Tuesday, September 30, 2008

Pinda ziarani Ghana


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua gwaride baada ya kuwasili kwenye uwanja wa
ndege wa Kotoko International Airport uliopo Accra, Ghana September 30, 2008
ambaco amemwakilisha Rais JakayaKikwete katika Mkutano wa 6 wa Wakuu wa Nchi za
Jumuiya ya Africa , Caribbean na Pasifiki. Kushoto ni Waziri wa Nchi wa Ghana,
S.K. Boaf (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Friday, September 26, 2008

Mtikila na siasa zake za maji taka

Mchungaji Christopher Mtikila akiwa hospitalini baada ya kutibiwa jeraha na mwenyekiti wa chama hjichowilayani Tarime Christian Nyakihita akionyesha jiwe na shati la mtikila ambalolilikuwa limelowa damu.(Picha na Frederick Katulanda)

Thursday, September 25, 2008

Mambo NMB sasa mswano




WAFANYAKAZI wa Benki ya NMB jana walirejea kazini na kuendelea kutoa huduma baada ya kubatilishwa kwa mgomo ulioanza Jumatatu wiki hii, huku kukiwa na kasoro kadhaa katika huduma ambazo zililalamikiwa na wateja wa benki hiyo.Katika tawi la Bank House kulikuwa na msururu mrefu wa wateja walio kuwa wamejipanga kwenye mstari wakisubiri kupatiwa huduma ambayo ilisitishwa tangu Jumatatu, huku mashine za kutolea fedha 'ATM' zikiwa hazifanyi kazi.Kwa mujibu wa wateja waliokuwapo maeneo hayo, mashine hizo zilikuwa hazifanyi kazi tangu walipofika asubuhi na kwamba, walipowasiliana na uongozi waliwaambia hawajui tatizo litatatuliwa saa ngapi.Lakini ilipofika saa 4:00 asubuhi baadhi ya ATM za makao makuu ya benki hiyo, zilianza kufanya kazi kwa kusuasua na baada ya muda zilirejea katika hali yake ya kawaida na watu wakaanza kuchukua fedha.Habari Kwa Hisani Ya Mzee Wa Sumo

Wednesday, September 24, 2008

South african heritage day exhibition


SOUTH AFRICAN HERITAGE DAY EXHIBITION
EXHIBITION & SALE OF ART WORKS FROM SOUTH AFRICA & TANZANIA
ALLIANCE FRANÇAISE
24 SEPT - 3 OCT
9 AM - 7 PM
ALLIANCE FRANÇAISE
Your French Language and Cultural Centre in Dar es Salaam
French courses, Resource centre, Films, Exhibitions, Concerts, Shows.
Ali Hassan Mwinyi Road (car park behind Las Vegas Casino)
Office opening hours: Mon-Fri: 9am-1pm / 2pm-6pm & Sat: 10am-1pm


Raila ndani ya nyumba


Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga akipita mbele ya gwaride maalum lililoandaliwa kwa ajili yake alipowasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwl. JK Nyerere Dar es Salaam jana. Kulia kwa Odinga ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke Abdalah Kihato.




Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mgeni Wake Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odingawakiwa katika picha ya pamoja na na wajumbe wa nchi mbili hizo baada ya mazungumzoyao kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es salaam September24, 2008. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Monday, September 22, 2008

hebu nambieni jamani nini kinapikwa

Jamani hivi vyungu vinapika nini na tena katika eneo la mficho kama hili nambieni jamani , au ni kinywaji au sijui ni chakula??

Safari ni safari




Hebu nambieni hii safari ya kinamna gani, mdau

Abdul Njaidi ameinasa picha hii akiwa safarini kuelekea Chalinze, nyumba imebbwa juu ya gari ni mambo ya mjini hayo.

Please come in and have something to eat

A woman came out of her house and saw 3 old men with long white beards sitting in her front yard. She did not recognize them.

She said 'I don't think I know you, but you must be hungry. Please come in and have something to eat.'

'Is the man of the house home?', they asked.

'No', she replied. 'He's out.'

'Then we cannot come in', they replied.
In the evening when her husband came home, she told him what had happened.
'Go tell them I am home and invite them in!'
The woman went out and invited the men in'

'We do not go into a House together,’ they replied.

'Why is that?' she asked.

One of the old men explained: 'His name is Wealth,' he said pointing to one of his friends, and said pointing to another one, 'He is Success, and I am Love.' Then he added, 'Now go in and discuss with your husband which one of us you want in your home.'

The woman went in and told her husband what was said.. Her husband was overjoyed. 'How n ice!!', he said. 'Since that is the case, let us invite Wealth. Let him come and fill our home with wealth!'

His wife disagreed. 'My dear, why don’t we invite Success?'

Their daughter was listening from the other corner of the house. She jumped in with her own suggestion: 'Would it not be better to invite Love? Our home will then be filled with love!'

'Let us heed our daughter's advice,’ said the husband to his wife.
'Go out and invite Love to be our guest.'
The woman went out and asked the 3 old men, ‘Which one of you is Love? Please come in and be our guest.'

Love got up and started walking toward the house.
The other 2 also got up and followed him. Surprised, t he lady asked Wealth and Success: 'I only invited Love, Why are you coming in?'

The old men replied together: 'If you had invited Wealth or Success, the other two of us would've stayed out, but since you invited Love, wherever He goes, we go with him. Wherever there is Love, there is also Wealth and Success!!!!!!'

MY WISH FOR YOU...
-Where there is pain, I wish you peace and mercy.
-Where there is self-doubting, I wish you a renewed confidence in your ability to work through it.
-Where there is tiredness, or exhaustion, I wish you understanding, patience, and renewed strength.
-Where there is fear, I wish you love, and courage.


Sunday, September 21, 2008

Bomoa bomoa ya kikatili Magomeni







FAMILIA sita zimekosa sehemu ya kuisha baada ya watu wanaodai kununua nyumba ya urithi ya watoto zaidi ya 10 wa marehemu Yussuf Mbonde iliyo Magomeni Mwembechai kubomoa nyumba hiyo kwa kutumia greda huku wakilindwa na vijana wa kukodi maarufu kama mabaunsa pamoja na usimamizi wa polisi waliokuwa na silaha.

Bomoabomoa hiyo ilitokea jana majira saa 9:00 alasiri baada ya uvamizi huo kutokea na kusambaratisha nyumba na vitu vyote vilivyokuwemo ndani.

Mwananchi ilifika eneo hilo mara baada ya tukio hilo na kuwakuta wanafamilia hao wakilia kwa uchungu huku wakilalamikia kitendo hicho ambacho wamekiita ni cha ukatili. habari zaidi soma Mwananchi.Habari yote hii imendikwa na Salim Said ambaye pia kapiga picha zote.

watoto shuleni



Watoto wa Shule ya Sekondari Mbezi Msigani wakifanya mambo ndani ya shule yao wakati wa hafla ya kuwaaga wenzao wanaotarajiwa kuanza nitihani ya kuhitimu kidato cha nne mwaka huu. Picha na MIchael Matemanga.

safisha safisha BoT





Baadhi ya wafanyakazi 8 wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) waliofikishwa Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kistu jijini Dar es Salaam jana kujibu tuhuma za kughushi vyeti wakijifunika nyuso zao kuwakwepa paparazi Septemba 20 wakati wakienda kupanda karandinga tayari kwa safari ya Mahabusu hadi Oktoba 6 shitaka lao litakapo anza kusikilizwa.
Wafanyakazi hao, ni Justina J Mungai, ambaye imeelezwa kuwa ni mtoto wa Joseph Mungai, ambaye amewahi kushika wizara tofauti ikiwemo ya elimu, Christina G Ntemi, Siamini Eddie Kombakono, Janeth John Mahenge, Beatha Constantine Massawe, Jacquiline David Juma, Philimina Philibert Mutagurwa na Amina Mohamed Mwinchumu.


TUHUMA za kuwepo kwa upendeleo wa watoto wa vigogo kwenye ajira za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zimesimamisha kizimbani wafanyakazi wanane ambao wameshtakiwa kwa kosa la kughushi vyeti.
Tuhuma dhidi ya watoto 16 wa vigogo ziliibuka wakati kashfa ya wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), ikiwa imeshamiri kiasi cha kusababisha aliyekuwa gavana, Daud Ballali kusitishwa mkataba wake na kufanyika kwa mabadiliko kadhaa kwenye uongozi wa chombo hicho nyeti cha fedha.
Na Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, aliahidi kuzishughulikia tuhuma hizo wakati huo baada ya tuhuma hizo kushikiwa bango.
Jana, wafanyakazi wanane wa BoT, baadhi yao wakiwa wamejifunika nyuso kwa nguo na nywele za bandia, walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakishtakiwa kwa tuhuma za kughushi vyeti na kutoa hati za uongo.
Wafanyakazi hao, wengi wao wakiwa wanawake, ni Justina J Mungai, ambaye imeelezwa kuwa ni mtoto wa Joseph Mungai, ambaye amewahi kushika wizara tofauti ikiwemo ya elimu, Christina G Ntemi, Siamini Eddie Kombakono, Janeth John Mahenge, Beatha Constantine Massawe, Jacquiline David Juma, Philimina Philibert Mutagurwa na Amina Mohamed Mwinchumu.
Wafanyakazi hao walifikishwa katika mahakama hiyo saa 4.00 asubuhi na kusomewa shtaka mbele ya Hakimu Neema Chusi. Wakili wa serikali, Edgar Luoga, akisaidiana na Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Abubakar Msangi, ndio walioongoza mashtaka hayo.
Washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa hati za uongo kwa mwajiri wao, ambaye ni BoT.
Washtakiwa Mungai, Massawe na Mwinchumu, wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2001, wakati Ntemi, Kombakono, Mahenge na Mutagurwa wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2002. Wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa BoT hati za uongo, wakionyesha kuwa vimetolewa na Baraza la Mitihani la Taifa, wakati si kweli.
Ilidaiwa kuwa, Mutagurwa alighushi cheti hicho mwaka 2000.

Saturday, September 20, 2008

Rais kwenda Marekani

RAIS Jakaya Mrisho Kikwete anaondoka nchini leo (Jumamosi, Septemba 20, 2008) kwenda New York, Marekani, ambako atahudhuria na kuhutubia kikao cha mwaka huu cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN).

Rais amepangiwa kuhutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Jumanne ijayo, Septemba 23, 2008 katika nafasi yake pia kama Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU).

Mbali na kuhutubia Baraza Kuu, Rais Kikwete amepangiwa kuhudhuria mikutano mingine muhimu kuanzia ule ambao utaangalia Mahitaji ya Maendeleo ya Afrika. Mkutano huo, utajadili ahadi za nchi tajiri kwa Afrika na Maendeleo ya Bara hilo, na kuona ahadi hizo zinatekelezwa namna gani.

Rais pia atahutubia kikao cha ufunguzi cha viongozi ambao watajadili maendeleo ya Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDG’s). Baada ya kuwa amehutubia kikao hicho, Rais atashiriki katika mijadala kuhusu afya ya Mama na Mtoto, na pia mjadala kuhusu ugonjwa wa Malaria, masuala yote mawili yakiwa sehemu muhimu ya MDG’s.

Ijumaa, Septemba 26, Rais atakwenda mjini Washington, ambako atatoa hotuba muhimu ya ufunguzi kwenye Kikao cha Mwaka cha Wabunge Wenye Asili ya Afrika katika Bunge la Marekani, na pia kuhutubia mkutano wa viongozi wa shughuli za biashara katika Marekani.

Mbali na mikutano ambayo amepangiwa kuhutubia ama kushiriki, Rais Kikwete atakutana na kufanya mazungumzo na viongozi wengi wa shughuli za kisiasa, kibiashara na kiuchumi duniani na katika Marekani.

Miongoni mwa viongozi ambao Rais Kikwete atakutana nao na kufanya mazungumzo nao ni pamoja na Rais wa Iran, Mheshimiwa Ahmedinajad; Katibu Mkuu wa Baraza la Umoja wa Ulaya, Mheshimiwa Javier Solana; na mfanyabiashara maarufu duniani wa shughuli za kompyuta na teknolojia ya mawasiliano, Bill Gates.

Rais Kikwete pia atakutana na Waziri Mkuu wa Denmark, Mheshimiwa Anders Fogh Rasmussen; na Katibu Mkuu wa Shirika la Kazi Dunia (ILO), Juan Somavia.

Rais Kikwete pia atafanya kikao cha pamoja kati yake, Katibu Mkuu wa UN, Ban Ki Moon na Makamu wa Rais wa Sudan, Ustaz. Ali Osman kuzungumzia mgogoro wa eneo la Darfur nchini Sudan.

Wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku mbili katika Sudan mwanzoni mwa mwezi huu, Mwenyekiti huyo wa AU, alimwahidi Rais Omar El Bashir wa Sudan kuwa angefanya kikao kati yake, Katibu Mkuu wa UN, na mwakilishi wa Sudan kuhusu hali ya Darfur wakati wa Kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka huu.

Kikao hicho kitaangalia jinsi gani ya kuharakisha zoezi la kupeleka askari wa kulinda amani wa UN na AU katika Darfur, na pia jinsi ya kuahirisha, kwa angalau mwaka mmoja, hati ya kukamatwa kwa Rais Bashir iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Uharifu (ICC).

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.



20 Septemba, 2008

Friday, September 19, 2008

usingizi nomaaa


Mlinzi akiuchapa usingizi katika lindo mjini Dodoma bila ya kujua kuwa anahatarisha
usalama wake na wa mali anayolinda kwa kutolinda vyema silaha yake.Picha na Jube
Tranquilino

kuni


Mkazi wa Manispaa ya Morogoro eneo la Kihonda Mbuyuni akiwa amebeba makuti ambayo anatumia kama kuni ili kuweza kutumia kupikia chakula, kutokana na nishati ya mkaa kupanda bei kutoka sh 15000 hadi kufikia kiasi cha sh 20000
baadhi ya wananchi wa kipato cha chini wanashindwa kumudu ghalama hizo.(Picha na Juma Ahmadi, Morogoro),

Thursday, September 18, 2008

Musendo: Jela imethiri maisha yangu



Ilikuwa siku, wiki mwezi na miezi na hatimaye miaka mitatu na miezi kadhaa ilikwisha, Zephania Msendo alijikuta kuwa mtu huru tena juzi baada ya kumaliza adhabu yake ya kutumikia kifungo cha miaka mitatu.

Aliachiwa huru kutoka gereza la Mkuza lililo Kibaha mkoani Pwani.

Musendo ni mwandishi mwandamizi ambaye amepitia vyombo mbalimbali vya habari, mara ya mwisho akiwa analiongoza gazeti la Family Mirror akiwa mhariri mkuu.

Lakini bidii yake ya kazi na ujuzi aliokuwa nao ulizimwa ghafla baada ya Hakimu wa Mahakama ya Kisutu kumhukumu kifungo cha miaka mitatu jela kwa madai ya kula rushwa ya Sh 100,000 baada ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCB) kumshtaki.

“Imeathiri sana maisha yangu, imeharibu familia yangu na nimepata hasara kwani kipato kimesimama kwa muda wote na mipango yangu imeparanganyika,” anasema Musendo katika mahojiano maalum na gazeti la Mwananchi jana.

Msendo, ambaye kwa sasa ameungana na familia yake nyumbani kwake Kawe jijini Dar es Salaam, anasema kuwa mipango yake kwa sasa ni kujiweka sawa, na kama akipata kazi atashukuru ili aweze kuisaidia tena familia yake akiwa kichwa cha familia. Imeandikwa na Mpoki Bukuku.

Wednesday, September 17, 2008

Baraza la wanawake


Wajumbe wa mkutano wa baraza kuu la Jumuiya ya Wazazi nchini (UWT) wakijadili jambo wakati wa mapumziko mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquilino

Tuesday, September 16, 2008

Wajapan waja


The JAPANESE PARLIAMENTARY- VICE MINISTER FOR FOREIGN AFFAIRS CHATS WITH THE ACTING PERMANENT SECRETARY IN THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL CO-OPERATION, AMBASSADOR CHARLES SANGA ON ARRIVAL AT THE JULIUS NYERERE INTERNATIONAL AIRPORT IN DAR ES SALAAM YESTERDAY. THE JAPANESE VICE-MINISTER IS LEADING A 37 STRONG DELEGATION OF JAPANESE BUSINESSMEN AND WOMEN TO TANZANIA.(PHOTO BY ASSAH MWAMBENE OF FOREIGN AFFAIRS).

Monday, September 15, 2008

Mugabe na Tsvangirai wapatana




President Robert Mugabe of Zimbabwe and the Movement for Democratic Change MDC-T Morgan Tsvangirai exchange the instruments shortly after the signing ceremony that took place at Rainbow Hotel in Harare this afternoon. President Jakaya Kikwete,the AU chairman attended the ceremony(photos by Freddy Maro)

Sunday, September 14, 2008

Hatari kwa afya


Mzibuaji mitaro ya maji machafu, akitoa taka zilizojaa katika mtaro wa kupitishia maji machafu uliopo mtaa wa Jamhuri jijini Dar es Salaam. Deus Mhagael

Hatari kwa afya


Mzibuaji mitaro ya maji machafu, akitoa taka zilizojaa katika mtaro wa kupitishia maji machafu uliopo mtaa wa Jamhuri jijini Dar es Salaam. Deus Mhagael

msongamano


Baadhi ya abiria na wafanyakazi wa daladala zinazotumia kituo cha Mwenge wanalalamika kwa kutokuwa na huduma ya choo katika kituo hicho, wameiomba manispaa ya Kinondoni kujenga choo. Deus Mhagale.

hatariii


Mwendesha pikipiki akiwa amepakia mwanamke na mtoto bila ya kuwapatia na kofia za usalama kama walivyokutwa Tabata Relini Dar es Salaam jana, jambo ni hatari kwa abiria hao endapo patatokea tatizo la ajali. Picha na Emmanuel Herman

Futari ya jana hii



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Ali Mohamed Shein katikati kakila futari pamoja na Wananchi wa Kisiwa cha Pemba aliyoiandaa kwa ajili ya Wananchi wa Kisiwa hicho huko katika Ikulu ya Chakechake jana. Kushoto ni Mkuu wa
Mkoa wa Kusini Pemba Mh. Juma Kassim Tindwa kulia Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Dadi Faki Dadi. Picha ya Amou Nassor (VPO)

Bakwata



Mufti, Sheikh Issa Shabaan Simba and his deputy Suleiman Gorogosi (right) chats during the National Muslim Council (BAKWATA) special general meeting in Dodoma yesterday. Photo/Jube Tranquilino

Saturday, September 13, 2008

Lucy Kihwele Aachia Ngazi MultiChoice


Hi all
Tomorrow is my last day as Publicity & Public Relations Manager with Multichoice Tanzania.It's been a great eleven(11)years with MultiChoice Tanzania and I am happy that within the period together we managed to achieve many goals and set new bar levels.
I received great opportunity that I could not resist;therefore I will join Standard Chartered Bank as Head of Corporate Affairs.I will advise my new contact details as soon as I have them. I’ll miss you all so much and I do hope our paths cross again someday.
If you wish to stay in-touch,my email address is tabasamun@gmail.com and my cell number will remain the same.Thank you to all of you for touching my life in a wonderful way.I’m blessed to have worked with you all and thanks MultiChoice for having connected me to you all.Please note that Furaha Samalu/Marketing Manager for MultiChoice Tanzania will be taking over my responsibilities as an interim measure and until my successor has been confirmed.
I am sure you will all give her support as always.Lastly and most importantly, thank you very much guys for all the support during my stay at MultiChoice Tanzania.
Take care and be blessed.
Regards,
Lucy T Ngongoseke Kihwele,
Publicity/Public Relations Manager,
MultiChoice Tanzania,
POB 8933,
Ali Hassan Mwinyi Road,
Plot no.964,Oyster bay,
Dar ES Salaam.Tanzania.

Wapambanaji wapata ajali

Herry Makange (kushoto) na Athuman Hamisi.

Herry Makange akimsaidia Athumani mara baada ya kumtoa katika gari



Gari ambalo alikuwa akisafiria Athumani Hamisi, Hery Makange na Anthony Siame namba T 961 AGT baada ya kupata ajali.
Wapigapicha za Habari wa tatu wa vyombo vya habari jijini Dar es salaam leo wamenusurika kufa katika ajali ya gari iliyotokea asubuhi wakiwa njiani kelekea Kilwa katika futari maalum iliyoandaliwa na kampuni ya Vodacom kupitia Voda Foundation.
Wapigapicha hao ni Athumani Hamisi wa Daily News na Habarileo, Herry Makange wa DTV na Channel 10 pamoja na Anthony Siame wa New Habari Cooperation.

Halizao zinaendelea vyema isipokuwa Athumani aliyepata majeraha kichwani tumboni na mkononi baada ya gari alilokuwa akiendesha kupinduka mara kadhaa kabla ya kutua nje ya barabada.
Athumani amesema walikuwa katika mwenzo wa kawaida na walipokaribia Kibiti sehemu ambako barabara ina changarawe juu ya lami, gari iliyumba na kuserereka na kuanguka.
Globu hii ya jamii inamuombea mpiganaji huyu apate nafuu ya haraka. Pia inatoa shukrani kwa msaada wa hali na mali ambayo Vodacom inatoa kwa majeruhi, pia asante ziende kwa Ruge Mutahaba wa Clouds FM ambaye alihakikisha gari inavutwa hadi Dar ambako imeegeshwa kituo kikuu cha kati cha polisi.
Vile vile shukrani za pakee ziwaendee pia Herry Makange aliyebaki kulinda gari na vifaa vya kazi ambavyo vyote vipo salama, na Anthony Siame ambaye hakubanduka ubavuni pa Athumani hadi anafika Muhimbili.
Picha zilipigwa na Siame, na hiyo ya hospitali ilipigwa na bernard rwebangira na pia zipo katika
mrokim.blogspot.com na issamichuzi.blogspot.com na haki-hakingowi.blogspot.com

Thursday, September 11, 2008

Watoto wanapimana nguvu


Watoto wawili walikiwa katika harakati za kuamulia ugomvi baina ya wenzao wawili katika eneo la Mkamba, wilayani
Kilombero. Picha na Jube Tranquilino

Wednesday, September 10, 2008

Seminar with Mwalimu Mwakasege from Tanzania

Pigo la kwanza kwa Makamba



Nape Nnauye aitikisa CCM
UAMUZI wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UV-CCM) wa kumvua uanachama Nape Moses Nnauye, sasa unaonekana dhahiri kukitikisa chama kizima.

Mtikisiko huo umedhihirika kufuatia kauli za wazi za kutoridhishwa na kustushwa na uamuzi huo wa Baraza Kuu, ambazo zimetolewa na makada waandamizi wa chama hicho, wakiwemo Mawaziri Wakuu wawili wastaafu Cleopa David Msuya na Frederick Sumaye.

Licha ya kauli hizo za wazi za makada hao waandamizi, taarifa kutoka ndani ya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho, hadi jana bado ilikuwa ikitambua nafasi za Nape, ambaye ni mwana wa aliyekuwa kada mwandamizi wa CCM marehemu Brigedie Moses Nnauye.

Kauli mpya ya Katibu Mkuu Yusuph Makamba, kwamba Nape bado atabaki na nafasi zake ndani ya chama ni ishara pia kwamba, chama ikiwemo CC na NEC hazijabariki maamuzi ya Baraza Kuu la UV-CCM.

Mtoto akatwa uume wote akitahiriwa



MTOTO Franciss Gasper, mwenye umri wa mwaka mmoja na mwezi
mmoja (pichani) anakojoa kwa kutumia mpira maalumu baada ya kukatwa uume wake wakati akitahiriwa kwenye zahanati inayofahamika kwajina la Olorein iliyopo Mererani mkoani Manyara.
Mama wa mtoto huyo aliyejitambulisha kwa jina la Spola Onero, 24, aliiambia Mwananchi kuwa alimpeleka mtoto wake katika hospitali hiyo Juni 15 mwaka 2008 kwa nia ya kumtahiriwa na alimkuta dakrati aliyemtaja kwa jina la Elisha Elunde na kumfahamisha kuwa anaweza
kufanya kazi hiyo.
Aliendelea kusema kuwa kabla ya hapo mwanae alikua
akisumbuliwa na maradhi (lawalawa) na kuona umuhimu wa kumtahiri ili kuondokana na maradhi hayo. Lakini baada ya kumtahiriwa mtoto huyo alilia sana na alimrejesha katika zahanati hiyo lakini daktari huyo, alimtoa wasiwasi na kumwambia kuwa uume wa motto wake utarejea taratibu.
"Nilimrudisha hospitali na nikamweleza kuwa mtoto hawezi kukojoa na daktari Elunde akanimbia kuwa nirudi nyummbani na nisimwambie mtu
mpaka mtoto atakapopona. Lakini nikaona mtoto anazidi kulia na uume
hakuna," alisema Bi. Spola kwa masikitiko.
Aliongeza kuwa mara kwa mara alipomrudisha mtoto kwa
daktari huyo alimwambia kuwa anaomba iwe siri na anafanya jitihada za kumpa dawa ili uume wa mtoto urejee katika hali ya kawaida.
Naye baba mkubwa wa mtoto huyo aliyejitambulisha kwa jina la
Ray Maseli alisema kuwa aligundua kuwa daktari huyo hakuwa na uwezo wa kumtahiri mtoto huyo baada ya kufanya uchunguzi na hivyo wakaripoti suala hilo kituo cha polisi Mererani na daktari huyo kukamatwa.
Aliongeza kuwa daktari huyo pamoja na kukamtwa aliachiwa huru
siku chache baadaye na kesi haikufunguliwa.
"Tulirejea kituo cha polisi kutoa taarifa upya na ndipo siku ya Alhamisi alikamatwa tena na kupelekwa katika kituo cha polisi kilichopo wilayani Babati. Habari na Hemed Kivuyo, Arusha.

Maamuzi mazito CCM




HATIMA ya mwanasiasa kijana, Nape Nnauye na jina la mgombea wa ubunge ya jimbo la Tarime Mjini ndio mambo yanayotarajiwa kukuna vichwa vya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) baada ya vichwa 39 vya Kamati Kuu kujadili jana hadi usiku wa manane.

Hakuna uamuzi uliotangazwa jana baada ya Kamati Kuu, chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, kujadili masuala hayo, pamoja na agenda nyingine za NEC kwa vipindi viwili, cha kwanza kikianza saa 9.00 alasiri na kingine saa kikianza saa 3:00 usiku.
“Wameamua kupumzika kwa ajili ya futari na tumeambiwa kuwa watakutana tena saa 3:00 usiku kuendelea na kikao cha maandalizi ya NEC,” alisema mmoja wa wafanyakazi kwenye jengo la CCM Makao Makuu mjini Dodoma.

Rais Jakaya Kikwete aliwasili Dodoma jana mchana na aliingia kwenye chumba cha mkutano, akiwa na lundo la nyaraka, hali iliyoonyesha kuwa kikao hicho kilikuwa na shughuli kubwa ya kujadili kabla ya kuyasukumia masuala hayo moto kwenye kikao cha leo.

Tuesday, September 09, 2008

watoto jamani


Vipaji vya watoto huanza kujichomoza mapema wangali wachanga hebu cheki kama hapa hawa watoto wanaonekana kuwa na vipaji vingi, wengine hapa ni madaktari, wengine watakuwa wanasiasa na wengine ndo hivyoo maji lazima yafuate mkondo wake.

Rudisha chenji bwanaaa


Abiria waliokuwa wamepanda kwenye dala dala aina ya Hiace, linalofanya safari zake kati ya Ubungo na Tabata jijini Dar es Salaam (kulia na kushoto), wakimkwida kondakta wa dala dala hilo kutokana na kutokukubaliana naye kuhusu nauli baada ya kushuka katika kituo cha Tabata Relini jana. Picha na Kassim Mbarouk.

Sunday, September 07, 2008

Miss Utalii 2008




Vaileth malkia wa Miss Utalii Tanzania
Na Jessca Nangawe
MREMBO Vaileth Timoth kutoka Dar es salaam jana alifanikiwa kutwaa taji la Miss utalii baada ya kuwabwaga wenzake 20 na kunyakuwa gari mpya aina ya Nissan Premira yenye thamani ya shilingi mil.15 katika kinyang'anyiro cha kumsaka miss utalii Tanzania lililofanyika kwenye ukumbi wa New World Cinema, Mwenge.
Shindano hilo lililokuwa la kusisimua na lenye ushindani wa hali ya juu jumla ya warembo 21 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania walipanda jukwaani katika mavazi tofauti tofauti yaliyokua yakiutangaza utalii na utamaduni wa Tanzania.
Katika hatua ya kwanza warembo kumi walifanikiwa kuingia katika hatua ya kumi bora ambapo kila mmoja alitakiwa kuelezea utalii wa Tanzania kwa jinsi anavyofahamu.
Waliofanikiwa kuingia katika hatua ya tano bora ni Zulfa Hahya (Kagera), Elizabeth Kilya(Kilimanjaro),Evalyne Julius (Manyara), Aneth Kanora (Arusha) na Vaileth Timoth Dar es salaam.
Aidha mshiriki kutoka Mkoa wa Mara, Josina Henry aliibuka Miss Vipaji mara baada ya kuonyesha umahiri mkubwa katika kuimba na kuonyesha uhalisia wa utamaduni wa Kitanzania katika shindano lililofanyika mkoani Morogoro wiki iliyopita na kujinyakulia kitita cha shilingi laki 5.
Zawadi kwa mshindi wa pili alikuwa ni Shs mil.2 ilikwenda kwa Aneth Kanora (Arusha) , wa tatu mil 1.5 Evalyne Julius (Manyara) wa nne Elizabeth Kilya (Kilimanjaro) na wa tano Zulfa Yahya (Kagera) pamoja na Miss vipaji waliondoka na laki 5 kila mmoja.
Naye Waziri wa Maliasili na utalii Shamsa Mwangunga ambae alikua mgeni rasmi katika shindano hilo alimtaka mrembo huyo kuiwakilisha Tanzania vema kwa upande wa mambo ya utalii katika mashindano ya Dunia.
"Tumekuwa na warembo ambao wamekuwa wakiwakilisha nchi kwenye mashindano ya dunia sasa ni wakati wako kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania,"Alisema Mwangunga.
Aidha Waziri alisisitiza waandaaji wa shindano hilo kutoa zawadi kwa wakati na ili walikusudia kwa nia ya kurudisha imani ya washiriki na wazazi kwa ujumla.