Sunday, October 31, 2010

ELVAS MUSIBA AFARIKI DUNIA!


Hayati Elvis Musiba.

Aliyekuwa Rais wa Chama Cha Wafanyabiashara na Wenye Viwanda nchini Tanzania (TCCIA), Elvis Musiba, amefariki dunia leo jijini Dar es salaam. kwa mujibu wa taarifa fupi iliyotolewa na ITV jioni hii, taarifa kamili na mipango ya mazishi itatolewa baadae na msiba uko nyumbani kwa marehemu, Mikocheni. Kwa wapenzi wa hadithi za vitabu, watamkumbuka marehemu kwa zile novo zake maarufu za Kikosi Cha Kisasi cha Willy Gamba na Njama zilizotamba nchini Tanzania katika miaka ya 80. Mungu alilaze roho ya marehemu peponi - Amin!

Wednesday, October 27, 2010

Madaktari wakiteta uwanja wa ndege Dar


Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal (kulia) akizungumza na Mgombea urais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, walipokutana uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere wa Jijini Dar es Salaam leo mchana wakati Dk. Shein, akiondoka kuelekea Visiwani Zanzibar na Dk. Bilal, akiwasili jijini kutoka Visiwani humo kwa ajili ya kufanya mkutano wa kampeni leo Okt 27.

Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal (kulia) akisalaimiana na Mgombea urais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, walipokutana uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere wa Jijini Dar es Salaam leo mchana wakati Dk. Shein, akiondoka kuelekea Visiwani Zanzibar na Dk. Bilal, akiwasili jijini kutoka Visiwani humo kwa ajili ya kufanya mkutano wa kampeni leo Okt 27. Kuliani ni mke wa Dk. Bilal, Bi Zakia Bilal.


Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal (kulia) akizungumza na Mgombea urais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, walipokutana uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere wa Jijini Dar es Salaam leo mchana wakati Dk. Shein, akiondoka kuelekea Visiwani Zanzibar na Dk. Bilal, akiwasili jijini kutoka Visiwani humo kwa ajili ya kufanya mkutano wa kampeni leo Okt 27. Kushoto ni mke wa Dk. Shein, Tunu Shein, akizungumza na mke wa Dk. Bilal, Zakia Bilal.


Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal (kulia) akisalaimiana na Mgombea urais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, walipokutana uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere wa Jijini Dar es Salaam leo mchana wakati Dk. Shein, akiondoka kuelekea Visiwani Zanzibar na Dk. Bilal, akiwasili jijini kutoka Visiwani humo kwa ajili ya kufanya mkutano wa kampeni leo Okt 27. Picha zote na Muhidin Sufiani.

Tuesday, October 26, 2010

Shinda mkoko Vodacom bado siku 15 tu


Magari aina ya Hyundai I10 yanayotolewa na kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania katika shindano lake la kila siku la Shinda Mkoko yakiwa katika msururu wakati yalipokuwa yakipelekwa katika maegesho yaliyopo kwenye kampuni ya kuuza magari ya FK Motors iliyopo barabara ya Nyerere.

Monday, October 25, 2010

Kampeni mgombea urais wa TLP


Katibu Mkuu wa TLP Rajabu Tao (kulia) akimnadi mgombea Urais wa chama hicho Mutamwega Mgahywa, kwa wananchi waliohudhuria mkutano wa mgombea huyo eneo la Manzese viwanja vya Bakhressa jijini Dar es Salaam juzi, ambapo walitangaza kumalizia kampeni zao Mkoani Mwanza.

Mgombea urais kwa tiketi ya TLP Mutamwega Mgahywa, akiwapungia mkono wananchi waliohudhuria mkutano wa mgombea huyo eneo la Manzese viwanja vya Bakhressa jijini Dar es Salaam juzi, ambapo wanatarajia kufungia kampeni zao Mkoani Mwanza. Picha zote na Said Powa

Ujumbe wa Tanzania waondoka kwenda Miss World


Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania,Ankal Hashim Lundenga akiwa katika mazungumzo na wazazi wa Genevieve Emmanuel mrembo anaeiwakilisha Tanzania katika masindano ya Dunia,katika uwanja wa ndege wa J.K. Nyerere leo.

Ujumbe wa watu 5 ukiongozwa na Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania bw. Hashim Lundenga umeondoka nchini leo kuelekea Sanya China katika kuhudhuria mashindano ya urembo ya dunia yaliyopangwa kufanyika Jumamosi Tarehe 30 Oktoba 2010.

Katika ujumbe huo yupo pia Katibu Mkuu wa Kamati bw. Bosco Majaliwa, Miss Tanzania Mshindi wa 2 Glory Mwanga, na Miss Temeke mshindi wa 2 Anna Daudi ambaye pia alifanikiwa kuingia katika 10 bora ya Fainali za Miss Tanzania 2010.

Mama Mzazi wa Miss Tanzania 2010 Genevieve Emmanuel, Mrs. Mary E. Mpangala pia yumo katika msafara huo ili kushuhudia Fainali hizo za kumtafuta Mrembo wa dunia ambazo zitafanyika Jumamosi hii katika kisiwa cha Hainan huko Sanya China.

Msafara huo unatarajia kurejea nchini Tarehe 3 Novemba 2010.

Z connect promotion


Un identified Motorcyclist showing a different style of driving motorcycles in Arusha during the Z connect promotion offered by mobile phone company, Zantel. Photo/Courtesy.

Jeshi la Kenya wamshukuru Mungu


Kikosi cha Misitu pamoja na familia zao wakiingia katika kanisa la Romani Catholic upande wa the holy family Minor Basilica kwaajili ya kuanza ibada ya shukrani kwa Mungu iliyofanywa jana na askari Polisi na familia zao nchini Kenya.

Rais Mwai kibaki akikata keki baada ya kumalizika kwa ibada ya shukrani kwa Mwenyezi Mungu iliyofanywa jana na askari Polisi wa Kenya pamoja na familia zao katika kanisa la Roman Catholic upande wa the holy family Minor Basilica huku Askofu wa kanisa hilo pamoja na makamanda wa Jeshi hilo wakishuhudia. Picha zote na Anna Nkinda - Nairobi.

DKT. NCHIMBI: SAFARI YA HESHIMA KWA WAZEE WA TAIFA

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemtembelea na kumjulia hali, Rais Mstaafu wa Awamu y...