Sunday, February 28, 2010

Nassib arudi tena TFF


Nchimbi (Kushoto) na Nassib (kulia) wakisubiri matokeo.
NI kawaida kuwa baada ya ushindi kuna mashamsham, lakini tofauti na jana, uchaguzi wa Makamu wa pili wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, ulikuwa na utulivu wa aina yake hata baada ya matokeo kutangazwa.

Mbali na wajumbe zaidi ya 100 kuchagua mgombea wa nafasi hiyo, pia walimchagua mwakilishi wa Kanda Nyanda za Juu Kusini ambaye ndiye mwakilishi katika mkutano wa TFF.

Katika nafasi ya Makamu wa Pili wa Rais, John Nchimbi alikuwa akichuana na Nassib Ramadhani aliyekuwa anatetea nafasi yake.

Nassib aliyekuwa akidhaminiwa na Mtibwa Sugar huku Nchimbi akisimamiwa na Majimaji, alitetea kiti chake baada ya kupata upinzani mkali wa kura 54 wakati Nchimbi alipata 47.

Katika uchaguzi huo uliokuwa na upinzani mkali huku wagombea wakiwa wamesindikizwa na wapambe wao jumla ya wajumbe 101 walipiga kura na hakuna kura hata moja iliyoaharibika.

Hata hivyo, kulikuwa na hisia za rushwa kitendo kilichowafanya baadhi ya wapambe wa wagombea kuimarisha ulinzi eneo la chooni huku wengine wakionekana kukaa vikundi vikundi. SOURCE: MWANANCHI BY VICKY KIMARO.

Wanafunzi nao wamo ktk burudani!!!





Wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Neema Trust iliyopo Mbezi jijini Dar es Salaam,wakitumbuiza wageni waalikwa waliohudhuria mahafari ya pili ya kidato cha sita shuleni hapo jijini Dar es Salaam juzi.Picha na Venance Nestory

Mashujaa Bendi yatikisa Vingunguti





-Neema Mkama Gumzo
-Mashabiki wajimwaga kuselebuka
Bendi mpya ya muziki wa dansi nchini MASHUJAA BAND, juzi iliweza kushambulia jukwaa la ukumbi wa Mashujaa Pub uliopo Vingunguti Dar es Salaam ambapo Wimbo Mpya wa Moshi wa Sigara ulionekana kuwavutia mashabiki walioweza kujitokeza kutokana na kuwagusa wengi hasa mwanamuziki kijana mdogo mwenye kipaji cha hali ya juu PATIENCE NSIMBI (pasia budance) unaongelea mapenzi namna ambavyo yanaweza kutoweka kama moshi wa sigara.
Bendi hiyo ambayo ilikaa kambini kwa zaidi ya siku 40 maeneo ya kigamboni ambako walikamilisha nyimbo mpya 6 ambazo zimeanza kuwa na mguso kwa jamii kutokana jinsi zilivyoimbwa, na hivyo kudhihirisha kwamba kimya walichokuwa wamekiweka kilikuwa na mafanikio.
mkuu wa bendi hiyo ELYSTONE ANGAI ambaye ni mzoefu katika fani ya muziki alizikoga nyoyo za mashabiki mara kwa mara kutokana na uhodari wake wa kulicharaza gitaa la solo huku akisaidiwa na mwanamuziki mkongwe EDWARD ANTONY MALIKIDOGO (jadol feed force), katika kukoleza kutokana na Sauti yake kuwaingia wote walioweza kushuhudia burudani hiyo.
Aidha katika Wimbo wa pili, MWANIKE ulioimbwa kwa mchanganyiko wa lugha 3 yaani Kiswahili,Kisukuma na Kihaya pia ulionyesha kuwavutia wengi walioweza kufika katika ukumbi wa makumbusho ikiwa ni katika onyesho maalum.
“kanda ya ziwa kaeni mkao wa kula” alisema Shaaban Mpalule ambaye ndiye msemaji wa Bendi hiyo, wimbo huo umetungwa na Mwanamuziki na rapper wa bendi SIMON NGOSHA(ngosha masanja)
bendi hiyo inaundwa na Wanamuziki wengi wazoefu na chipukizi jumla wakiwa 25 wakiwemo 7 wenye uraia wa jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo na wengine watanzania ,wamo pia kina dada wanaopamba jukwaa la bendi hiyo,yaani wacheza shoo,idadi yao ni 8 amabao pia ni wazoefu.
“Kazi ndiyo imeanza, ila inaonyesha matumaini makubwa kutokana na kile ilichowapa leo mashabiki waliofika hapa Mashujaa Pub, si tu kwamba nyimbo zimewakoga mashabiki wa Dansi bali pia wacheza shoo wanao mvuto kitu kilichopelekea mashabiki kuwa na hamu ya kutaka kuwaona wakiselebuka, kama ulivyowasikia mashabiki wakimwagia sifa kemukemu mcheza shoo wa kike Neema kutokana na Uhodari wake wa kuzungusha nyonga, ni chipukizi ambaye bila shaka anaweza kuwa tishio katika medani ya muziki wa Dansi ususani katika eneo lake la kujidai(Unenguaji) huyu anafananishwa na nyota wa miondoko hiyo hapa nchini Aisha Madinda”alisema Mpalule.
Na kuwataka mashabiki kujitokeza katika maonyesho yake ili waweze kushuhudia ikiwa ni pamoja na kupata baadhi ya nyimbo zilizokwisharekodiwa, ambazo tayari ziko sokoni.

Hitma ya mzee Kawawa



Rais Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiwa kwenye hitma ya Marehemu Mzee Rashid Mfaume Kawawa leo jijini Dar es salaam , wengine ni Mtoto wa Marehemu Vita Kawawa(kulia) na kushoto ni Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam Mussa Salum.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisamiliana jana jijini Dar es salaam na Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi Captain John Chiligati na Kingunge Ngombale Mwiru. Rais Kikwete alikutana na viongozi hao katika hitma ya Mzee Rashid Kawawa nyumbani kwake Madale jijini Dar es salaam leo.

Maziko ya Balozi Mwakawago


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF Seif Shariff Hamad wakati wa mazishi ya mwanasiasa mkongwe na mwanadiplomasia Marehemu Balozi Daudi Mwakawago yaliyofanyika katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo jioni.Katikati ni Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin Wiliam Mkapa.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka udongo katika kaburi la Marehemu Balozi Daudi Mwakawago wakati wa mazishi ya Mwanasiasa huyo mkongwe yaliyofanyika katika makaburi ya kisutu jijini Dar es Salaam leo jioni(picha kwa hisani ya Freddy Maro)

Friday, February 26, 2010

Rais Kikwete aifariji familia ya Mwakawago


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Daisy Mwakawago mjane wa Marehemu Balozi Daudi Mwakawago aliyefariki dunia juzi jijini Dar es Salaam.Marehemu anatarajiwa kuzikwa kesho jijini Dar es Salaam.Rais alikwenda nyumbani kwa marehemu kuifariji familia yake.Marehemu ameacha mjane na watoto watatu Lulu Mwakawago, Kie Mwakawago na Mtage Mwakawago (picha na Freddy Maro)

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa mwanasiasa mkongwe na mwanadiplomasia marehemu Balozi Daudi Mwakawago nyumbani kwake Msasani jijini Dar es salaam wakati alipokwenda kuifariji familia ya Marehemu.

Serena kujenga shule nyingi Afrika








NAIROBI, Kenya

MCHEZA tenisi namba moja katika ubora wa wachezaji tenisi wanawake duniani anayetokea Marekani Serena Williams amesema ana mpango wa kusaidia kujenga shule moja mpya katika sehemu mbalimbali za Afrika kila mwaka ili kuweza kuwasaidia watoto wa Afrika.

Serena ambaye hivi sasa yupo Barani Afrika kwa ajili ya miradi mbalimbali ya kijamii akiwa balozi wa kampuni ya HP ambayo inatengeneza kompyuta na vifaa vingine vya kiteknolojia, amesaidia ujenzi wa shule nchini Kenya, Senegal na Afrika Kusini, pia amesaidia kulipa ada za wanafunzi na amejiunga katika mpango wa kutokomeza malaria nchini Ghana.

"Ni dhamira yangu kufungua shule nyingi kwa ajili ya maelfu ya wanafunzi barani Afrika ambao hawajapata nafasi ya kwenda shule kupata elimu. Nimepanga kujenga shule moja kila mwaka,"alisema Serena mwishoni mwa wiki iliyopita wakati wa ziara yake ya siku tatu nchini Kenya, ambapo alifungua shule ya sekondari huko Makueni kilomita 150 kusini mashariki ya Nairobi.

Kabla ya ziara hii barani Afrika, Serena alishawahi kwenda Kenya mwaka 2008 na kufungua shule katika eneo hilo hilo la Kusini mashariki ya Kenya, eneo ambalo kwa muda mrefu limekuwa likitegemea chakula cha msaada kwa sababu ya ukame.

"Bila elimu, maisha yanakuwa magumu. Wazazi wangu kila siku walikuwa wakisisitiza umuhimu wa kupata elimu, natumai nimeleta matunda ya maneno yao kwa mimi kupata elimu na kuja hapa Kenya kufungua shule hii ya Wee,"alisema Serena Williams wakati akifungua shule ya sekondari inayoitwa 'Serena Williams Wee Secondary School.'

Thursday, February 25, 2010

Rais arejea home



Rais Kikwete akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam jana katika Uwanja wa Ndege wa Kimatifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mara baada ya kuwasili kutoka nje ya nchi ambapo alikuwa katika ziara ya kikazi. Mwingine katika Picha ni Kingunge Ngombale Mwiru.
Picha na Tiganya Vincent-MAELEZO.

Ngoma ya mganda


Mwalimu wa Sanaa katika shule ya Sekondari Makongo, Simon Mwaikono akiwaongoza wanafunzi wa shule hiyo kucheza ngoma ya mganda yenye asili ya Manda mkani Ruvuma wakati wa mahafali ya 11 ya kidato cha sita shuleni hapo. Picha na Michael Matemanga

BREAKING NEWS NYUUUUZ! BALOZI DAUDI MWAKAWAGO HATUNAYE TENA


MAREHEMU BALOZI DAUDI MWAKAWAGO.

MWANASIASA mkongwe, mwanadiplomasia na mmoja wa watu waliokuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru wa Tanzania, Balozi Daudi Mwakawago amefariki dunia.

Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa Mwakawago alifariki dunia baada ya kuugua malaria kwa siku tisa.

Kwa mujibu wa habari hizo, zilizothibitishwa na viongozi wa CCM, Mwakawago alifikwa na mauti hayo katika hospitali ya Aga Khan iliyoko jijini Dar es Salaam.

Makamu Mwenyekiti wa CCM bara Pius Msekwa, alilieleza gazeti hili jana kuwa alipata taarifa za kifo hicho jana asubuhi.

"Ni kweli Balozi Mwakawago amefariki alfajiri ya leo (jana) katika Hospitali ya Aga Khan alikokuwa amelazwa kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa," alisema Msekwa.

Alisema walipata taarifa hizo kutoka kwa mtoto wa marehemu, Yassin Mwakawago baada ya kufika katika ofisi za makao makuu ya CCM jijini Dar es Salaam na kutoa taarifa hizo.

"Taarifa za kifo cha Balozi Mwakawago tulizipata leo (jana) asubuhi baada ya mtoto wa marehemu, Yassin Mwakawago kufika ofisini na kutueleza msiba huo," alisema Msekwa.

Balozi Mwakawago atakumbukwa kama mwanasiasa na mwanadiplomasia mwandamizi aliyeshika nyadhifa mbalimbali ndani na nje ya nchi. SOURCE: Mwananchi

Wednesday, February 24, 2010

Maonyesho ya vita vya majimaji



Makamu wa Rais Dk Ali Mohamed Shein kushoto na ujumbe wake, wakiangalia sehemu iliyotumika kunyongewa Machifu wa mji wa Songea katika karne ya 19, wakati walipotembelea kwenye maonesho ya kumbukumbu ya Vita vya Majimaji yanayofanyika kila Mwaka Mkoani Ruvuma juzi.

Tuesday, February 23, 2010

Manowari ya Kivita ya Marekani yazuia shambulizi la kiharamia dhidi ya Meli ya Tanzania




Manowari ya Kivita ya Marekani iitwayo USS Farragut ambayo ilizuia shambulizi la kiharamia lililofanywa dhidi ya Meli ya Kitanzania MV Barakaale 1 hapo Februari 21, na kuwakamata maharamia waliohusika katika tukio hilo. Baada ya kupokea taarifa ya kuomba msaada kutoka kwa Nahodha wa MV Barakaale, Helikopta aina ya SH-60B Seahawk kutoka katika Manowari ya Jeshi la Marekani iitwayo USS Farragut iliwasili na kuzuia mashambulizi mawili dhidi ya meli hiyo ya Tanzania.

*************************************************************************************
Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania
Taarifa kwa Vyombo vya Habari


Februari, 23, 2010

Manowari ya Kivita ya Marekani yazuia shambulizi la kiharamia dhidi ya Meli ya Tanzania
Maharamia nane wakamatwa

Hapo tarehe 21 Februari, manowari ya Kivita za Marekani ilizuia shambulizi la kiharamia lililofanywa dhidi ya Meli inayopeperusha bendera ya Tanzania ya MV Barakaale 1, na kuwakamata maharamia waliohusika katika tukio hilo. Baada ya kupokea taarifa ya kuomba msaada kutoka kwa Nahodha wa MV Barakaale, Helikopta aina ya SH-60B Seahawk kutoka katika Manowari ya Jeshi la Marekani iitwayo USS Farragut iliwasili na kuzuia mashambulizi mawili dhidi ya meli hiyo ya Tanzania.

Helikopta hiyo iliweza pia kuwazuia maharamia hao kutoroka kwa kuurushia risasi za onyo mtumbwi wao pale ulipojaribu kuondoka eneo hilo kwa kasi. Hatimaye askari waliokuwa katika USS Farragut waliweza kuingia katika chombo hicho na kuwatia nguvuni washukiwa nane wa uharamia huo. Kwa sasa washukiwa hao wanashikiliwa ndani ya manowari hiyo ya Marekani.

Manowari Farragut ni sehemu ya kikosi maalumu cha kimataifa kijulikanacho kama Combined Task Force 151, kilichoundwa Januari 2009 kwa lengo la kukabiliana na uharamia katika eneo la Ghuba ya Aden na Pwani ya mashariki mwa Somalia, kikiwa na lengo mahsusi la kuzuia, na kupambana na uharamia ili kulinda usalama wa vyombo vya usafirishaji majini na kuhakikisha kuwa vyombo hivyo vinakuwa na uhuru wa kupita katika eneo hilo kwa faida ya nchi zote.

Kikosi hiki maalumu ni sehemu Jeshi la Wanamaji la Kimataifa (The Combined Maritime Forces) linalolinda doria katika eneo la kilomita za mraba milioni 8.6 za bahari ya kimataifa ili kuwa na jitihada na uratibu wa pamoja na hatimaye kufikia lengo la pamoja: kuimarisha usalama na ustawi wa eneo hili.

Jeshi la Wanamaji la Kimataifa linalenga katika kupambana na ugaidi, kuzuia uharamia, kuzuia usafirishaji haramu wa watu na madawa ya kulevya na kuhakikisha mazingira ya bahari yanakuwa salama kwa wasafirishaji wenye biashara halali. Jeshi la Kimataifa la Wanamaji linajumuisha takribani dazani tatu za manowari kutoka nchi za Australia, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Pakistan, Kanada, Denmark, Uturuki, Marekani na Uingereza pamoja na majeshi ya wanamaji kutoka nchi nyingine kadhaa.

Jeshi la Wanamaji la Kimataifa na Kikosi Maalum cha Combined Task Force 151 wamekuwa na mafanikio makubwa katika kuzuia vitendo vya uharamia katika Ghuba ya Aden na Pwani ya Somalia. Japokuwa majaribio ya uharamia yameongezeka katika miaka michache iliyopita, katika kipindi hicho, idadi ya matukio ya uharamia yaliyofanikiwa imepungua kwa asilimia 40.


AMERICAN EMBASSY
686 OLD BAGAMOYO ROAD, MSASANI, P.O. BOX 9123, DAR ES SALAAM, TEL. (255-22) 2668001, FAX 266-8251
HYPERLINK "http://tanzania.usembassy.gov"http://tanzania.usembassy.gov

Monday, February 22, 2010

TCU yatambua rasmi digrii za Dk Mathayo





KAMISHENI ya vyuo vikuu nchini (TCU) imesema imevitambua na kuvithibitisha vyeti vya Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Dk David Mathayo.

Katika barua iliyoandikwa kwenda kwa Dk Mathayo kutoka kwa Katibu mkuu wa TCU, Profesa Mayunga Nkunya, TCU imeeleza kuridhishwa kwake na uhalali wa vyeti vya shahada ya kwanza, shahada ya pili na cheti cha shahada ya falasafa (Ph.D) vilivyowasilishwa kwenye kamisheni hiyo.

“Kwa mujibu wa mamlaka iliyopewa TCU chini ya kifungu 5-(1)(n) cha sheria ya vyuo vikuu namba 7 ya mwaka 2005, tunapenda kutambua uhalali wa vyeti vyako ambavyo vinakubalika kwa misingi ya vyuo vikuu,” ilieleza barua hiyo ya TCU.

Barua hiyo iliyoandikwa Februari 13, 2010 ilieleza kuwa vyeti hivyo vya taaluma ni vile vinavyoonyesha kuwa Dk David Mathayo alipata shahada yake ya kwanza ya udaktari wa mifugo katika chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine (1997).

Baada ya hapo, aliweza kupata shahada ya pili ya Sayansi ya Kilimo katika Chuo Kikuu cha Pretoria nchini Afrika Kusini mwaka 2001 na kupata shahada ya juu ya udaktari wa Falsafa (Ph.D) katika Sayansi ya wanyama kwenye chuo kikuu cha Free State nchini Afrika Kusini mwaka 2003.

Profesa Nkunya pia ameelekeza nakala za batrua hiyo kwa Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ofisi ya Waziri Mkuu, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Katibu mkuu kiongozi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Imeandikwa na Andrew Msechu; SOURCE: MWANANCHI.

Sunday, February 21, 2010

Fare thee well, Reginald ‘Reggie’ Mhango



Former President, Benjamini Mkapa during the burial of veteran journalist Renald Mhango at Kinondoni cemetery in Dar es Salaam yesterday. Mhango died at Hindu Mandal Hospital on Thursday.PHOTO/ZACHARIA OSANGA.

************************************************************

By Abdi M Sultani

A few years ago, a close friend who had lost his favourite child – the apple of his eye, as they say – said to me in a ‘side show’ during the burial arrangements gathering: “It is like I understand why this son of mine had to die so young.”

I couldn’t fathom his “understanding”, so I asked for an elaboration.

“Nice people don’t live long… if, you’re given a sampling of people and you want to make a good bet on who will return to God, pick the nicest among them... good people usually die and leave us, the crooked ones, behind,” he had said, as he wiped away tears.

These weren’t words from the mouth of an acknowledged sage, but then, I mused, don’t we have a Kiswahili saying: “Wema hawana maisha” (Nice people don’t live long)? Afro 70 Band’s Patrick Balisydia used the saying in a tribute song to Samora Machel.

These were the thoughts going through mind upon receiving, on Friday morning, a call from a media colleague, satirist Adam Lusekelo (he of Sunday News ‘Light Touch’ fame), who broke to me news of Reggie’s death.

“Yes, our friend Reggie is dead… I’ve been told he suffered a stroke yesterday (Thursday), and that did it!” said Adam, in a solemn voice.

My instant remark was: Haiwezekani – it’s not possible!

“It’s true, Abdi, Reggie is gone; we’ve lost a really nice guy,” said Adam.

He didn’t have to give the second name – ‘Mhango’, for, in the Tanzania media fraternity, whenever the name Reggie was uttered, much as there are quite a few other scribbling Reginalds, it was like it suited Mr Reginald Mhango the most.

Wearing his trademark perpetual smile that amplified his ebony black complexion, he would always introduce himself as ‘Reggie’ and we in the media, from cub reporters to senior editors, simply called him Reggie.

The name Reginald Mhango was not new to me, for in the 1970s, I would come across the ‘byline’ in the pages the Daily News/Sunday News, the only local English language newspapers then.

So, upon meeting him ‘live’ for the first time in 1999, when he arrived from Malawi to join the Guardian Ltd as the head of the new baby in IPP Media family of newspapers – Daily Mail, it was like I was meeting a person you’ve always known.

“I am Reggie,” he had introduced himself to me when we met in the newsroom.

“Reggie who?” I asked.

“Mhango,” he had said.

“Oh, you mean you’re Reginald Mhango of Daily News?” I had remarked.

As our managing editor (ME), we all appreciated the way he linked up the efforts of the wide array of reporters and sub-editors. The Daily Mail subbing team included veteran Richard Mngazija and up-and-coming ones like David Mbulumi (he had just finished university). Writers ranged from giants like Kajubi Mukajanga to novices like Emmanuel Kihaule (had just finished his A-Level at Makongo High School).

A former group managing editor with New Habari Corporation, Atillio Tagalile, says few editors can equal Reggie in mentoring young scribes. He says Reggie had the rare quality of tolerance when it came to handling trainee journalists, who he would push and encourage to do and re-do their stories until they got it right.

“Many of today’s big names in the media owe what they are to Reggie, for I know quite a few who, in the hands of some no-nonsense news editors I know, would’ve run away from the newsroom in despair,” says Tagalile, who, as a Senior Reporter at the Daily News in 1986, had Reggie, then the News Editor, as his immediate boss.

In The Guardian Ltd newsroom, everybody felt free to have a chat with Reggie, and it didn’t matter whether you were writing for English or Kiswahili titles. So approachable, he was always ready share his long experience gained over (then) close to 30 years in the media.

Besides his amiability and helpfulness in the newsroom, he made good company even in informal settings, mixing with fellow old-timers like Mangengesa Mdimi, Paschal Shija and virtual newcomers like Bernard Mapalala and this writer.

The teetotaller that he was, the man had no problem ‘hanging out’ with those of us who would take one or two to wash down a hearty meal of ugali with fish (Reggie’s favourite kitoweo, the ‘true Mnyasa’ that he was) at Dar es Salaam’s Igongwe Inn at Mwenge.

I believe I am speaking for many by saying that, to those of us who have known Reggie over the years, working with him at Daily News, Daily Mail, PST or The Guardian newspapers, we sincerely feel that at 64, Reggie was too young to die. The media, friends and, of course, his family, wanted him still.

But maybe, to use the words of the friend I mention at the opening of this tribute, “the nice ones tend to die earlier”.

Reginald Mavunika Mhango ‘Reggie’, who was laid to rest at the Kinondoni cemetery in Dar yesterday, was a very nice guy. We loved him, yes, but, as the scriptures teach us to acknowledge, God loved him more.

May He, the Almighty Lord, rest our friend Reggie’s soul in everlasting peace.

Friday, February 19, 2010

Maandalizi ya Tanzania Kili Music Award 2010


Katibu Mtendaji wa baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Gonche Materego(kulia) na meneja wa bia ya Kilimajaro George Kavishe wakiwa na baadhi ya wanamuziki mashuhuri wakati wa uzinduzi wa Tuzo ya mwanamuziki bora Tanzania (Tanzania Kili Music Award 2010) wa pili kushoto ni kushoto Ambwene Esaya ‘AY’, Nyoshi EL Sadaat, wa FM Internationale na Mzee Yusufu wa Jahazi, mara baada ya Katibu Mkuu huyo kuzindua tuzo hiyo Dar es Salaam jana. Picha na Emmanuel Herman

Katibu Mtendaji wa baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Gonche Materego(kulia) na meneja wa bia ya Kilimajaro George Kavishe, wakizidua rasmi tuzo ya mwanamuziki bora Tanzania (Tanzania Kili Music Award 2010) Dar es Salaam jana. Picha na Emmanuel Herman.


Kiongozi wa bendi ya FM Internationale Nyoshi EL Sadaat, akitoa mawazo yake wakati wa utafutaji mawazo ya uboresha wa tuzo ya mwanamuziki bora Tanzania (Tanzania Kili Music Award 2010), iliyozinduliwa rasmi Dar es Salaam, jana. Picha na Emmanuel Herman

Bomani aishangaa serikali kuogopa mgombea binafsi

Asema baba wa taifa Mwalimu Nyerere alibariki hilo mwaka 1995


MWANASHERIA Mkuu wa Kwanza mzalendo nchini, Jaji Mark Bomani amesema serikali inakwamisha bila sababu suala la mgombea binafsi katika uchaguzi, ambalo licha ya kupata baraka za mahakama lilishapata baraka zote za baba wa taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Mbali na kuitaka serikali kuacha kigugumizi katika kuruhusu utekelezaji wa suala hilo; alikosoa mfumo wa sasa wa uchaguzi na uteuzi wa mawaziri na kupendekeza kwamba, siyo lazima waziri awe mbunge.

Suala hili lilifunguliwa kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania na Mwenyekiti wa DP, Christopher Mtikila ambayo ilitoa hukumu mwaka 2006 iliyoruhusu kuwepo mgombea binafsi, lakini serikali imeendelea kuweka ngumu kwa kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa kuomba hukumu hiyo ipitiwe upya.
Februari 8, mwaka huu Jaji Mkuu, Augustine Ramadhan aliahirisha kusikiliza rufaa hiyo baada ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu kutojiandaa vizuri hivyo kuomba isogezwe mbele. Akiahirisha rufaa hiyo, Jaji Ramadhan alisema hukumu ya Mahakamu Kuu itaendelea kama ilivyo hadi hapo rufaa itakapopitiwa na jopo la majaji wa Mahakama ya Rufaa na kumlaumu Naibu Mwanasheria Mkuu kwa kutojiandaa kikamilifu wakati wao ndiyo walioomba ipitiwe upya.

Katika taarifa yake maalumu aliyoitoa kwa gazeti hili jana, Jaji Bomani alisema mfumo wa mgombea binafsi katika chaguzi sio haramu kwa kuwa umeshakubaliwa na wataalamu mbalimbali.

Kauli hiyo ya Jaji Bomani imekuja karibu majuma mawili tangu jopo la majaji saba wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuitaka serikali kuwa makini katika rufaa waliyoikata dhidi ya hukumu ya mahakama kuu kuwepo kwa mgombea binafsi.

Walisema endapo serikali italegalega katika rufaa yake dhidi ya hukumu hiyo iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, suala la kuruhusiwa mgombea binafsi katika uchaguzi mkuu ujao, liko palepale.

Jaji Bomani ambaye alishawahi kushiriki katika kamati mbalimbali za kutafiti mfumo sahihi wa uchaguzi unaofaa Tanzania, alitoa changamoto kwa Rais Jakaya Kikwete kuwa ndiye anayepaswa kusimamia suala hilo.

Alisema Rais Kikwete ana nguvu na nafasi ya kihistoria kutekeleza uamuzi huo wa mahakama kwa kuruhusu mgombea binafsi katika uchaguzi mkuu ujao.

Jaji Bomani alisema hatua nzuri na muhimu ya kuanzia katika utekelezaji wa suala la mgombea binafsi na kuboresha mfumo wa uchaguzi Tanzania, ni kupitia upya ripoti ya Jaji Kisanga, jambo alilosema kuwa serikali haijachelewa.
Imeandikwa na Salim Said na Nora Damian: SOURCE:MWANANCHI

Kada CCM akabiliwa na mashtaka sita ya utapeli


ALIYEKUWA Katibu Mwenezi wa CCM, mkoani Dar es Salaam, Haji Manara (35), jana alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni kujibu mashtaka sita ya kujipatia mali na fedha kwa njia ya udanganyifu.

Alipandishwa kizimbani saa 7:45 mchana na kusomewa mashtaka hayo mbele ya hakimu mkazi Benadictor Beda.

Mwendesha mashtaka Batseba Kasanga alimwambia hakimu Beda kuwa katika shtaka la kwanza mtuhumiwa aliiba gari aina ya Toyota OPA mali ya Abdul Ngalawa.

Kwa mujibu wa Kasanga tukio hilo lilifanyika Novemba 27 mwaka jana eneo la Magomeni jijini Dar es Salaam.

Mwendesha mashtaka huyo alifafanua kuwa katika tukio hilo, mtuhumiwa alipewa gari hilo na mlalamikaji ili akaiuze kwa Sh10 milioni na kumpa fedha hiyo lakini, baada ya kuiuza, hakumpelekea fedha wala kumrudishia gari yake.

Kasanga alizidi kudai mahakamani hapo kuwa Desemba 19, mwaka jana, kwa njia ya ulaghai, mtuhumiwa alijipatia magari mawili yenye namba aina ya Toyota IPSAM na Toyota NADIA mali ya Asma Miraji.

Alisema mtuhumiwa alipewa magari hayo kwa makubaliano kuwa angeyarudisha baada ya siku kumi lakini, hakufanya hivyo.

Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka huyo, katika shtaka lingine Manara alijipatia pia Sh5 milioni kutoka kwa Jocob Manyanga kwa makubaliano kuwa angemuuzia gari lake, kitu ambacho hakufanya.

Alisema tukio hilo lilitokea Januari tano mwaka huu manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Kasanga alimweleza hakimu Beda kuwa Desemba 20 mwaka jana, eneo la Magomeni mtuhumiwa huyo alijipatia tena Sh3 milioni kutoka kwa Wilson Matimba kwa makubaliano ya kumuuzia gari yake.

Alisema pia Januari 29 mwaka huu eneo la Magomeni saa 11:00 jioni, Manara alijipatia Sh19 milioni za mkopo kutoka kwa Dotto Hussein akieleza kuwa yeye ni mfanyabiashara na kwamba angemrudishia fedha hiyo baada ya siku tano.

Mwendesha mashtaka huyo aliendelea kudai mahakamani hapo kuwa Manara pia alijipatia Sh36 milioni kutoka kwa Fadhili Mtandika mkazi wa eneo Magomeni jijini Dar es Salaam kwa njia ya utapeli.

Alisema mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Januari 13 mwaka huu saa 2:00 usiku.

Hata hivyo mtuhumiwa huyo alikana makosa yote sita na kurudishwa rumande kwa kukosa dhamana hadi Machi 4 mwaka huu kesi hiyo itakapoendelea.

Mtuhumiwa aliswekwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ambayo ni pamoja na kuwa na wadhamini wawili wanaofanyakazi zinazofahamika, wawe na mali isiyohamishika yenye thamani ya Sh 35milioni au fedha tasilimu Sh 17milioni.Ummy Muya

Wednesday, February 17, 2010

Maunga adakwa na dawa za kulevya



HALID Salim Maunga (35), raia wa Uingereza aliyekuwa na hati ya kusafiria namba 109483453, juzi asubuhi alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam na kete 69 za madawa ya kulevya aina ya cocaine pamoja na bangi gramu 610.

Akizungumza na Mwananchi jana, Kamishna Msaidizi wa Polisi wa viwanja vya ndege nchini, Mwajuma Kiponza alisema Halid alikamatwa na askari wa Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na maofisa wa Mamlaka ya viwanja vya Ndege (TAA) wakati akiwa katika hatua za mwisho za ukaguzi katika uwanja hapo.

Alisema polisi pamoja na maofisa hao, walimtilia mashaka raia huyo, wa Uingereza aliyekuwa amefikia maeneo ya Makumbusho jijini Dar es Salaam na kuanza kumpekua na walibaini alificha kete 16 kwenye pindo la suruali yake sehemu ya kiunoni na kete 14 zilikutwa katika pindo ya chini ya suruali yake.

“Baada ya kumgundua kuwa amebeba vitu hivi polisi walimkamata na kumpeleka kituoni kwa ajili ya kumhoji zaidi, lakini walipofungua begi lake walikuta vinyago vitatu ambavyo vilikuwa na kete hizo za madawa ya kulevya pamoja na bangi.

“Vinyago hivyo vilikuwa na mfano wa mnyama na binadamu na kimoja kilikutwa na bangi pamoja na kete 21 za madawa ya kulevya na kingine kilikutwa na bangi pamoja na kete 18 na hivyo kufanya jumla ya kete hizo kuwa 69, alikuwa akienda nchini Uingereza na ndege ya Shirika la ndege la British Airways,” alisema Kiponza

Alisema baada ya kumhoji aliwaeleza kuwa alikuwa akiishi maeneo ya Makumbusho na Polisi walifika mpaka nyumba aliyokuwa akiishi, lakini hawakufanikiwa kukamata kitu chochote.

Alifafanua ndugu wa Halid walithibitisha kumfahamu ndugu yao ila walipoulizwa kazi anayoifanya walidai hawaifahamu na kufafanua kuwa wanachokijua ni kuwa ndugu yao anaishi nchini Uingereza.

Alipoulizwa swali na gazeti hili, njia zinazotumiwa na jeshi hilo kuwabaini watu mbalimbali wanaobeba madawa ya kulevya, Kiponza alisema; “kitu cha kwanza kinachotusaidia ni mashine zilizopo pale uwanjani, sikatai wapo wanaopita ila huwa tunakuwa makini sana hasa kwa wasafiri ambao hutoka au kwenda nchi ambazo zinasifika kwa biashara za madawa haya.”

Alisema wanatunza kumbukumbu za hati za kusafiria za wasafiri wanaokwenda katika nchi hizo na kunakili tarehe wanazoondoka na watakayorejea ili iwe rahisi kwao kuwafuatilia licha ya kuwa wakati mwingine wasafiri hao hurudi bila kuwa na mzigo wowote. Fidelis Butahe na Zaina Malongo: SOURCE:: MWANANCHI

mwana wa mkulima afuata kilimo Rome


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Rais wa IFAD, Dk. Kanayo Nwanze kabla ya kuhutubia mkutano wa IFAD jijini Rome, Italia alikomwakilisha Rais, Jakaya Kikwete. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Wanafunzi Temeke wafunga barabara



ZAIDI ya wanafunzi 1000 wa shule za msingi za Umoja na Miburani zilizoko Temeke Dar es Salaam, jana walifunga barabara kwa zaidi ya saa nne na kusababisha vurugu kubwa katika eneo la Sudani, makutano ya Barabara ya Tandika na Temeke.

Huku wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe wa kutaka eneo hilo liwekewe matuta, wanafunzi hao waliokuwa na silaha mbalimbali, walirusha mawe hovyo na wengine kurukaruka barabarani.

Vurugu hizo pamoja na zile za kurushia mchanga magari, zilisababisha msongamano mkubwa wa magari katika eneo hilo.

Habari zilizosema fujo hizo zilitokana na mmoja wa wanafunzi hao kugongwa na daladala.

Kwa mujibu wa habari hizo, tukio hilo ni la tatu kutokea katika eneo hilo. Juzi mwanafunzi mmoja alinusurika kugongwa na gari na mwingine aligongwa na guta.

“Hatutoki hapa mpaka matuta yajengwe leo, serikali mbona mnatuua, Jengeni matuta basi, hapa hakieleweki tunataka haki yetu.” alisema mmoja wa wanafunzi hao.

“Tumeenda wilayani eti wanatuambia turudi shuleni watakuja kujenga matuta baada ya siku tatu lakini, sisi bado tunakuja shule na kuvuka barabara hii, hatudanganyiki,” alisema mwingine.

Mashuhuda wa tukio hilo walilieleza gazeti hili kuwa saa 1:00 asubuhi ya jana, mwanafunzi Abdul Idrisa wa darasa la pili katika Shule Msingi Umoja, aligongwa na daladala iliyokuwa inatoka Tandika kuelekea Kariakoo.

Mwanafunzi huyo alipata majeraha makubwa sehemu mbalimbali za mwili na kukimbizwa katika Hospitali ya Temeke kwa matibabu.

Hata hivyo Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke, Dk Gilbert Buberwa, alisema hali ya mwanafunzi huyo inaendelea vizuri.

“Tulimpokea mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka saba, saa 3:00 asubuhi na baada ya kumfanyia X-ray, tumegundua kuwa amejeruhiwa maeneo ya miguuni lakini, uchunguzi bado unaendelea," alisema Dk Buberwa na kuongeza; Habari imeandikwa na Felix Mwagara: SOURCE: MWANANCHI

'Haturidhiki na uamuzi wa bunge kuhusu Richmond'



WANAHARAKATI wa FemAct na vikundi vingine vya kiraia nchini wameeleza kutoridhishwa na kushtushwa na utendaji wa Bunge na Wabunge baada ya kushindwa kuchukua hatua madhubuti dhidi ya kashfa ya Richmond na nyingine.

Kutokana na hatua hiyo wananaharakati hao, wametangaza kuandaa maandamano nchi nzima kuonyesha kutoridhishwa na utendaji wa Bunge.
Aliema wananchi watahamasishwa kuonyesha hasira dhidi ya chombo hicho na kudai mfumo mbadala wa demokrasia nchini.

Wakitoa tamko la pamoja lililoshirikisha asasi na vyama vya kiraia zaidi ya 50, makao makuu ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) jijini Dar es Salaam, wanaharakati hao wamelitaka Bunge kujisafisha kwa kuweka maslahi taifa mbele badala ya maslahi ya vyama na wabunge binafsi.

“Tofauti na matarajio ya wananchi, Bunge limemaliza kikao chake bila kuchukua hatua madhubuti kuhusu kashfa ya Richmond, Kiwira, Ticts, TRL, Loliondo na North Mara. Jambo hili limetushtua na kutusikitisha sana,” alisema Kaiza Buberwa mkurugenzi wa asasi ya Fordia.

“Sisi wananchi tunanona kuwa Bunge limeshindwa kutekeleza wajibu wake kikatiba wa kuisimamia serikali, kutokana na mfumo mbaya wa madaraka na uwajibikaji kati ya serikali na bunge unaoruhusu maslahi ya chama tawala kuchukua hatamu kuliko maslahi ya taifa,” alisema Buberwa.

“Tunapendekeza Bunge lijisafishe na kuweka maslahi ya taifa mbele kuliko maslahi ya vyama na wabunge binafsi,” alisema mkurugenzi wa kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Francis Kiwanga.

“Kama Asasi za kiraia tumeamua kuandaa maandamano makubwa ya kitaifa kuonyesha kutoridhishwa na utendaji usioridhisha wa Bunge la sasa na kudai mfumo mbadala wa demokrasia shirikishi ambao una uwezo zaidi kutetea maslahi ya wananchi,” alisema.

Wanaharakati hao walibainisha kuwa fedha zilizopotea katika kashfa ya Richmond zinazofikia Sh173 bilioni zingeweza kutosha kujenga nyumba19,211 za walimu wa shule ya msingi huku kila shule ikigharimu Sh9 milioni.

Walisema kutokana na mfumo uliopo hivi sasa, ni vigumu Bunge kuiwajibisha serikali na ndiyo sababu Bunge limefunika kisiasa kashfa za Richmond, mgodi wa makaa ya mawe Kiwira, TRL na Ticts. Imeandikwa na Exuper Kachenje: SOURCE -MWANANCHI

Tuesday, February 16, 2010

President Kikwete praises Karimjee Family


H.E. Excellency Jakaya Mrisho Kikwete, The President launched the Karimjee Jivanjee family book on Saturday February 13th from 5.00pm to 8.00pm at an exclusive function at the Kilimanjaro Kempinski Hotel.

Hatim A. Karimjee, Chairman of Karimjee Jivanjee Ltd began by welcoming H.E. The President, the Honorable Minister of Home Affairs Lawrence K. Masha, MP, Honorable Regional Commissioner for Dar es Salaam William Lukuvi, Ambassadors and distinguished guests including Karimjee Jivanjee family members visiting from the UK, Mauritius and Pakistan.

He began by saying “This is a very special day for the Karimjee Family because it has been our intention to write this history for many years and finally it has been achieved. This book has taken three years of research and writing”.

He congratulated Professor Gijsbert Oonk for writing an excellent book, well illustrated with many historical photos. He continued by highlighting Professor Oonk’s strength as an academic and a historian and his approach which was always to cross reference and look for other sources to reach the truth.

The book which records the 200 year history of the family is firstly a fascinating adventure story and secondly is a tribute to the Karimjee family’s ancestors who crossed the “kali pani” in a dhow from India to Africa at the beginning of the 19th Century. Having reached Zanzibar, the family ancestors prospered in the face of amazing difficulties through determination, hard work and an enterprising spirit. SOURCE KARIMJEE FAMILY

Msekwa ammwagia sifa Spika Sitta


Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara) Pius Msekwa akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mjini Dodoma leo. Kulia ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NEC, John Chiligati. Picha na Jube Tranquilino.

*************************************************

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa amemmwagia sifa Spika wa Bunge Samuel Sitta kwa kile alichoeleza kuwa amefanikiwa kumaliza sakata la Richmond kwa busara kubwa.
 
Akizungunza na waandishi wa habari jana mjini Dodoma leo, Msekwa alisema sababu ya uhasama wa wabunge wa CCM, Msekwa alisema yalitokana na sakata lililoibuliwa mwanzoni mwa mwaka 2007 na kusababisha mtikisiko mkubwa ndani ya serikali ya awamu ya nne.

CCM iliingia kwenye mtafaruku uliotengeneza makundi mawili makubwa mwaka 2008 baada ya sakata la Richmond kutinga bungeni na kisha kuwakumba baadhi ya makada wa juu wa chama hicho, waliotuhumiwa kuhusika na kashfa hiyo ya kifisadi iliyotokana na zabuni tata ya uzalishaji umeme wa dharura iliyoipa ushindi kampuni hiyo(Richmond).

Baadhi ya makada wa chama ngazi za juu katika chama na serikali, akiwemo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na mawaziri wawili walioitumikia Wizara ya Nishati na Madini kwa nyakati tofauti wakati wa mchakato wa zabuni hiyo, Dk Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi walilazimika kujizulu kutokana na kudaiwa kuhusika katika sakata hilo, huku maofisa wengine wa umma wakitakiwa kuchukuliwa hatua na serikali.
 
Alisema baada ya sakata hilo kulipuka kulitokea mgawanyiko mkubwa katika chama uliozaa makundi mawili. Alitaja vinara wa makundi hayo kuwa ni mbunge wa Monduli Edward Lowassa na Spika wa Bunge, Samuel Sitta.
 
Kwa mujibu wa Msekwa makundi hayo kila moja lilikuwa likituhumu kundi jingine kuwa lina nia ya kuwang’oa wenzao madarakani, jambo hilo lilileta mtafaruku mkubwa.
 
“Tumewaita vinara wa makundi hayo na kukaa nao meza moja. Lakini hatukuwa na nia ya kutaka kuwatoa kafara kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari, bali tulitaka amani idumu jambo linaloonyesha kuwa tumefaulu,” alisema Msekwa na kuongeza:
 
“Pamoja na kukaa nao kwa muda wa saa nne katika moja ya kumbi za pale bungeni, kila mmoja alikuwa na kero zake jambo tulilogundua kuwa kila mtu alikuwa akifagilia kitumbua chake kisiingie mchanga”.
 
Katika kile kinachoweza kutafsiriwa kama ni kumtonesha kidonda jana Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, Msekwa alimfagilia spika Sitta kwa kumaliza sakata la Richmond na kisha kuonya kuwa watakaoliendeleza watachukuliwa hatua.
 

Miss Tanzania apata dhamana


Miss Tanzania, Miriam Gerald, akiwa na ndugu zake kuelekea nyumbani baada kudhaminiwa na mkurugenzi wa mashindano hayo Hashim Lundenga kwenye mahakama ya hakimu mkazi Kinondoni jijini Dar es Salaam jana. Miriam pamoja na rafiki yake wa kiume Kenedy Victor wanashtakiwa kwa kosa la kujeruhi na kuharibu mali na wote wamekewa dhamana. Picha na Silvan Kiwal

******************************************************************************************************************

HATIMAYE Miss Tanzania 2009, Miriam Gerald ameachiwa kwa dhamana baada ya kukaa rumande kwa siku tatu, kuanzia Ijumaa mchana kwa kukosa dhamana.

Mrembo huyo wa mwaka jana, alipelekwa rumande kwa kile kilichoelezwa kushambulia pamoja na kuharibu mali.

Katika shtaka la kwanza, wanatuhumiwa kumshambulia Shaaban Moshi kwa vitu vyenye ncha kali shtaka lililosomwa na mwendesha mashtaka Inspekta wa Polisi, Nassor Sisiwahy, mbele ya Hakimu, Kwey Lusemwa.

Shitaka la pili, watuhumiwa kufanya uharibifu wa mali yenye thamani ya Sh laki 720,000. Mali iliyoelezwa ni vifaa vya muziki. Ijumaa walishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kupelekwa Gereza la Segerea.
Hata hivyo, jana alipata dhamana pamoja na rafiki yake, Kennedy Victor.

Baada ya kuruhusiwa na mahakama, Mratibu wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga aliwaomba radhi Watanzania kwa yanayotokea kwa washindi wa taji hilo.

Lundenga aliyasema hayo jana nje ya Mahakama ya Kinondoni baada ya kumwekea dhamana mrembo wake na kusema: "Hayo ni mambo ya kimaisha na yanaweza kumtokea yeyote."

Mrembo huyo aliwasili mahakamani hapo saa 5.15 asubuhi akiwa kwenye gari aina ya Land Cruizer STK 4253 ambalo liliingia Mahakamani hapo kwa kasi akiwa na wenzake wawili na Miriam alishuka akiwa amejifunika mtandio usoni.

Baada ya hapo, saa 11.30 washtakiwa hao walipandishwa kizimbani na Hakimu Richard Kabate ambaye aliwaachia kwa dhamana kwa niaba ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Kwey Lusema.

Wote walitimiza masharti ya dhamana yao na kuwataka kurudi tena mahakamani Februari 25 .

Lundenga alitoa dhamana hiyo kwa mrembo wake Miriam huku Kennedy akitolewa dhamana na rafiki yake Omary Juma Idd ambaye ni mfanyakazi wa Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.

'' Siwezi kuongea mengi kwa kuwa kesi bado ipo mahakamani ila naweza kusema kuwa yaliyomtokea Miriam ni matatizo tu ya kimaisha hatutakiwi kumlaumu kwani mpaka sasa bado hatujajua kama kosa hilo katenda au la,'' alisema Lundenga.

Aidha Lundenga alisema kuwa kwa kitendo alichofanyiwa Miriam si cha kistaarabu na kamati yake inawatafuta warembo hao wanasheria na wanapopatwa na matatizo wawe wanaongea na sio warembo wenyewe. SOURCE: MWANANCHI

Monday, February 15, 2010

Bia za TBL sasa bei juu


WANYWAJI wa bia zinazotengenezwa na kiwanda cha Tanzania Breweries Limited (TBL) sasa itabidi wajitutumue zaidi kugharimia starehe hiyo kutokana na bei ya bidhaa hizo kuongezeka.

Afisa Uhusiano wa TBL, Doris Malulu alisema kwamba bei hiyo mpya itaanza kutumika kuanzia leo.

Malulu alisisitiza wauzaji wa rejareja kuuza kwa bei iliyoidhinishwa na TBL ili kuepuka dhuluma na kuwaongezea mzigo wanywaji.

Hata hivyo, uchunguzi wa Mwananchi umebaini kwamba kama bei hiyo mpya itazingatiwa hasa kwa jiji la Dar es Salaam, huenda isiwe ni jambo la ajabu kwa sababu baa nyingi tayari zilianza kutumia bei hiyo tangu Julai, mwaka jana.

TBL walijaribu kupambana na walanguzi hao tangu mwaka jana kwa kusambaza vibao ili vibandikwe kwenye mabaa na kuonyesha bei halisi, lakini baadhi ya mabaa walivitupilia mbali na kuuza kwa bei wanazotaka wao.

Kwa mujibu wa bei hiyo mpya iliyotangazwa na TBL jana, bia za Safari, Kilimanjaro, Tusker, Bingwa na Balimi ambazo zinauzwa kwa ujazo wa mililita 500, sasa bei yake halisi ni Sh1,400 badala ya bei ya zamani ya sh1,300.

Aina ya bia hizo, ambazo zinauzwa katika ujazo wa mililita 330, badala ya Sh1,100 sasa zitauzwa kwa Sh.1,200, isipokuwa Balimi ambayo itakuwa Sh1,000.

Akifafanua zaidi juu ya bei hiyo mpya, Malulu alisema kwa ujumla bei ya bia zote kwa rejareja zimeongezeka kwa Sh100.

Bei mpya ya aina nyingine za bia za TBL pamoja na kiwango cha ujazo wa mililita kwenye mabano ni Ndovu Special Malt (375) Sh1,400, Castle Lager (500) Sh1,500, (330) 1,300, Castle Milk Stout (500) Sh1,600 na (375) Sh1,300.

Guinness (500) Sh1,800, Redd’s Premium Cold (330) na (375) Sh1,400 wakati bia zinazopatikana zaidi Kanda ya Kaskazini za Eagle (500) Sh1,100 na (300) Sh700.

Kwa mujibu wa bei hizo mpya, Kinyaji kisicho na pombe cha Guinness Malt (300) kitauzwa kwa Sh900 na (330) Sh1,100.

Malulu alizitaja sababu za kupanda kwa gharama za vinywaji wanavyozalisha kuwa ni kutokana na kupanda kwa gharama za uzalishaji na usafirishaji.
“Bei zimepanda kutokana na sababu mbalimbali miongoni ikiwa ni pamoja na kupanda kwa gharama za malighafi, usafirishaji, kupanda kwa bei ya mafuta na kushuka kwa thamani ya shilingi,” alisema Malulu.

Alisisitiza kwamba matangazo ya viwango vipya vya bei ya jumla na rejareja tayari wameyachapishwa na yatasambazwa kwenye baa na maduka yote ya jumla nchini. imeandikwa na Leon Bahati. SOURCE MWANANCHI

watano wafa kwa kuangukiwa na kifusi

Watano wafariki dunia
kwa kufukiwa na kifusi

Israel Mgussi, Dodoma

WATU watano wamefariki dunia papo hapo na wengine wawili kujeruhiwa baada ya kufunikwa na kifusi kwenye machimbo ya kokoto yaliyopo katika kijiji cha Ntyuka, nje kidogo ya mji wa Dodoma.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Salum Msangi, waliopoteza maisha katika tukio hilo kuwa ni Mwajuma Mnubi, Monika Chizumi, Mbeleje Ndigomba wote wakazi wa kijijini hapo na Jonasi Mnubi (2) na jina la marehemu mmoja halikupatikana. Hata hivyo, majina ya waliojeruhiwa hayakuweza kupatikana.

Msangi alisema tukio hilo lilitokea mnamo saa 5 asubuhi, lakini polisi walipata taarifa majira ya saa 6 mchana na kwamba, uokoaji ulianza saa 7 mchana hadi saa 10 jioni.

“Tulifika eneo la tukio kwenye saa 7 mchana na kuanza kufukua kifusi tukisaidiana na wafanyakazi wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA)ambao walitoa katapila lililosaidia kwa kiasi kikubwa kufukua udongo,” alisema.

Mashuhuda hao walisema, marehemu hao ambao walisimama kwenye gema karibu na shimo hilo, walijikuta katika wakati mgumu baada ya udongo wa mahali walipokuwa wamesimama kumeguka na kutumbukia shimoni na kufukiwa kabisa.

Kutokana na shimo hilo kuwa kubwa walishindwa kutoka na wala watu wengine walishindwa kuwanusuru kutokana na kiasi kikubwa cha udongo uliowafunika.

“Tukio hili lilitokea muda wa saa tano asubuhi, lakini tulishindwa kuwaokoa wakiwa hai kutokana na kiasi kikubwa cha udongo kilichomeguka na kufunika kabisa shimo, hivyo tuliamua kuomba msaada polisi na uokoaji ulianza rasmi saa saba mchana baada ya wanausalama hao kufika,” walisema mashuhuda wa tukio hilo.

Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Dk James Msekela alishiriki kikamilifu katika ufukuaji wa shimo hilo na alitoa kiasi Sh50,000 kwa kila familia ya marehemu hao na kuwatahadharisha watu wanaojihushisha na uchumbaji wa kokoto kuwa makini ili wasije wakakumbwa na balaa kama hilo.

Kijiji cha Ntyuka ni maarufu kwa shuguli za uchimbaji wa kokoto zinazotumika katika ujenzi na asilimia 80 ya shughuli za ujenzi mjini Dodoma hutegemea kokoto za kutoka eneo hilo.

CCM mambo juu ya mambozz

Source TBC.

Mpaka sasa mkutano haujaisha ila Taarifa toka Dodoma, ni kuwa wajumbe karibu wengi kwenye mkutano wa NEC ya CCM wanapendekeza kamati ya Mzee Mwinyi iongezwe muda ili kuweza kuendelea kumalizia tofauti zilizopo baina ya wana CCM.

Katibu mwenezi wa CCM, kutoa taarifa rasmi mara tu baada ya mkutano kumalizika hata iwe saa nane ucku, atakuwa na press confrence muda huwo!!!!!!!

Lakini suala bajeti ya uchaguzi ndani ya CCM na mvutano baina ya makundi ndani ya chama ni miongoni mwa mambo yaliyozua mvutano katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (Nec) uliyomalizika jana na kushindwa kufikia hitimisho na badala yake inadaiwa kuwa walilishana yamini ili mambo yaishe.

Mazingira hayo pia yaliwafanya wajumbe wa mkutano huo kuitaka Kamati ya Mzee Ali Hassan Mwinyi iliyopewa jukumu la kuchunguza kiini cha mparaganyiko ndani ya chama hicho tawala, hivyo kuiongezea muda ili kuweka sawa baadhi ya mambo ambayo hayakuwa na majibu ya kujitosheleza.

Suala la maridhiano ya Zanzibar pia linadaiwa kuwasha moto katika mkutano huo ikidaiwa kwamba, kulikuwa na mvutano mkali miongoni mwa wajumbe, huku baadhi wakitaka tarehe ya uchaguzi wa rais wa Zanzibar isogezwe mbele na wengine wakipinga.

Sunday, February 14, 2010

CCM Mambo mazito


Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM wakiwa wamesimama kumkumbuka Katibu Mkuu wa CCM Mstaafu hayati, Rashidi Kawawa kabla ya kuanza kwa mkutano wao Mjini Dodoma Februari 14, 2010. Kulia ni Makamu wa Rais, Dk. Ali MohamedShein na wapili kulia ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM na Mawaziri Wakuu Wastaafu, Frederick Sumaye (kushoto ) na Edward Lowassa , wakiteta kabla ya kuanza kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma , Februari 14, 2010. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM na Spika wa Bunge, Samuel Sitta (kulia) akisalimiana na wajumbe wenzake ambao pia ni Mawaziri Wakuu wastaafu, Frederick Sumaye (kushoto) na Edward Lowassa (katikati) kablaya kuanza kwa mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Mjini Dodoma Februari 14, 2010..(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

JK atangaza Malaria janga la taifa



RAIS Jakaya Kikwete ameutangaza ugonjwa wa malaria kuwa ni Janga la Taifa na kuwaambia Watanzania kuwa Serikali yake imeanza safari ya kuutokomeza ugonjwa huo nchini. Malaria ndiyo ugonjwa unaoua Watanzania wengi zaidi kuliko mwingine wowote.

Rais Kikwete ambaye ni mwenyekiti wa marais wanaopambana na malaria barani Afrika alisema kwamba, ugonjwa wa malaria ni vita ambavyo ni lazima Watanzania wavishinde kwa vile nia ipo, sababu ipo na uwezo upo.

Aliongeza kusema kuwa, lengo la serikali ni kuhakikisha kuwa malaria inakuwa ugonjwa wa historia kwa Tanzania kwa kuwa hata nchi nyingine zimefanikiwa kuutokomeza.

Alisema kuwa kila siku ya Mungu, kiasi cha watu kufikia 291 hufariki kwa ugonjwa wa malaria, wengi wao wakiwa watoto wadogo, vifo ambavyo alivielezea kuwa vinaweza kuzuilika na kutibika.

“Kila siku ya Mungu, hapa nchini, wanakufa watu hadi 291 kwa ugonjwa wa malaria. Kwa maneno mengine, kila saa inayopita, wanakufa watu zaidi ya 10 kwa ugonjwa wa malaria.” Rais Kikwete aliliambia taifa usiku wa kuamkia jana.

“Hawa ni watu wengi mno. Hivyo, malaria ni Janga la Taifa letu. Lakini cha kusikitisha zaidi ni kwamba malaria ni ugonjwa unaoweza kuzuilika na kutibika. Ndiyo maana tumeamua kuwa wakati tunaendelea kushughulikia kutibu wagonjwa wa malaria, tuelekeze nguvu zetu katika kuzuia kwa kuanza juhudi za kutokomeza malaria nchini.”

Rais Kikwete alikuwa akizungumza moja kwa moja na taifa wakati anazindua Kampeni dhidi ya Malaria katika burudani maalumu iliyofanyika kwenye Viwanja vya Leaders Club mjini Dar es Salaam juzi usiku.

Kampeni hiyo imeanzishwa kwa ushirikiano baina ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii nchini na taasisi za Malaria No More, Population Services International (PSI) na Chuo Kikuu cha John Hopkins, vyote vya Marekani.

&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

Wabunge wapya wateule wa Rais


Mbunge wa Kuteuliwa, Ismail Jussa Ladhu, akiapa Bungeni Mjini Dodoma juzi ijumaa

Mbunge wa Kuteuliwa, Janet Zebedayo Mbene akiapa Bungeni Mjini Dodoma juzi ijumaa. Picha za Edwin Mjwahuzi.