Monday, December 07, 2015

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI AZUNGUMZA NA WAFANYAKAZI WA KIWANDA CHA URAFIKI


 Askari wakipita karibu na kiwanda cha urafiki jijini Dar es Salaam huku wakiwaangalia kwa makini wafanyakazi wa kiwanda hicho waliomo katika mgomo wakidai manejimenti yakiwanda hicho kiasi cha shilingi Bilioni 9.

Bidhaa zinazouzwa katika moja ya eneo la kiwanda cha urafiki yaliyokodishwa na uongozi wa menejimenti ya kiwanda hicho unaolalamikiwa na wafanyakazi kwamba wanajipatia mapato kwenye maeneo ya kiwanda hicho huku wao wakiwalipa kiduchu.
 Baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda cha urafiki wakiwa kwenye geti la kuingilia kiwandani hapo wakimngoja Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda ili kuzungumza nao.

Mkuu wa Wilaya ya kinondoni Paul Makonda, akiwasili na msafara wake kiwandani hapo kwa ajili ya kuzungumza na wafanyakazi walio katika mgomo. 
Mkuu wa Wilaya ya kinondoni Paul Makonda akizungumza na wafanyakazi wa Kiwanda cha Urafiki leo jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa kiwanda cha Urafiki wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda

No comments: