Tuesday, November 29, 2016

WAZIRI MKUU MH. KASSIM MAJALIWA AKUTANA NA MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA NYUMBA (NHC)

mchec1
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji  wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu kwenye chumba cha watu mashuhuri cha uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere jijini  Dr es salaam Novemba 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
mchec2
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Mchechu kwenye uwanja wa ndge wa Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Novemba 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI NAPE NNAUYE APOKEA PICHA YA RAIS DK JOHN POMBE MAGUFULI ILIYOCHORWA NA KIKUNDI CHA ANGAVU

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye (kulia) akipokea picha ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kutoka kwa Mwenyekiti wa Angavu Youth Group Athumani Salum (kulia)  jijjini Dar es Salaam. Picha hiyo imechorwa kwa ustadi na kikundi cha Angavu Youth Group.
Muonekano wa picha ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli iliyoichora kwa ustadi na kikundi cha Angavu Youth Group ambapo imekabidhiwa  jijini Dar es Salaam kwa Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye kwa niaba ya Mheshimiwa Rais.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kabla ya makabidhiano ya picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli iliyochorwa na kikundi cha Angavu Youth Group  jijini Dar es Salaam. Picha hiyo imekabidhiwa kwa Waziri huyo kwa niaba ya Mhe. Rais. kushoto ni Mwenyekiti wa Angavu Youth Group Bw. Athumani Salum na kulia ni Katibu wake Bi. Oliver Charles.Picha na Anitha Jonas – MAELEZO
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye (kulia) akisikiliza kwa makini hotuba iliyokuwa ikisomwa na Katibu wa Angavu Youth Group Bi.Oliver Charles (katikati) wakati wa makabidhiano ya picha ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli jijini Dar es Salaam.

WAZIRI LWENGE ATEMBELEA KIWANDA CHA KUTENGENEZA MABOMBA NCHINI

 Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge akiangalia aina ya bomba lililotumika kwenye mradi wa Ruvu Chini na Mkurugenzi wa Kiwanda cha Tanzania Steel Pipes Limited, Nicolas Loh (kulia) pamoja na Meneja Biashara, Ryan Koh.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge akiwa kwenye karakana ya kiwanda hicho.
Mafundi wakiwa kazini katika karakana ya Kiwanda cha Tanzania Steel Pipes Limited.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge akimsikiliza Mkurugenzi wa Kiwanda cha Tanzania Steel Pipes Limited, Nicolas Loh na kujionea moja ya mabomba yanayotengenezwa na kiwanda hicho.


Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Inj. Gerson Lwenge mwishoni mwa wiki alitembelea Kiwanda cha Tanzania Steel Pipes Limited (TSP) kilichopo Shekilango, Dar es Salaam.

Kiwanda hicho kinachotengeneza mabomba ya maji, ambayo pia yanatumika katika utekelezaji wa miradi ya maji nchini, ukiwemo mradi ya maji ya Ruvu Chini, KASHWASA na Ruvuma.

“Nimeridhishwa na uwekezaji wa kiwanda hiki cha mabomba, ambacho kina uwezo wa kuzalisha mabomba yenye ubora wa kutekeleza miradi yetu ya maji nchini”.“Hii ni hatua kubwa kwa nchi yetu ikizingatiwa kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuinua uchumi wa viwanda nchini, hivyo maendeleo ya kiwanda hiki ni hatua nzuri ya kufikia lengo hilo”, alisema Waziri Lwenge.

Inj. Lwenge alisema uwezo ilionao kiwanda hiki ni chachu ya maendeleo kwa Sekta ya Maji na Umwagiliaji kwani kwa muda mrefu Serikali imekuwa ikununua mabomba kutoka nje ya nchi, na hata yanayotengenezwa hapa mengi ni ya plastiki ambayo hayadumu muda mrefu ukilinganisha na ya chuma.Naye Mkurugenzi wa kiwanda cha Kiwanda cha Tanzania Steel Pipes Limited (TSP) alisema nia yao kubwa ni kutengeneza bidhaa nzuri zenye ubora wa kimataifa na kushindana katika soko la kimataifa, na kuiomba Serikali itumie bidhaa za wawekezaji wa ndani zenye ubora wa hali ya juu.

Alisisitiza bidhaa zao zinatengenezwa hapa nchini tangu hatua ya awali na wala si kuagizwa kutoka nje, zina uwezo wa kudumu mpaka miaka 50, zinatumika nje ya nchi ikiwemo Rwanda, ambapo zinatumika kwenye miradi mikubwa ya maji.Dhumuni la ziara hiyo lilikuwa ni kujionea uwezo wa kiwanda hicho kwa upande wa uzalishaji na ubora wa bidhaa zao.

TAZAMA PICHA MBALIMBALI ZA TUKIO LA RAIS DKT.MAGUFULI ALIPOMWANDALIA RAIS EDGAR LUNGU DHIFA YA KITAIFA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM


 Rais Mstaafu wa awamu ya Pili AlhajAli Hassan Mwinyi,Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid Karume wakielekea kwenye dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa heshima ya Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Lungu katika ukumbi wa Ikulu jijini Dar es salaam usiku huu.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakielekea kwenye dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa heshima ya Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Lungu katika ukumbi wa Ikulu jijini Dar es salaam usiku huu.
 Rais Dkt John Pombe Magufuli na  Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Lungu katika ukumbi wa Ikulu kwa dhifa hiyo ya kitaifa aliyomwandalia mgeni wake Ikulu jijini Dar es salaam usiku huu.
 Meza kuu ikiwa imesimama kwa Wimbo wa Taifa
 Rais Dkt Magufuli akimsindikiza mgeni wake Rais Edgar Lungu wa Zambia kusalimiana na viongozi mbalimbali
 Rais Edgar Lungu wa Zambia akisalimiana na Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi. Kulia ni Naibu Spika Dkt Tulia Ackson
 Rais Edgar Lungu wa Zambia akisalimiana na Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
 Rais Edgar Lungu wa Zambia akisalimiana na Naibu Spika Dkt Tulia Ackson
 Rais Edgar Lungu wa Zambia akisalimiana na Spika Mstaafu Mhe. Pius Msekwa
 Rais Edgar Lungu wa Zambia akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman
 Rais Edgar Lungu wa Zambia akisalimiana na Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt Amani Abeid Karume
 Rais Edgar Lungu wa Zambia akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba
 Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Bw. Gerson Msigwa akisherehesha hafla hiyo
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia
 Rais Edgar Lungu wa Zambia akigonganisha glasi na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan
 Wimbo wa Taifa 
 Viongozi wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa wa Zambia ukipigwa
 Viongozi wa vikosi vya ulinzi na usalama pamoja na Mkuu wa Itifaki wa Zambia wakiwa wamesimama kwa wimbo wa Taifa 
 Sehemu ya Mawaziri waliohudhuria wakiwa wamesimama
 Viongozi wakiwa wamesimama
 Makatibu wakuu na sehemu ya ujumbe wa Zambia
 Wageni waalikwa na viongozi wa vyama vya siasa
 Baadhi ya mabalozi mbalimbali waliohudhuria
 Wageni mbalimbali
 Mabalozi mbalimbali
 Mabalozi na maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje 
 Wafanyabiashara na viongozi wa taasisi mbalimbali
  Wafanyabiashara na viongozi wa taasisi mbalimbali na maafisa wa Wizara ya Mambo ya nje
 Viongozi wa taasisi mbalimbali
 Viongozi wa kidini na wageni mbalimbali

 Makatibu wakuu na Balozi wa Tanzania nchini Zambia Mhe. Grace Mujuma
 Rais Dkt Magufuli akigonganisha glasi na mgeni wake Rais Edgar Lungu wa Zambia
 Mrisho Mpoto na Banana Zorro na Mjomba band akitumbuiza

 Mrisho Mpoto akighani wimbo maalumu
 Rais Edgar Lungu akiagana na viongozi 


 Rais Edgar Lungu akiagana na viongozi 
 Rais Edgar Lungu akiagana na Rais wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein
 Rais Edgar Lungu akiagana na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan
 Rais Edgar Lungu akisindikizwa na mweyeji wake Rais Dkt Magufuli
 Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid Karume wakiondoka baada ya dhifa

Rais Dkt. Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Rais Mstaafu Dkt.  Jakaya Mrisho kikwete na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakifurahia jambo mara baada ya dhifa hiyo ya Kitaifa Ikulu jijini Dar es salaam. PICHA NA IKULU