Thursday, February 26, 2009

Profesa Saffari: CUF wamenidhalilisha



SIKU mbili baada ya kuangushwa vibaya katika kinyang'anyiro cha uenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Abdallah Safari amesema wajumbe wa mkutano mkuu walimdhalilisha na kwamba anaandaa kitabu kueleza udhalilishaji huo.
Profesa Safari alitoa malalamiko hayo leo kuhusu matokeo ya uchaguzi huo uliomrudisha madarakani Profesa Ibrahim Lipumba, aliyepata kura 646, huku mpinzani huyo akiambulia kura sita tu.
Wakati Profesa Safari akijieleza, wajumbe walikuwa wakimzomea na baadaye kumrushia maswali yaliyomtingisha, ikiwa ni pamoja na kutaka ataje jina la katibu wa tawi lake, swali ambalo alibabaika kulijibu.
"Nimedhalilishwa; nimezomewa; nimeulizwa maswali ya kipuuzi. Ule ni uhuni hakuna kitu pale," alisema Profesa Safari.
"Wajumbe wa mkutano mkuu wa CUF wamepotosha na kuharibu maana ya demokrasia ndani ya CUF na kutumia vibaya nafasi hiyo ya kuchagua viongozi."
Alipobanwa kueleza iwapo anafikiria kuwania tena nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama hicho, Profesa Safari alisema hawezi na hana nia ya kuwania uongozi wa chama hicho.
"Sifikirii wala sina nia tena ya kuwania nafasi yoyote ndani ya CUF. Nitakapoita mkutano na waandishi wa habari, nitaeleza mengi. Mbali ya kuzindua kitabu changu, nitaamua shauli la kufanya pamoja na kesi ya uanachama wangu," alisema Profesa Safari. Habari ya Salim Said.

Ban: Afrika inaweza kuondokana na umasikini






Africa has potential to uplift its people fro poverty and it was a misconception to believe that it was a black continent, the UN secretary general, Ban Ki-moon said at a public lecture in Dar es Salaam yesterday.

He made the remarks shortly after he received harmonious welcome at the Mwalimu Julius Nyerere terminal one with flamboyant parade and traditional dances.

He pointed out that with a goodwill and commitment, the continent could unlock its full potential in a matter of time.

He named several countries he described as “seas of hope” that have provided examples that demonstrate that capability naming Tanzania, Malawi, Kenya and Uganda as examples of countries which have performed extremely well.

In case of Tanzania, the UN chief said it has demonstrated exemplary performance in school enrolment with Malawi doing recommended job to improve agricultural production.

He said Kenya has done well in children immunisation while Uganda’s efforts to control HIV/Aids was unmatched by many countries around the world.

“These examples show that Africa can do it if there is commitment,” he said at a public lecture attended by members of the diplomatic cop, ministers, business community and the general public.

Ki-moon pledged the UN commitment and support to such countries noting that their performances have demonstrated that together they can confront poverty among their people.

But Ki-moon had a message for Africa and its leaders saying the continent was tired of endless conflicts and crisis that stall development and progress.

He used the public lecture to remind developed countries of Africa’s critical situation that require global concerted efforts to avoid slipping back in success cases.

He noted that the global economic recession, climate change, food insecurity and war could stagnate and erode achievements by countries to meet the Millennium Development Goals (MDGs).

Wednesday, February 25, 2009

Lipumba mwenyekiti tena



PROFESA Ibrahim Lipumba jana aliongoza viongozi wenzake wa Chama cha Wananchi (CUF) kuibuka na ushindi mkubwa kwenye uchaguzi mkuu wa chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam.

Lakini alikuwa ni katibu wake, Seif Sharif Hamad aliyeongoza kwa kura nyingi alipoibuka na ushindi wa asilimia 99.5, akiwa hana mpinzani katika kinyang'anyiro cha nafasi hiyo.

Kwa mujibu wa Jaji Usi Haji Usi aliyetangaza matokeo hayo, Prof. Lipumba, ambaye alikuwa akichuana na Profesa Abdallah Safari na koplo Stephen Masanja, alishinda kirahisi nafasi ya uenyekiti alipozoa kura 646, ambazo ni asilimia 97 ya kura zote na kurudi kwenye nafasi yake atakayoishikilia kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

Kura zote zilikuwa 665 upande wa Mwenyekiti tatu ziliharibika
646 Lipumba asilimia 97

Safari alipata kura asilimia 0.8

Masanja kura 10 ambazo ni asilimia 1.5

Kura zote za katibu mkuu 659
zilizoharibika 2
hapana 4

ndio 651 na ushindi ni asilimia 99.5

makamu kura zote 657

zilizoharibika 5

hapana 4

644 ambao ni ushindi wa asilimia 98.6

Tuesday, February 24, 2009

Liyumba apatikana azuka mahakamani

Picha ya Bongo pix
Mkurugenzi wa zamani wa utawala na utumishi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba, ambaye anadaiwa kutoweka, litajulikana leo wakati kesi inayomkabili ya tuhuma za kutumia vibaya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya Sh 221 bilioni, ameonekana leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu.

Liyumba ameingia mahakamani hapo akiwa katika gari lake binafsi la kifahari na alishuka katika gari lake bila ya wasi tofauti na ilivyokuwa ikiriupotiwa ya kwamba mtuhumiwa huyo alikuwa akitafutwa kwa udi na uvumba. Kupatikana kwake kumeondoa utata uliokuwapo siku za nyuma kuhusu kuwapo au kutoroka kwake.

Alikuwa akisakwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), muda mfupi baada ya kupewa dhamana katika mazingira yenye utata na taasisi hiyo, ambayo sasa ina uwezo wa kuendesha kesi, ilipewa kibali cha kumkamata, lakini ilishindwa kumtia nguvuni na hivyo kusababisha uvumi kuwa mtuhumiwa huyo ametoweka.

Mtuhumiwa huyo, ambaye ameshtakiwa kwa pamoja na Deogratius Kweka ambaye bado yuko ndani, alimudu kutoka mahabusu baada ya mahakama kukubali hati moja yenye mali za thamani ya Sh882 milioni katika dhamana ya thamani ya Sh55 bilioni, baada ya hati kadhaa kuonekana kuwa na kasoro, ikiwemo ya kusafiria ambayo ilionekana kuisha muda wake. Taarifa zaidi bidae.

Mhindi aliyeua yuko hai


Baada ya kukaa kimya kwa muda baada ya taarifa za utata za kifo cha Komal Katakia, 22, raia wa India ambaye anatuhumiwa kumuua mtu mwingine mwenye asilia ya asia, leo ameibukia mahakamani Kisutu leo yu bukheri wa afya, sasa sijui taarifa za mwanzo zililenga kutupotosha ili wamtoroshe nje ya nchi ili wadai amekufa au sijui ni vipi

Kesi ya Komal na mumewe, Vinosh Praven, ambao wanatuhumiwa kumuua mfanyabiashara, Abdulbasiti Abdallah, 21 wakati huo huo Mamlaka ya Magereza imetoa ufafanuzi kuwa yule mama wa kihindi aliyedaiwa kufariki duniani akiwa gerezani ama kwa kujinyonga au kuuawa kwa mateso Soma Zaidi kuwa bado yuko hai na ni mzima buheri kwa afya. Taarifa hizo zilianza kuzagaa Ijumaa iliyopita na kukolea zaidi Jumamosi namna hii, lakini Msemaji wa Magereza amesema ni uzushi na huyo mama yuho hai.

Monday, February 23, 2009

Kombe la Afrika




wasichana na wavulana wakishiriki katika ufunguzi wa michuano ya CHAN jijini Ivory Coast. Picha zote za saleh Ally

Bongo star search


baadhi wa washirishiriki wa shindano la Bongo Star search kanda ya kaskazini wakiwa katika mstari mrefu kwa ajili ya kufanya usaili wa uimbaji/picha na Emmanuel Herman

Sunday, February 22, 2009

Mhindi aliyeua mwenzie afia jela


Yule binti wa kihindi, Komal Katakia(22) aliyeolewa na Vinoth Praven (23) raia wa India anayedaiwa kuua muhindi mwenzie anaelezwa kufia gerezani mwishoni mwa wiki.
Binti huyo amabye alionja lupango baada ya mumewe kudaiwa kumuua Abdulbasiti Abdallah (21) alilazimika kuunganishwa katika mashtaka ya mumewe nae akaenda Keko.
Habari za kifo cha Komal zilianza kuenea jijini hapa kuanzia juzi Ijumaa huku baadhi ya watu wakidai kuwa ameuawa na wengine wakisema kuwa amejinyonga.
Taarifa za awali zinasema kuwa mwili wake umepelekw amuhimbili ukiwa na majereha kadhaa, habari zaidi baadae.

Friday, February 20, 2009

vijana wamekwiva si mchezo


Baadhi ya wanajeshi waliohitimu mafunzo ya awali ya kijeshi katika shule ya mafunzo ya awali ya kijeshi ya Makutupora mkoani Dodoma wakionyesha umahiri wakati wa kufunga mafunzo hayo jana. Jumla ya vijana 1306 wamehitimu mafunzo hayo kati ya 1310.

Thursday, February 19, 2009

Msekwa mwenyekiti mpya TCD


MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Pius Msekwa amesema, Mkurugenzi mkuu wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa Hassy Kitine ametumia haki yake ya kikatiba kutoa maoni kuhusu mwelekeo wa taifa.


Amesema yeye akiwa Kiongozi wa CCM hawezi kujadili maoni ya binafsi ya mtu kwani ni sawa na kuingilia haki yake.


Msekwa alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana alipotakiwa na Mwananchi kutoa maoni yake binafsi na CCM kufuatia kauli iliyotolewa na Kitine juzi kwamba tangu kipindi cha mwisho cha utawala wa Rais Benjamin Mkapa nchi, ilivurugika na kwamba maadili yameporomoka kuanzia ndani ya CCM.


Katika mkutano wake maalum na baadhi ya vyombo vya habari katika mgahawa wa Gymkana jijini Dar es Salaam pamoja na mambo mengine Kitine alisema mfano wa kuoza kwa maadili ndani ya CCM upo wazi pale waziri anapojiuzulu wadhifa wake kwa tuhuma, lakini bado anabaki kuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Mbunge.


Akizungumza na Mwananchi jana katika hoteli ya Regency, Msasani, Msekwa alisema "Sioni kama ni utaratibu mzuri kutolea maoni yaliyotolewa na mtu mwingine."


Alisema kutoa maoni ni haki ya kila mtanzania ambayo amepewa kikatiba ili mradi asivunje sheria, na kuongeza kuwa Kitine ametumia haki yake ya kikatiba.


"Kila mtanzania ana haki ya kutoa maoni ili mradi asivunje sheria," alisema Msekwa.


Aliongeza kuwa kwa maoni yake binafsi CCM haitazungumzia maoni ya mtu binafsi na wala si utaratibu mzuri kwa viongozi kuzungumzia na kutolea kauli maoni ya watu.

Liyumba aponyoka



KAMANDA Amatus Liyumba aliyekuwa Mkurugenzi wa utawala wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ametoweka na hajulikani alipo mpaka sasa kiasi kwamba Taasisi ya Kuzuia na kupambana na rushwa (PCCB) imeiomba mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu itoe hati ya kukamatwa kwake siku mbili baada ya kumwachia kwa dhamana.

Hati ya kukamatwa Liyumba na wadhamini wake wawili, ilitolewa juzi na hakimu Mkazi anayesikiliza kesi hiyo, Khadija Msongo.

Wakati Liyumba bado hajakamatwa, wadhamini wake jana walikamatwa na kuwekwa mahabusu ingawa baadaye waliachiwa baada ya hakimu kudai kuwa hawezi kutoa uamuzi wowote kutokana na jalada la kesi hiyo kuitishwa mahakama kuu.
Hakimu Msongo aliwataka wadhamini hao kufika mahakamani leo ambapo atatoa uamuzi.

Mwendesha Mashataka wa TAKUKURU, Tabu Mzee aliieleza mahakama kuwa juzi na jana, Liyumba ambaye ni mshtakiwa namba moja katika kesi ya kuisababishia serikali hasara ya Sh221 bilioni, hakuweza kupatikana kwa simu wala nyumbani kwake.

Liyumba na mwenzake Deogratias Kweka, walifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Januari 27 mwaka huu na kurudishwa rumande baada ya kushindwa kutoa Sh55 bilioni taslimu au hati ya mali isiyohamishika yenye thamani hiyo. Taarifa kwa kina soma www.mwananchi.co.tz

Tuesday, February 17, 2009

Joseph maina afariki dunia

Taarifa zilizotufikia punde tu zinaeleza kuwa yule gwiji wa muziki wa dansi na ambaye ni mmoja wa visiki vya bendi ya Msondo Ngoma Jazz Band bwana Joseph Maina amefariki dunia akiwa safarini ndani ya daladala akitokea maeneo ya Mbagala. Kwa sasa maiti ya mwanamuziki huyo tunaelezwa iko ndani ya hospitali ya Temeke imeshushwa na wasamaria wema. Maina kwa wale wasiomjua ni mwanamuziki mkongwe na mtunzi wa nyimbo nyingi lakini kubwa ni ile ya Baba Gift habari zaidi tutakuwa tukiendelea kuwaletea.

Mambo ya twanga




Duhhh mambo ya Valentine hayakuwa ya kawaida mwanangu hebu cheki mambo yalikuwa juu ya mambo na hata wewe mwenyewe ungekuwapo hakika ungenikubalia kweli ilikuwa si mchezo Twanga ungeipenda mwenyewe maanake ni kujimwaya mwaya tuuuu, au wasemaje

Sunday, February 15, 2009

Sauti za Busara





Kuna haja ya kuongeza ukubwa wa eneo, ama kupandisha bei za viingilio ili kuepuka msongamano ndani ya viwanja vya Ngome Kongwe pindi msimu wa Tamasha la kimataifa la Sauti za Busara utakapowadia tena hapo mwakani kutokana na kiwango kikubwa cha mahudhurio kinyume na ilivyotarajiwa.
Tofauti na miaka iliyopita, tamasha la mwaka huu lilitawaliwa sana na wageni, kutoka Tanzania Bara, Afrika Mashariki na Bara la Ulaya, hali ambayo ilisababisha hata upatikanaji wa malazi kwa wageni na usafiri wa kuingia Zanzibar kuwa wa taabu sana, na hata bei za vyakula kuwa juu zaidi tofauti na miaka iliyopita.
Likiwa ni tamasha la sita kufanyika, tangu kuanzishwa kwake, mwanzoni kulikuwa na shaka kwamba huenda lisifanikiwe mwaka huu kutokana na ushiriki mchache wa wasanii wa muziki wa kizazi kipya wa nyumbani, ambapo mwanamuziki pekee wa Hip Hop kutoka nyumbani Joh Makini ndio aliwakilisha muziki wa nyumbani lakini mambo yalikwenda kinyume.
Hii labda ilikuwa ni kutokana na kuhudhuriwa na wadau wengi wa burudani kutoka Ulaya, kikundi kama Segere Original kutoka Tanzania Bara, Cultural Music Troupe, Oudaden kutoka Morocco na Bi Kidude kutoka Zanzibar ambaye alizindua pia filamu ya maisha yake inayoitwa As Old as my tongue walionekana kutia fora kupitiliza.
Ukumbi wa Ngome Kongwe ambao una kawaida ya kuingiza watu 2500, ulionekana kujaa mara mbili ya kawaida ambapo wakazi wa Zanzibar ambao ni nadra sana kupata burudani walilazimika kuingia mapema ukumbuni, takriban masaa mawili kabla ya onesho kuanza ili kupata mahala pazuri pa kukaa patakapowawezesha kuangalia onesho kwa umakini zaidi.
Bi Kidude ambaye mwaka huu kwa mara ya kwanza alipanda jukwaani akiwa amevaa viatu, alikonga nyoyo za mashabiki wake ambao si kwa rika, wala jinsia, uwanja mzima walionekana kumfurahia tofauti na muziki wa kizazi kipya ambao walionekana kulazimisha mashabiki kupiga kelele na makofi, jambo ambalo lilidhihirisha kutofanikiwa kwao.
Tamasha, linatarajiwa kumalizika jumanne ambapo kutakuwa na Full Moon Party, ambapo watu mbali mbali kutoka nchi mbali mbali wanatarajiwa kuonesha uwezo wao katika kupiga muziki.

Rais Hu Jintao ndani ya Tanzania




Chinese President Hu Jintao (3rd R, front) is greeted by Tanzanian President Jakaya Mrisho Kikwete (2nd R, front) upon his arrival at the airport in Dar es Salaam, Tanzania, Feb. 14, 2009. Hu arrived here on Saturday night for a state visit to Tanzania. (Xinhua/Rao Aimin)

Rais wa China Hu Jintao ma mwenjeji wake Rais Kikwete wakipunga mkono mara baada ya kuwasili ikulu Dar es Salaam jana. Picha na Emmanuel Herman.

DAR ES SALAAM, Feb 15 (Reuters) - Chinese President Hu Jintao brought a 150 million yuan ($21.95 million) aid gift to Tanzania on Sunday on the penultimate leg of a tour intended to cement China's ties with Africa despite the global slowdown.
Met by trumpets and dancers on arrival in Dar es Salaam, Hu repaid the hospitality with a 120 million yuan aid package for mainland Tanzania and 30 million for the Zanzibar islands.
"The traditional friendship between China and Tanzania ... can be viewed as an exemplary relationship of sincerity, solidarity and cooperation between China and an African country, and for that matter between two developing countries," Hu said.
The Chinese leader, who has already been to Mali and Senegal, witnessed the signing of the aid deals with Tanzania's President Jakaya Kikwete.
Hu winds up his trip on the Indian Ocean island of Mauritius in a carefully-selected tour of nations that rank outside Africa 's economic and resource heavyweights.
Analysts say it is a deliberate message that Beijing, whose trade with Africa has shot up tenfold this decade to $107 billion last year, wants to engage right across the continent, even with smaller nations and in sectors beyond oil and mining.
By George Obulutsa.

Friday, February 13, 2009

JK amvua cheo DC aliyecharaza viboko walimu Bukoba

Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Rais Jakaya Kikwete amemvua madaraka na kumwachisha kazi rasmi kuanzia jana mkuu wa wilaya ya Bukoba, Albert Mnali aliyeamuru polisi mmoja kuwachapa viboko walimu katika shule tatu za msingi zilizo wilayani kwake kutokana na kushika mkia katika matokeo ya darasa la saba.

Taarifa iliyotolewa na ofisi ya Waziri Mkuu jana ilieleza kuwa Rais Kikwete amechukua hatua hiyo ili iwe fundisho kwa kuwa kitendo alichokifanya Mkuu huyo wa wilaya hakikubaliki, kimedhalilisha, cha kuvunja moyo walimu na kinavunja maadili ya kibinadamu.

Katika uamuzi huo, Rais Kikwete alisema mkuu huyo wa wilaya amedhalilisha wadhifa wa ukuu wa wilaya kwa kuwa alikosea kuchukua hatua hiyo kwa kuwa mwenye mamlaka ya kuwawajibisha walimu ni kamati za nidhamu za mikoa na wilaya na wala si mtu mmoja kama alivyofanya mkuu huyo.

Alisema kuwa amechukua hatua hiyo baada ya kufuatilia maelezo ya pande zote zinazohusika na kuwa serikali imeridhia kiongozi huyo avuliwe wadhifa.

Mauaji: Baada ya Zombe, Bageni amwaga mboga, ajitetea kwa saa sita



MSHITAKIWA wa pili katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini na dereva teksi wa Manzese Dar es Salaam, Mrakibu wa Polisi (SP), Christopher Bageni amezidi kumuweka pabaya mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Abdallah Zombe.


Bageni na wenzake tisa, akiwemo Zombe, wanashitakiwa kwa tuhuma za kuwaua wafanyabiashara watatu wa madini ya rubi kutoka Mahenge mkoani Morogoro- Sabinus Chigumbi, maarufu kama Jongo, Ephrahim Chigumbi, Mathias Lunkombe na dereva wa teksi wa Manzese jijini Dar es salaam, Juma Ndugu.


Bageni alidaiwa na Zombe kuwa ndiye aliyeamuru wafanyabiashara hao kuuawa, lakini jana alimshambulia Zombe kuwa muhusika mkuu. Hadi sasa, mtuhumiwa mmoja katika kesi hiyo, Koplo Saad Alawi, ambaye anadaiwa kufyatua risasi na kuwaua wafanyabiashara hao, hajakamatwa.


Katika utetezi huo uliodumu kwa saa sita, Bageni aliieleza Mahakama Kuu kuwa Zombe alimrubuni kuwa wapeleke taarifa ya uwongo kwenye tume ya Jaji Musa Kipenka, iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete kuchunguza ukweli wa vifo vya wafanyabiashara hao.


Mbele ya Jaji Salum Massatti anayeisikiliza kesi hiyo, Bageni alidai kuwa Zombe alimweleza kuwa walisoma na Jaji Kipenka darasa moja katika Shule ya Sekondari Songea na kwamba ameahidi kuwasaidia katika suala la mauaji hayo.


“Mshitakiwa wa kwanza aliniambia kuwa Jaji Kipenka ni “classmate” wake... walisoma naye darasa moja Songea Boys na kwamba wamewasiliana na amemwambia kuwa tupeleke taarifa iliyorekebishwa ili awasaidie vijana wetu,” alidai Bageni wakati akijibu maswali kutoka kwa wakili wa serikali, Angaza Mwipopo.


Bageni alidai kutokana na ushauri huo wa Zombe waliamua kuibadili taarifa waliyoipeleka kwenye tume hiyo, tofauti na taarifa waliyoiandaa ambayo ilipelekwa katika kitengo cha uhalifu, maarufu kama 99. Taarifa nyingine cheki hapazaidi

Thursday, February 12, 2009

Mtaa wa Congo


Jamani mambo yanakuwa juu ya mambo jiji linazidi kufumuka, linapendeza linajaa watu kila kukicha hapa pichani hebu cheki kila mmoja hapa na lake wapo wanaotoka Congo kwenyewe hadi wale wanaotoka huko Nyakitonto, Kanyamahera, Jimbo, Namagondo na kadhalika.

Mkwara wa pili kwa magazeti ya kuchafuana


AISEE huyu jamaaa hapo juu ni kiboko yaani yeye hukurupuka na kutoa maamuzi tuu kwa upande fulani lakini katika upande mwingine walaaa, ni hivi majuzi gazeti lao la serika lilichemka na wakalisema hakuchukua hatua lakini eti leo ameobuka na kuyataka magazeti matatu ya ‘Taifa Tanzania’, ‘Taifa Letu’ na ‘Sema Usikike’ kujieleza ndani ya siku saba kwa nini yasifungiwe kutokana na kuandika habari zinazodaiwa kuingilia uhuru wa watu binafsi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Waziri wa wizara hiyo alisema magazeti hayo yanatakiwa kujieleza ndani ya siku saba kuanzia jana kutokana na kuchafua watu na kupandikiza chuki baina watu na watu.

DC acharaza walimu viboko

*Ni kwa matokeo mabaya darasa la saba
*Waziri asema katu hawawezi kuvumilia

MKUU wa wilaya ya Bukoba Albert Mnali, amemwamuru askari polisi mmoja kuwapiga viboko walimu katika shule tatu za msingi zilizoko Wilaya ya Bukoba kwa sababu wilaya hiyo imekua ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba.

Tukio hilo lilitokea juzi wakati mkuu huyo wa wilaya Koplo wa polisi aliyeambatana naye kwa kuwalaza chini walimu hao na kumuamuru koplo huyo kuwadhibu viboko viwili makalioni na mikononi.

Walimu waliocharazwa viboko tisa wanatoka shule ya msingi Katerero, 11 wa shule ya msingi Kanazi ambao walichapwa viboko viwiwili kila mmoja na walimu 12 kutoka shule ya msingi Kansenene viboko vinne vinne kila mmoja.

Akizungumza jana waandishi wa habari juu ya tukio hilo mkuu huyo wa Wilaya alisema alilazimika kuwatandika viboko walimu hao baada ya kugunda au kuwepo uzembe kazini, ikiwemo kuchelewa kufika kazini na kutofundisha kama mikataba yao ya ajira inavyosema. Taarifa zaidi punde

Waziri Mkuu leo


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitembelea Chuo Kikuu cha Mtakatifu Yohana kwenye maktaba ya Chuo hicho Mjini Dodoma, jana.(Picha na Ofisi ya Waziri MKuu)

Wednesday, February 11, 2009

Morgan Tsvangirai apishwa Waziri Mkuu Zimbabwe


HARARE, Zimbabwe

KIONGOZI wa chama cha upinzani cha Movement for Democratic Change (MDC) nchini Zimbabwe, Morgan Tsvangirai ameapishwa rasmi kuwa Waziri Mkuu na hivyo kuungana na Rais Robert Mugabe katika serikali ya umoja wa kitaifa.


Tsvangirai aliapishwa rasmi na Rais Mugabe jana, huku watu wachache wakiamini kuwa Tsvangirai ataweza kutekeleza mapendekezo yake mbele ya Mugabe.


Kiongozi huyo wa upinzani kupitia MDC alisema awali kuwa, anatambua kitisho cha kumezwa na chama cha Zanu-PF kama mahasimu wa zamani wa Mugabe, bila ya kubadilisha mkondo unaofuatwa na taifa linalosambaratika, kwani Tsvangirai si kiongozi wa serikali mpya ya mpito.


Pamoja na Tsvangirai manaibu waziri mkuu wawili pia waliapishwa, ambao ni Thokozani Khupe ambaye ni msaidizi wa Tsvangirai kwenye chama cha MDC na Arthur Mutambara ambaye ni kiongozi wa kundi lililojitenga kutoka MDC.


Jumanne wiki hii Tsvangirai alimteua Katibu Mkuu wa chama chake, Tendai Biti kushika wadhifa wa Waziri wa Fedha, baada ya Jaji wa Mahakama Kuu ya nchi hiyo kufuta mashtaka ya uhaini dhidi yake wiki iliyopita.


Kufuatia kuapishwa kwake, Tsvangirai ana haki ya kutoa mapendekezo na wakati mwingine kumwakilisha Mugabe anayebakia kuwa rais, licha ya kushindwa uchaguzi uliofanywa mwezi wa Machi mwaka jana.


Mugabe anaendelea kuwa kiongozi wa serikali na vile vile mkuu wa Tsvangirai, hatua hiyo inaonekana kuwatia wasiwasi Wazimbabwe wengi, ambapo mmoja wao ambaye ni mwanaharakati wa haki za binadamu, Tsitsi Torongo mwenye miaka 29 alisema:


"Mimi binafsi kamwe sijawahi kukiamini chama cha Zanu-PF. Hofu yangu ni kuwa wataendelea kuizuia serikali hiyo kufanya kazi yake na hivyo kuzuia masuala muhimu kushughulikiwa kama ipasavyo."

Zombe: DPP alinifanyia mchezo mchafu

MSHITAKIWA wa kwanza katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wanne wa madini na dereva teksi wa Manzese Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Abdallah Zombe ameieleza Mahakama Kuu kuwa kilichomfanya akamwaga machozi kizimbani jana ni mchezo mchafu alifanyiwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Zombe ambaye alikuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam alijikuta akimwaga machozi mara kadhaa juzi wakati akijitetea mbele ya Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Salum Masatti kuhusiana na tuhuma hizo zinazomkabili yeye pamoja na askari wenzake tisa.

Akijibu maswali kutoka kwa Waendesha Mashtaka(PP) jana kuhusiana na ushahidi wake wa utetezi alioutoa mahakamani hapo juzi, Zombe aliiambia mahakama kuwa maelezo yaliyoandikwa na baadhi ya washtakiwa wakiwa mahabusu, ambayo ndio DDP aliyatumia kama ushahidi wa kumuunganisha katika kesi hiyo yaliandaliwa na DPP mwenyewe na kuwapa washitakiwa hao.

Zomba alisema kutokana na maelezo hayo kupangwa yalitolewa gerezani hapo kwenda kwa DPP kwa njia za panya bila kupitia kwa Mkuu wa Gereza la Ukonga wanaohifadhiwa, kama utaratibu ulivyo.

Alidai kuwa barua za maelezo ya washitakiwa hao zote ambazo nakala zake alizitoa juzi mahakamani hapo kama vielelezo kwa ajili ya ushahidi wake yaliandikwa Juni 3 mwaka 2006 mchana ingawa baadhi hazina tarehe.

Tuesday, February 10, 2009

Zombe amwaga chozi mahakamani

Ajitetea saa tatu

MSHTAKIWA wa kwanza katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini kutoka mjini Mahenge, Morogoro na dereva teksi wa Manzese jijini Dar es Salaam inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Abdallah Zombe jana alijikuta akimwaga machozi kizimbani wakati akiwasilisha utetezi wake.

Zombe alijikuta akimwaga machozi mara kadhaa wakati akijitetea mbele ya Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Salum Masatti kuhusiana na tuhuma hizo zinazomkabili yeye pamoja na askari wenzake tisa.

Hatua ya Zombe kupanda kizimbani jana na kuanza kujitetea ilikuja baada ya mahakama hiyo kuridhika kuwa yeye na wenzake wana kesi ya kujibu dhidi ya mauaji ya wafanyabiashara hao kulingana na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo hoja za mawakili wa watuhumiwa hao na majibu ya hoja hizo kutoka kwa upande wa mashitaka. Kwa taarifa zaidi bonyeza hapa

Wengi wamiminika kushuhudia kesi ya Sendeka



MAMIA ya watu wengi wao wakiwa ni wamasai toka Simanjiro jana walimiminika katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Arusha kufuatilia kesi ya inayomkabili mbunge wa jimbo la Simanjiro mkoa wa Manyara, Christopher Ole Sendeka aliyepandishwa tena kizimbani kujibu shitaka la kumshambulia Mwenyekiti wa jumuiya ya vijana ya CCM mkoa wa Arusha, James Ole Millya.

Kesi hiyo ya jinai namba 3/2009 ambayo ilihudhuriwa na mamia ya watu wengi wao wakiwa ni wamasai toka Simanjiro, ilitajwa mbele ya Hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa Arusha, James Karayemaha kwa mara ya pili.

Sendeka anatuhumiwa kumchambulia Millya, Januari tisa wilayani Monduli mkoani Arusha, ambapo wote walikuwa wakihudhuria semina ya wazee wa mila ya kimasai na viongozi toka jamii ya kimasai, mkutano uliandaliwa na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Katika kesi hiyo jana kwa mara ya kwanza, Mawakili wawili Kelvin Kwagirwa toka kampuni ya uwakili ya Oljale na Moses Mahuma toka kampuni ya uwakili na Dancon Oola, walijitambulisha kumwakilisha Mlalamikaji James Millya.

Mawakili hao, waliomba kufuatilia kesi hiyo kwa kuwa mshitakiwa anawakilishwa na jamhuri katika shauri hilo.

Zombe ana kesi ya kujibu


WATATU WAACHIWA HURU
ZOMBEA ATOA SOMO LA SHERIA

HATIMAYE Mahakama Kuu imetegua kitendawili cha hatima ya aliyekuwa mkuu wa upelelezi mkoani Dar es Salaam, Abdallah Zombe na wenzake 12 baada ya kuamua kuwa wana kesi ya kujibu katika tuhuma zinazowakabili za mauaji ya wafanyabiashara watatu na dereva wa taksi mmoja, huku ikiwaachia watuhumiwa watatu.

Mahakama imeridhika kuwa washtakiwa hao watatu katika kesi hiyo namba 26 ya mwaka 2006 hawana kesi ya kujibu.

Zombe na wenzake wanashtakiwa kwa tuhuma za kufanya makosa manne ya mauaji ya kukusudia ya wafanyabiashara watatu wa madini kutoka mjini Mahenge, Morogoro- Sabinus Chigumbi, maarufu kama Jongo, Ephrahim Chigumbi, Mathias Lunkombe na dereva teksi wa Manzese jijini Dar es salaam, Juma Ndugu.

Jaji wa Mahakama Kuu, Salum Masatti alisema mahakama hiyo imeridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo kuwa Zombe, ambaye ni mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo na wenzake tisa wana kesi ya kujibu kuhusiana na vifo vya wafanyabiashara hao.

Washtakiwa wengine walioonekana wana kesi ya kujibu ni mshitakiwa wa pili ambaye ni Mrakibu wa Polisi (SP), Christopher Bageni, mshitakiwa wa tatu ambaye Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Ahmed Makelle na wa tano WP 4593 PC Jane Andrew.

Wengine ni mshitakiwa wa saba CPL Emmanuel Mabula, mshitakiwa namba tisa D.8289 PC Michael Sonza, mshitakiwa wa 10 D 2300CPL Ebeneth Saro, wa 11, D.9312D/C Rashid Lema, D4656 C/CPL Rajab Bakari na D.1367 D/CPL Festus Gwabisabi.

Jamani waliosoma Milambo huu wimbo mwaukumbuka

Hapa utamkuta Headmaster wetu wakati huo Bw. Anthony Msemakweli enzi hizo tukimwita jina la Fupa, kulia kwake yupo Second Master Mwalimu Kyala ilikuwa matata, lazima kwanza uwe suruali umepiga pasi, nguo safi na hawakuruhusu watu kujongo na huu wimbo uliimbwa mara baada ya watu kupata sifongo au uji wakati huo.

Milambo shule yangu naipenda,

Chorus:Milambo shule yangu naipenda,

Ina michepuo

Chorus: Yenye sifa tele,

Hasa wa lugha,

Chorus: Kingereza, Kiswahili, Kifaransa,

Biashara

Chorus:Na Masomo ya jamii na michezo,

Na Kilimo

Mashambani bustani, ufugaji

Motto wetu siku zote

Chorus: Elimu ni amana, pia ni ufunguo,
huleta ufanisi,
Elimika,

Chorus: aaaa Jenga taifa,

Friday, February 06, 2009

Eti chumbani kwa Dk Slaa kumekutwa vinasa sauti


Taarifa ambazo ambazo haziridhishi kabisa kuamini zimetufikia jana usiku kutokea Dodoma ambapo pia iliitishwa Press Conference usiku huo huo Slaa mwenyewe akidai kuwa aliwekewa vifaa vivyo vya kurekodi sauti. Mambo mawili ambayo naungana na ndugu yangu Maro inasikitisha kwamba tumeingia kwa mkumbo kwa mawazo ya kulia tu ni haya.

1.Kwanini tunashikilia Dk Slaa ndiyo amewekewa vifaa hivyo na watu ambao hawatuwafahamu ili khali inawezekana kabisa Dk Slaaa na CHADEMA wakawa wameweka vifaa hivi kama kujitafutia Umaarufu. Hilo Linawezekana na ni moja ya mbinu za kisiasa ili watu waendelee kuamini kuwa unaweza kuleta Mabadiliko. Tusubiri uchunguzi na iiwezekana Mzee Mwanakijiji na Bongo Radio any mahojiano na wale wahudumu wa ile Hotel.

2.Kuanza kuhisi kuwa ni Masha ndiyo kafanya jmbo hili,ama waziri kijana.Huu ni upotoishaji tena kwa hoja kwamba Masha alilipuliwa na Dr. Slaa. Kama tumefika katika siasa za chuki kama alivyosema Mzee Mkapa basi 2010 uchaguzi utakuwa ni wa aina ya ajbu kutokea katika Nchi hii.

2009/2/6 Josephat Isango
Watanzania ambao kwa muda huu mmelala fofofo, muda huu ni Saa saba Usiku, Dodoma hali sio nzuri usiku wa leo, Dr, wilbrod Slaa na Tarab Ally wamewekewa vitu vinavyosadikiwa kuwa ni vifaa vya kuwarekodi kwenye vyumba vyao vya kulala, kwenye sehemu za uvungu wa vitanda. hatujajua lengo la watu hao kuweka vifaa hivyo, ila ninachoweza kusema ni wabunge ambao wamekuwa na changamoto Bungeni, huenda kuna njama za Wabunge hao kuhujumiwa. Nchi yetu sijui inaenda wapi tuiombee.

Thursday, February 05, 2009

Republicans wamchagua mwenyekiti mweusi


Naibu Gavana wa Maryland, Michael Steele, amechaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa Chama cha taifa cha Republicans (Republican National Committee). Ni mwuesi wa kwanza katika historia ya chama hicho kuongoza chama.
Kama mnakumbuka walivyofanya mkutano mkuu wao mwezi Agosti, weusi walikuwa wachache mno huko, uliweza kuwahesabu kwenye mkono. Na weusi wengine waliokuwepo walidai kuwa walitukanwa matusi ya kibaguzi. Kipindi hicho vyombo vya habari vilihoji uhaba wa weusi katika chama cha Repbulicans na kuuliza kama Republicans ni chama cha wazungu tu.
Huenda Republicans wanadhania kuwa wakiwa na Mwenyekiti mweusi basi labda weusi watavutiwa kujiunga na chama hicho.
Lazima kuna watu hapa ambao hawana raha kutokana na kuchaguliwa kwake. Wazungu walikuwa na usemi, "A Black Man will be President when Hell Freezes Over" yaani mtu mweusi atakuwa rais kipindi motoni kunageuka barafu tupu. Basi huo barafu umeingia motoni. Obama ni rais na Steele ni mwenyekiti wa Republicans.
Lazima wabaguzi wa KKK wanalia.

Hatima ya Zombe J'3




AKIJIBU AU ASIPOJIBU ATAKUTWA NA HATIA
HATIMA ya Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Abdallah Zombe katika kesi ya mauaji ya kukusudia inayomkabili pamoja na askari wenzake 12, itajulikana Jumatatu ijayo.

Zombe, aliyekuwa mkuu wa upelelezi mkoani Dar es Salaam, RCO, na kaimu kamanda wa polisi, ARPC, wakati wa mauaji hayo ya wafanyabiashara wanne wa mjini Mahenge mkoani Morogoro na dereva mmoja wa teksi wa Manzese jijini Dar es salaam, ndiye mtuhumiwa namba moja kwenye kesi hiyo inayosikilizwa Mahakama Kuu.

Wanasheria wamekuwa wakiwasilisha hoja zao kama Zombe na wenzake, wana kesi ya kujibu katika hatua za awali za kesi hiyo inayovuta hisia za wengi, na baada ya mawakili wa watuhumiwa kuiambia mahakama kuwa wateja wao hawana kesi ya kujibu na hoja hizo kujibiwa jana na mawakili wa upande wa mashtaka, hukumu ya suala hilo sasa itatolewa Februari 9.

Akiahirisha kesi hiyo jana baada ya upande wa mashtaka kumaliza kujibu hoja za upande wa utetezi, jaji wa Mahakama ya Rufaa, Salum Massati alisema kuwa uamuzi huo utatolewa Jumatatu saa 4:00 asubuhi.

Rais huko Dodoma


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dodoma leo wakati Rais alipokwenda chuoni hapo kukagua ujenzi unaoendelea.(picha na Freddy Maro)

Wednesday, February 04, 2009

Nora bwana na mambo yake




KAMPUNI ya Beknet Tanzania Limited imeandaa uzinduzi wa albamu ya Upande wa Pili wa Ndoa isiyo ya Uaminifu katika Ukumbi wa Cinema wa Century Cinemax Mlimani City Februari 6.

Akizungumza na Mwananchi jijini jana, mkurugenzi wa filamu hiyo, Bariki Keenja alisema anatarajia uzinduzi wake utafana kwani katika filamu yake kuna mengi ya kufurahisha.

Alisema katika filamu hiyo, imezungumzia maisha halisi ambayo yapo katika jamii ya sasa ambapo mwanamke au mwanaume kumsaliti mwenzi wake kwa namna moja au nyingine na hii hutokana na tamaa zisizo na msingi.

Filamu hiyo imewashirikisha wasanii mbalimbali akiwemo Nuru Nasoro ''Nora'', Elizabeth Chijumba ''Nikita'', Ahmed Olotu anayetambulika kwa jina la kisanii, Mzee Chilo na Subira Maulid.

Pichani kulia Nora akisikiliza swali kwa makini kutoka kwa mmoja wa waandishi wa habari alipomuuliza kuhusiana na habari za kashfa ambazo zimekuwa zikimuandama muigizaji huyo juu ya mapenzi na wanaume tofauti tofauti

Mawakili wasema Zombe hana cha kujibu



MAWAKILI wa washitakiwa wa kesi ya mauaji ya kukusudia ya wafanyabiashara watatu wa madini na dereva teksi wa Manzese Dar es Salaam, jana waliisihi mahakama kuu kuwaachia huru washtakiwa wao kwa madai katika ushahidi uliotolewa unaonyesha hawana kesi ya kujibu.

Wakitoa hoja zao za kuishawishi mahakama kuamini kuwa washtakiwa hao hawana kesi ya kujibu, mawakili hao kwa nyakati tofauti waliieleza mahakama hiyo kuwa ushahidi uliotolewa mahakamani hapo hauwahusishi na tuhuma za mauaji hayo moja kwa moja na badala yake ni ushahidi wa mazingira tu.

Mawakili hao pia waliuchambua ushahidi uliotolewa dhidi ya wateja wao na kuieleza mahakama kuwa unajichanganya kwa maelezo kuwa mashahidi hao wamekuwa wakipingana katika maelezo yao, jambo ambalo mawakili hao walisema linaacha utata kwa mahakama kujua ushahidi upi ni wa kweli na upi si wa kweli.

Mawakili wa washtakiwa wote waliieleza mahakama kuwa kati ya watu 37 waliotoa ushahidi mahakamani hapo, hakuna shahidi hata mmoja aliyeweza kuithibitishia mahakama hiyo jinsi washtakiwa hao walivyotenda kosa la mauaji hayo.

Walisema ushahidi wote uliotolewa ni wa kusikia tu na si wa kushuhudia kosa likitendeka. na James Magai

kipanya leo

Tuesday, February 03, 2009

Katibu Mkuu UN kutembelea Tanzania

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-Moon atatembelea Tanzania baadaye mwezi huu, imethibitishwa mjini Addis Ababa, Ethiopia.

Ban Ki-Moon amethibtisha mwenyewe kuhusu ziara hiyo ya siku mbili, kuanzia Februari 25, mwaka huu.

Katibu Mkuu huyo alitangaza ziara hiyo wakati alipokutana na kuzungumza na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, katika Kituo cha Mikutano cha UNCC-ECA mjini Addis Ababa.

Viongozi hao wawili wako mjini Addis Ababa, Ethiopia, kuhudhuria mkutano wa 12 wa kawaida wa viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU).

Ban Ki-Moon alisema atazuru Tanzania baada ya kumaliza ziara yake nchini Afrika Kusini.

Hii itakuwa ziara ya kwanza kwa Katibu mkuu huyo wa UN, kutembelea Tanzania.

Katika mazungumzo hayo, Ki-Moon, alimsifia Naibu Katibu Mkuu wa UN, Dk Asha Rose Migiro wa Tanzania, kwa kuwa mwanamke mchapa kazi.

Mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika




KIONGOZI wa Libya, Muammar Gaddafi, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) akichukua nafasi iliyokuwa ikishikiliwa kwa mwaka mzima na Rais Jakaya Kikwete.

Gaddafi, mmoja wa viongozi wakongwe Afrika, akiwa amekaa madarakani kwa takriban miaka 40 tangu alipoingia madarakani kwa mapinduzi yasiyo ya kumwaga damu mwaka 1969, akiwa na miaka 27 tu, alichaguliwa kushika wadhifa huo wa juu AU na viongozi wakuu wa nchi 53, katika mkutano wa 12 wa umoja huo unaofanyika nchini Ethiopia.

Mwandishi wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Elizabeth Blunt, aliyeko kwenye mkutano huo, alikuelezea kuchaguliwa kwa kiongozi huyo msoshalisti, kuwa tukio lililowagawa viongozi wa AU katika makundi mawili, moja ya kundi likimuunga mkono, wakati jingine likionyesha kutoridhishwa na kuchaguliwa kwake.

Kanali Gaddafi anaingia madarakani kwa kipindi cha mwaka mmoja, akiwa mmoja wa viongozi ambao katika miaka ya hivi karibuni wamekuwa mstari wa mbele kupigania muungano wa nchi za Afrika, wenye lengo la kuunda serikali moja, akiita ‘United States of Africa’, yenye sarafu moja na jeshi moja.

Vyombo vya habari vya nchi za Ulaya Magharibi, vinamtaja Gaddafi kuwa mmoja wa viongozi wajanja na wepesi wa kubadili mwelekeo kwa nia ya kujenga mahusiano mema ya kidiplomasia, kwa kuzingatia matakwa ya wakati.

Kiongozi huyo anakumbukwa kwa namna alivyotokea kuwa mmoja wa maadui wa nchi za Magharibi na Marekani hadi mwaka 2003, wakati alipoamua kusitisha mpango wake wa kuendelea kutengeneza silaha za sumu, hatua ambayo ilisababisha jumuiya ya kimataifa kurejesha uhusiano wa kidiplomasia na Libya.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa AU, Habiba Mejri-Sheikh, jana, ilieleza kwamba, kiongozi huyo wa Libya ambaye uongozi wake umekabiliana na matatizo mbalimbali ya kidiplomasia ambayo wakati fulani yalisababisha taifa lake litengwe kimataifa kabla ya mambo kubadilika, aliwahutubia wakuu wa AU kueleza mwelekeo wa uongozi wake katika kipindi cha mwaka mmoja ujao.

“Sasa hivi (jana jioni) anahutubia mkutano kama mwenyekiti kuelezea programu na matarajio yake,” alisema msemaji huyo wa AU.

Monday, February 02, 2009

GTV yafilisika



GTV imesitisha huduma zake Tanzania na sehemu nyingine duniani kwa kile kilichoelezwa kuwa kukumbwa na mgogoro wa fedha hivyo kampuni hiyo kushindwa kutoa huduma zake.

Tatizo la maji siyo kwetu tu hebu cheki huku


Residents of Nyangu village, Kinango District at the coast are having it rough. First, a long and dry spell has meant that the village’s only dam has dried up, forcing them to dig holes to harvest the little water that seeps out. Second, roaming pastoralists also want a share of this water. As a result, fights have become a common feature as the two groups scramble for the scarce commodity. In these pictures, Ms Rose Zambia (in a striped dress) struggles to ward off several Masaai morans and women who wanted to ‘hijack’ her hole and help themselves to her water. Photos Maarufu Mohamed/Standard

Sunday, February 01, 2009

hebu cheki kitu kipya

Rais Kikwete yuko Ethiopia



Tanzania 's President and chairman of the African Union Jakaya Mrisho Kikwete (L) arrives for the 12th African Union Summit of Heads of States at the United Nations office in Addis Ababa February 1, 2009. REUTERS/ Antony Njuguna (ETHIOPIA)

Watu 100 wateketea kwa moto Kenya






ZAIDI ya watu 100 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 200 kujeruhiwa baada ya lori la mafuta ya petroli kupinduka na kulipuka katika mji wa Molo kwenye mkoa wa Rift Valley nchini Kenya.
Taarifa kufikia jana jioni zilieleza kuwa vifo vinavyotokana na tukio hilo vilifikia 111, likiwa ni tukio la pili la moto kubwa kwa wiki hii, baada ya kuungua duka la kujihudumia vyakula na bidhaa (Supermarket) la Nakumat Downtown, Jumatano wiki iliyopita.
Katika tukio hilo la awali, zaidi ya watu 50 walipotea wakiwa hawajulikani waliko, lakini siku mbili baadaye miili ya watu 27 ikiwa imepatikana katika mabaki ya jengo la duka hilo huku juhudi za kutafuta miili zaidi zikiendelea, mingi kati ya iliyopatikana ikiwa imeteketea kiasi cha kutotambulika.
Taarifa za awali zilizotolewa jana zilieleza kuwa lori hilo la mafuta lilipoteza mwelekeo na kuacha barabara karibu na mji wa Molo ambapo mamia ya watu walijitokeza na kulizunguka lori kwa lengo la kuchota mafuta yaliyokuwa yakimwagika.
Waathirika wa ajali hiyo walikuwa wamelazwa kwenye sakafu ya hiospitali, huku wakiwa wamewekewa chupa za maji.
Ajali hiyo inadhaniwa kuwa ilitokana na mmoja wao wananchi hao wanadaiwa kuwa walikuwa wanaiba mafuta, kuwasha sigara katika eneo hilo.