
Kwa upande wa nyumba za mradi wa Samia Housing Kijichi Residence
wenye nyumba za chumba kimoja (32.02 sqm), vyumba viwili (62.70 sqm) na
vyumba vitatu (95.30 sqm). Katika mradi huu mauzo yanaanzia shilingi
milioni 112 yakiwa na VAT.
Kwa mkoa wa Tanga, NHC inatangaza mauzo ya nyumba mradi wa
Mkwakwani Plaza zenye vyumba viwili (80 sqm) na vitatu (108 sqm),Katika
mradi huu mauzo yanaanzia shilingi milioni 185 yakiwa na VAT, huku
mkoani Tabora ikitangaza kuuza nyumba kwenye mradi wa Tabora Plaza yenye
vyumba viwili (95 sqm) na vitatu (124 sqm). Katika mradi huu mauzo
yanaanzia shilingi milioni 225 yakiwa na VAT.
Bei za nyumba hizi zimepangwa kwa kuzingatia mahitaji ya Watanzania
wa kipato tofauti, na lengo kuu ni kutoa fursa kwa kila mmoja kumiliki
nyumba bora. Wateja wanaweza kupata huduma kwa kupiga namba ya huduma
0736 114 433 au kuwasiliana moja kwa moja na maafisa mauzo walioteuliwa.
Batakanwa amesema NHC itaendelea kujenga taifa kwa kutoa makazi
bora na kuwataka Watanzania kutumia fursa ya kipekee ya kumiliki nyumba
katika maeneo yenye miundombinu bora na mazingira salama.
Kupitia miradi hii, NHC imeonesha dhamira ya kuharakisha maendeleo
ya makazi nchini na kuwapa wananchi fursa ya kuishi na kufanya biashara
katika mazingira ya kisasa.
No comments:
Post a Comment