Monday, December 07, 2015

AIRTEL FURSA YATUA BUKOBA, YAONGEA NA VIJANA KUTOOGOPA VIKWAZO KATIKA UJASILIAMALI

 Mjasiliamali wa mjini Bukoba Adamu Hemed akipokea cheti kutoka kwa meneja biashara wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Mohamedi kabeke baada ya kuhudhuria mafunzo ya ujasiliamali yaliyoendeshwa na mradi wa Airtel FURSA kwa Zaidi ya vijana 200. kati ni Afisa ujasilimali wa VETA mjini bukoba Bw, Frabius Ngemela na Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando mwishoni mwa wiki hii mkoani Kagera.
 .Mkulima wa mboga mboga kutoka Bukoba mjini Agnetha Frenk akipokea cheti toka kwa meneja wa biashara Airtel BUkoba Mohamed kabeke baada ya kuhudhuria mafunzo ya ujasiliamali yaliyoendeshwa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel mjini Bukoba kati ni Afisa ujasilimali wa VETA mjini bukoba Bw, Frabius Ngemela na anaefuata ni Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando. Semina hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki kwa siku mmoja na kuhudhuriwa na vijana zaidi ya 200 mkoani Kagera.
Mkazi wa mtaa wa Nshambya mjini Bukoba Janath Shafi anayejishughulisha na biashara ya ufugaji wa mbuzi akipokea cheti toka kwa meneja wa biashara Airtel BUkoba Mohamed kabeke baada ya kuhudhuria mafunzo ya ujasiliamali kwa vijana yaliyandaliwa na kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Airtel mkoani Kagera. Cheti baada ya kuhudhuria mafunzo ya ujasiliamali yaliyoendeshwa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel, Katikati ni mwalimu wa mambo ya ujasiliamali ambae pia ni Afisa ujasilimali wa VETA mjini bukoba Bw, Frabius Ngemela na anaefuata ni Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando. Semina hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki kwa siku mmoja na kuhudhuriwa na vijana zaidi ya 200 mkoani Kagera.
 Kijana anayejishughulisha na ufugaji wa kuku kutoka Kijiji cha Katoka Wilaya ya Bukoba Vijijini Lucas Joseph akipokea cheti toka kwa meneja wa biashara Airtel BUkoba Mohamed kabeke baada ya kuhudhuria mafunzo ya ujasiliamali kwa vijana yaliyandaliwa na kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Airtel mkoani Kagera. Katikati ni mwalimu wa mambo ya ujasiliamali ambae pia ni Afisa ujasilimali wa VETA mjini bukoba Bw, Frabius Ngemela na anaefuata ni meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando. Semina hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki kwa siku mmoja na kuhudhuriwa na vijana zaidi ya 200 mkoani kagera.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya ujasiliamali yaliyofanyika mjini Bukoba yaliondaliwa na kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Airtel kupitia mpango wake wa fursa tunakuwezesha. Semina hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki kwa siku mmoja na kuhudhuriwa na vijana zaidi ya 200 mkoani kagera

· Bukoba zaidi ya wajasiliamali vijana 200 wanolewa na Airtel Fursa
KAMPUNI ya mawasiliano ya simu za mkononi airtel imewataka watanzania kuchangamkia fursa zilizopo kwa kufanya ujasiriamali kwa mtazamo mpana kwa lengo la kuondokana na umasikini au maisha duni yasiyo na kipato maalum.

Hayo yamesemwa na mwalimu wa mambo ya ujasiliamali ambae pia ni Afisa ujasilimali wa VETA mjini Bukoba Bw, Frabius Ngemela kwa zaidi ya wajasiliamali 200 waliohuduria semina ya ujasiliamali ya Airtel Fursa BUKOBA akiwataka vijana wajasiliamali kutumia ujuzi na maarifa katika kuboresha miradi yao kama njia mojawapo ya kukabiliana na suala la umasikini na kuwataka wajasiliamali hao kutokata tamaa ya maisha badala yake waongeze juhudi katika uzalishaji mali bila kuogopa vikwazo ili kujikomboa.

Airtel Fursa imekuja Bukoba leo kuwaambia msikate tamaa, nawafundisha leo kuvitambua vikwazo na msiviogope katika shughuli zenu, mkashirikiane na mradi wa Airtel Fursa ili kujikwamua.

Kwa upande wake Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando alieleza “Airtel Fursa sio tu tunawasaidia vijana kuzitambua fursa pia tunawapatia mitaji na vitendea kazi muhimu ambavyo vimekua ni vikwazo vya kutimiza malengo yako ili uweze kuzalisha zaidi na kusaidia jamii zao.

“Hadi sasa tumeshazunguka mikoa zaidi ya 12 ndani ya miezi hii minne tukiwaeleza vijana jinsi wanavyoweza kukamata FURSA na kuwasaidia kupitia warsha kama hizi pia kuwapatia vitendeakuzalis kazi na vifaa mbalimbali waweze kuzalisha zaidi” alisema Mmbando.

wakiongea mara baada ya kupatiwa elimu ya ujasilimali baadhi ya wajasiliamali wadogo Peace Ruben MJASIRIAMALI, alisema licha ya kupatiwa elimu hiyo bado wanakabilina na changamoto mbalimbali ikiwemo mitaji ya kuendeshea biashara zao ambapo pia wametumia nafasi hiyo kuiomba kampuni ya airtel kwa kutumia mradio wao wa Airtel fursa kuwapatia mitaji itakayo wasaidia kuendesha biashara zao.

“Mi kazi yangu ni kufuma vitambaa na nguo za kuzuia baridi kwa watoto , wateja wangu wanapatikana kwa urahisi hapa bukoba na nje ya bukoba yaani hapo mpakani mwa Tanzania na Uganda lakini tatizo ni vitendea kazi vya kutosha ili kuongeza uzalishaji, ikiwa Airtel Fursa itanitoa nitafurahi sana” alieza Peace Ruben

No comments: