Wednesday, June 30, 2010

Muda wa usajili line waongezwa



SERIKALI imeongeza muda wa usajili wa simu za viganjani ili kuwezesha wananchi wengi waweze kujisajili baada ` kusikiliza kilio chao ili kuwapa fursa zaidi ya kujisajili.

Hayo yalisemwa jana Bungeni na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Peter Msollla wakati akiwasilisha hotuba yake ya makadrio ya mapato na matumizi ya fedha ya wizara hiyo.

“Serikali ya Chama Cha Mapinduzi ni sikivu imesikia kilio cha wananchi wengi. Imeongeza muda wa usajili wa simu za viganjani hadi Julai 15, mwaka huu baada ya hapo simu zote ambazo hazijasajiliwa zitafungwa,” alisema Profesa Msolla .

Aidha Waziri Msolla alisema jumla ya kampuni 14 hadi sasa zimepewa leseni ya kutoa huduma za mawasiliano ya simu.
Aliongeza kuwa idadi ya watumiaji wa simu kwa kigezo cha njia za simu (line) zinazotumika imefikia 18,207,390, hivyo idadi hiyo ni ongezeko la asilimia 400 ikilinganishwa na watumiaji 3,542,563 waliokuwepo mwaka 2005.

Alisema idadi ya simu za mezani hadi sasa ni 174,800 ilinganishwa na 154,420 zilizokuwepo mwaka 2005.

“Hii ni sawa na ongezeko la la asilimia 13.2 . ukuaji huu umepanua wigo wa mawasiliano ya simu na kuongeza huduma nyingine zinazoendana na matumizi ya simu hapa nchini

Alizitaja huduma hizo kuwa ni upatikanaji wa taarifa, huduma za mtandao, ulipaji wa Ankara za simu, maji, umeme na huduma za kibenki.

Awali Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilitoa agizo kuwa namba zote za simu za mkononi zisajiliwe kati ya Julai 1, mwaka 2009 hadi Desemba 31, mwaka 2009.

Awali mamlaka hiyo iliongeza muda wa mara ya pili wa miezi sita wa kusajili simu hizo, kuanzia Januari mwaka 2010 hadi Juni mwaka huu baada ule wa kwanza kuonyesha watu wengi walikuwa hajajisajili. SOURCE: BUNGE.

2 comments:

Anonymous said...

Ad spending for specialty lines is heavily skewed towards motorcycles, is growing off a small base, but still only
amounts to about two cents for every dollar spent on conventional Car Insurance
30 Day Policy. Once you're travelling at lower speeds usually at the time of emergency situations. One thing to know is the minimum number of car insurances required?

My homepage: auto insurance []

Anonymous said...

No sweat though Trust me, if you have the right tools to how to get girlfriend.
There could be a sign that she does not, or worse, are downright shabby, you will act like a
jerk around her. Of course they do-they are depending on theory.
But good looks alone will not how to get girlfriend.
Stuff toys: Php 3, 000/yearJewelries ring, necklace, etc. That is why a man wants to be.


Feel free to visit my weblog :: how to get a girlfriend (http://howtogetagirlefriend.com/)