Sunday, February 26, 2012

TABORA BOYS WAKUTANA MBALAMWEZI BEACH

Mwenyekiti wa Mkutano wa Wana Tabora Boys, Edwin Kidiffu wa kwanza kulia ambaye pia ni mwanasheria wa Ewura akimsikiliza kwa makini Makwinya aliyeinua mikono juu akifafanua jambo katika mkutano huo uliofanyika ufukwe wa Mbalamwezi, wanaomsikiliza ni Bina Katikiro mwenye fulana ya bluu


Mzee wa Mshitu akiwapo kwenye mjadala uliokuwa ukiendelea kwa baadhi ya wana Tabora Boys Secondary School waliopata kusoma katika shule hiyo kongwe na yenye sifa tele nchini walipokutana jioni ya jana katika ufukwe wa Mbalamwezi jijini Dar es Salaam, pamoja na mambo mengine ilikuwa ni kukutana, kutafakari na kujadili way forward ya wana Tabora School hao.

Braza Kamtande Sikalwanda (Mchawi wa hesabu) aliyeipandisha chati mno Sekondari ya Tabora enzi hizo (katikati) akijadili jambo na Braza Kipeya wakati wa mkutano huo wa wana Tabora Boys uliofanyika jana katika Ufukwe wa Mabamwezi. Anayewashuhudia kulia ni Danny Lyimo.

Makwinya naye alikuwapo, huyu jamaa enzi hizo akiwa Tabora Boys alikuwa mkoba wa kutumainiwa wa timu ya shule na hasa pale timu ilipoweza kuitandika timu ngumu ya Uyui Sekondari mabao mawili kwa bila jambo lililizua balaa. Hapa jamaa anapiga maji ya mende.


Dokta Mzee Gombo ambaye ni Specialist wa Meno Muhimbili enzi hizo alikuwa PC wa PCB kwa lugha rahisi alikuwa kiranja wa darasa la wakali wa kombinesheni ya PCB akiwa na akina Charles Sebastian na Rahim Mzee, kwa mbali waweza kumuona Second Chief George, ambaye sasa ni daktari wa magonjwa sugu.

Palipo na picha, mara nyingi pana simulizi isiyoandikwa. Lakini kwa wazoefu wa maisha ya Tabora Boys, kila taswira huibua mlolongo wa kumbukumbu—za jasho, udugu, na nyakati zilizowatengeneza kuwa watu walivyo leo. Katika picha iliyopigwa hivi karibuni, Danny Lyimo anaonekana akishuhudia tukio lisilo la kawaida: Makwinya akisalimiana kwa hisia na Luwaga Kizoka—maarufu kama Nyigu. Nyuma yao, Renasco Mbilinyi anasimama kimya, lakini uso wake unaeleza mengi kuliko maneno.

Ni salamu ya kawaida, lakini pia ni ishara ya muda uliopita—wakati ambao ulikuwa mgumu lakini wenye fadhila za maisha. Salamu hiyo inavunja ukuta wa miaka, inafuta vumbi la kimya, na kuunganisha upya mioyo iliyounganishwa zamani na kiapo kisichoandikwa cha udugu wa Tabora Boys.

Danny Lyimo, kwa macho makini, hachungulii tu watu wawili wakisalimiana. Anaona nyuma ya pazia—miaka ya mafunzo ya kijeshi, zaezi la range, sindicate, sare za khaki, na nderemo za uwanjani. Anaona watoto waliogeuzwa wanaume. Anaona familia iliyozaliwa si kwa damu, bali kwa historia na kushirikiana katika kila hali.

Nyigu, kama alivyofahamika shuleni, hakuwa jina tu—alikuwa nembo ya msimamo. Makwinya, kwa salamu hiyo, hakumkumbatia mtu bali kumbukumbu nzima ya enzi zao. Na Renasco, japo nyuma ya pazia, anashuhudia ushahidi wa udugu unaovuka wakati, umbali na hadhi.

Tukio hili dogo lina ujumbe mkubwa: Urafiki wa kweli hauzeeki. Haubadilishwi na miongo wala majina ya vyeo. Huo ni urafiki uliopikwa kwa jua la Tabora, ukakomazwa na kwata, na kufungwa kwa heshima ya sare na ndoto za baadaye.

Kwa wengi, salamu hii ya kawaida ni picha tu. Lakini kwa familia ya Tabora Boys, ni waraka wa historia unaoandikwa upya—ushahidi wa kuwa nyakati hubadilika, lakini mioyo iliyounganishwa katika ujana huendelea kupigana kwa mdundo mmoja, hata miaka mingi baadaye.

Na timu ya Mzee wa Mshitu, kama kawaida, inaahidi kuwaletea picha na taarifa zaidi—kwa sababu kumbukumbu hizi si mali ya waliokuwepo tu, bali ni urithi wa wote walioguswa na utukufu wa Tabora Boys.

Wednesday, February 15, 2012

JK ashiriki ufyatuaji matofali Msoga





Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika hatua mbalimbali za kusaidia kufyatua matofali ya kisasa kwenye kambi ya mafunzo ya ujasiriamali na ujenzi kwa vijana 380 toka wilaya zote za Mkoa wa Pwani za Kibaha mjini Kibaha vijijini, Mafia, Kisarawe, Mkuranga na Rufiji.

Kambi hiyo ya mwezi mmoja iliyo katika kijiji cha Msoga, wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani, ni moja kati ya kambi kadhaa zinazoandaliwa mkoani humo, ambapo ikimalizika hii ya ujenzi mnamo february 29, itafuatia ya upandaji miti na mazingira itakayokuwa katika Chuo cha Elimu Kibaha. Baada ya Hapo itafuatiwa kambi ya ukulima wa mazao ya mbogamboga wilayani Rufiji.

Rais Kikwete ameusifu mkoa wa Pwani kwa kubuni kambi hizo na kutaka mikoa mingine iige mfano huo ili kuwapa vijana ujuzi wa kuweza kujiajiri wenyewe.

Ameahidi kuendelea kusaidi vikundi vya vijana vya aina hiyo ambavyo amevitaja kama hazina nzuri ya maendeleo na utatuzi wa vitendo wa tatizo la ajira.

Rais Kikwete ametoa mashine za kufyatulia matofali ya kisasa 76 ambapo kila moja kati ya vikundi 38 vilivyopo vitapewa mashine mbili mpya na waliyofanyia kazi wataondoka nayo na kuwa ya tatu. Pia Amewapa vijana hao mifuko 3800 ya saruji (kila kundi mifuko 100), viatu vigumu (gum boots) pamoja na mananasi toka shambani kwake.

PICHA NA HABARI NA IKULU


MAJALIWA: FANYENI TAFITI ZENYE TIJA KWA WANANCHI

Dar es Salaam, 18 Juni 2025 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, ametoa wito kwa watafiti na wapangaji wa s...