Tuesday, December 08, 2015

TGDC NA MKAKATI WA UZALISHAJI WA UMEME KUPITIA JOTOARDHI

 Meneja Mkuu Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Mhandisi Boniface Njombe (kushoto) pamoja na Mtaalamu Mkuu toka Kampuni ya TOSHIBA Bwana Kentaro Kurahara wakiweka saini Mkataba wa wa Maelewano (MOU) wa kufanya tafiti kwa pamoja zinahusu maeneo yenye viashiria ya upatikanaji wa nishati ya jotoardhi katika Ofisi za TGDC zilizopo Jijini Dar es Salaam.
 Meneja Mkuu Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Mhandisi Boniface Njombe (kushoto) pamoja na Mtaalamu Mkuu toka Kampuni ya TOSHIBA Bwana Kentaro Kurahara wakikabidhiana Mkataba wa Maelewano (MOU) wa kufanya tafiti kwa pamoja zinahusu maeneo yenye viashiria ya upatikanaji wa nishati ya jotoardhi katika Ofisi za TGDC zilizopo Jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja (kulia) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa ICEIDA, Bwana Engilbert Gudmundsson, wakiweka saini Mkataba wa Makubaliano ya Ushirkiano wa kufanya tafiti kwa pamoja zinahusu maeneo yenye viashiria ya upatikanaji wa nishati ya jotoardhi katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini zilizopo Jijini Dar es Salaam.

Na Benedict Liwenga-MAELEZO.
KUTOKANA na ongezeko la mahitaji ya nishati ya umeme nchini, nishati itokanayo na jotoardhi (Geothermal Energy) imetajwa kuwa ni muhimu katika kuepukana na hasara kubwa na isiyo ya lazima inayotokana na matumizi ya mitambo ya mafuta katika kuzalisha umeme na kuifanya Tanzania kuondokana na tatizo la umeme usiokuwa na uhakika pamoja na kuleta maendeleo nchini.

Ili kuleta Maendeleo haya katika sekta ya nishati, Tanzania hainabudi kugeukia katika vyanzo vingine vya uzalishaji umeme ikiwemo nishati hiyo ambayo kwa kutumia mvuke wa maji yaliyochemshwa na joto la asili lililopo chini ya ardhi, nishati ya umeme inaweza kuzalishwa na kukidhi mahitaji ya nishati ambayo yatasaidia kuwa kiunganishi cha ukuaji wa uchumi nchini. 

Tanzania iko katika ukanda wa Bonde la Ufa (Rift Valley), hivyo kuna uwezekano mkubwa wa uwepo wa hifadhi kubwa ya nishati itokanayo na jotoardhi ambayo inaweza kutumika katika uzalishaji wa umeme na kuinua uchumi wan chi yetu.

Nishati hii itakuwa mkombozi kwa taifa letu hususani kwa mwananchi wa kipato cha chini kwani tunaamini kuwa matumizi ya nishati hiyo yatapelekea kupungua kwa gharama za manunuzi ya umeme na kutokana na ukweli kwamba nishati hiyo pindi ipatakinapo haitarajiwi kuisha.

Unafuu wa umeme utakaozalishwa na jotoardhi unatokana na ukweli kwamba mitambo inayotumika kuzalisha umeme huo kuendeshwa kwa mvuke ambao unatokana na majimoto toka ardhini tofauti na uzalishaji wa umeme uliokuwa unatumika kwa kutumia mitambo yenye kutumia mafuta ambayo gharama yake ilikuwa juu kwa Serikali.

Hapa nchini, kuna viashiria vingi vinaonyesha uwepo wa jotoardhi hasa kwa maeneo ya vijijini ambako umeme sehemu nyingi haujafika, kutokana na hilo sasa Serikali yetu hainabudi kutupia macho katika nishati hii kwa kuhakikisha kwamba wananchi ambao wnaaishi maeneo ambayo nishati hiyo inapatikana wananufaika na umeme huo.


Jotoardhi ina matumizi mengi kwa jamii yetu, mfano majimoto yatokayo ardhini yanaweza kutumika katika kukaushia mazao mfano matumizi ya Vitalu shamba(Green Houses) badala ya kutegemea jua. Mwananchi wa kipato wa chini anaweza kutumia majimoto kukausha mazao yake kwa mfano mpunga, maharage, mahindi, karanga katika ubora ule ule kama wa jua. 

Matumizi mengine ya majimoto ni katika kupasha nyumba joto hasa katika wananchi wale waishio mikoa yenye baridi kali kwa kujenga mabomba ya kupitisha maji ya moto ndani ya nyumba zao.

No comments: