Saturday, September 29, 2007

Usafiri wa kwetu Mtwara


huku kwetu mambo poa sasa safari inachukua masaa 12 tu tofauti na ilivyokuwa zamani.

Zee Comedy hawa aaaa









Hivi kwa mfano hivi sasa liserekali lote la CCM likiwa na baraza la mawaziri 62 limeshindwa kukabiliana na tuhuma za ufisadi alizozitoa mtu mmoja, Dk Willibrod Slaa, pamoja na kujitahidi kufurukuta kujibu, nadhani majibu mmeyaona, kwanza yametolewa kimficho, hakuna aliyejitokeza hadharani akajibu, li-statement limetolewa jioni halafu hakukuwa na mtu, likasokomezwa kwenye vyombo vya habari kiupendeleo, halafu sijui wamepata nini.

Kwanini wasingelitumia kundi la Ze Commedy ambalo leo katika uzinduzi wa mfuko wa uadilifu,uwajibikaji na uwazi (FEAT) katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar, ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa rais Dk Mohamed Shein, majamaa wamekamua ile mbaya.

Kwa mfano wangekodi hili kundi likazunguka nchi nzima, pamoja na macommedy lakini mambo yangeeleweka. Angalieni katika uzinduzi wa mfuko huo mambo yalikuwa mukide.

Vyombo hivi ambavyo vinasimama na vinajihusisha na uwajibikaji, uwazi na uadilifu hapa nchini vitapewa uwezo na rasilimali kupitia ufadhili wa mfuko huu vitekeleze kwa ufanisi zaidi majukumu yake ambayo ni pamoja na kufuatilia utekelezaji wa mipango ya serikali katika azma yake ya kukuza na kudumisha utawala bora.Vile vile mfuko huo utalenga kuvisaidia vyama vya kitaaluma na visivyo vya kiserikali kwa kuvipa uwezo ili kuimarisha maadili ya kitaaluma miongoni mwa wanachama wake.

Aidha baadhi ya asasi/tasisi za umma ambazo zimelengwa kunufaika namfuko huu ni bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania na kamati zake,Ofisi ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali, taasisi ya kuzuia nakupambana na rushwa, tume ya haki za binadanu na utawala bora.

Mfuko wa uadilifu,uwajibikaji na uwazi ni sehemu ya mpango huu na umetengewa jumla ya dola za Marekani milioni nne na nusu kwakipindi cha miaka miaka mitano.Mfuko huo utaendeshwa na kamati ya uendeshaji chini ya usimamizi wa sekretari ya maadili ya viongozi wa umma ambayo ni idara inayojitegemea chini ya ofisi ya Rais,utawala bora.Ni hayo tu kwa ufupi washkaji wangu. Picha zimetoka kwa MICHUZI JUNIOR

Tamko la Serikali Kwa Slaa

SERIKALI imetoa taarifa kujibu shutuma za rushwa kwa viongozi na watendaji wakuu wa serikali zilizotolewa na Mbunge wa Karatu kwa kupitia CHADEMA Dk. Wilbrod Slaa hivi karibuni.

Taarifa hiyo iliyotolewa Ijumaa Sept. 28, 2007 na Waziri ya Habari, Utamaduni na Michezo Mh. Muhammad Seif Khatib imesema shutuma hizo hazina msingi wowote na zinastahili kupuuzwa.

"Tafsiri pekee na mantiki ya kutolewa kwa tuhuma hizi wakati huu ni kuwa hili ni jaribio la kuwavunja moyo wananchi kuhusu manufaa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005," imeeleza.

Imesema kwmba Serikali inapinga vitendo vya rushwa nchini "kwa nguvu zake zote" na kama Dk. Slaa na wenzake wana lengo la kupiga vita rushwa basi tuhuma hizo wangezifikisha katika vyombo vinavyohusika ili zishughulikiwe.

Dk. Slaa, akiwaongoza wanasiasa wenzake kadhaa wa kambi ya upinzani, walitoa tamko hadharani Septemba 15 mwaka huu kwenye viwanja vya Mwembeyanga, wilaya ya Temeke, mkoani Dar es Salaam, kuwatuhumu viongozi kadhaa wa umma kuwa wanashiriki vitendo vya rushwa.

Kufuatia tuhuma hizo, gazeti la kila wiki la MwanaHalisi linalotolewa jijini Dar es Salaam, limekuwa likisambaza tuhuma hizo bila ya kutafuta ukweli wake, taarifa imesema.

Taarika kamili ya Serikali inatarajiwa kuchapishwa ikiwa ni tangazo katika magazeti kadhaa ya kila siku Jumamosi Sept. 29, 2007.

Taarifa imesema Serikali ya Tanzania wakati wote imekuwa ikitekeleza mipango na mikakati mbalimbali ya kupambana na rushwa, awamu ya kwanza ya mwaka 1997/2004 na awamu ya pili mwaka 2005/2010.

Imenukuu Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005, Ibara ya 110, inayoelezea mapambano dhidi ya rushwa na tamko la Rais Jakaya Kikwete dhidi ya rushwa katika hotuba yake ya kuzindua Bunge Desemba 29, 2005.

Serikali imeanzisha Ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwenye Wilaya zote nchini, imeshughulikia taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na inashirikisha wananchi katika mapambano dhidi ya rushwa, imesema.

"Serikali isingebuni na kutekeleza mikakati hii kama isingekuwa na nia ya dhati ya kupambana na tatizo la rushwa [WINDOWS-1252?]nchini…Serikali haikutarajia kwamba watakuwepo miongioni mwetu watakaotumia fursa hizi kuibua taarifa za uzushi kwa lengo la kuchafua majina ya wenzao ili kujipatia umaarufu wa kisiasa wasioustahili," imeongeza.

Taarifa imesema Serikali inaelewa kwamba Dk. Slaa na wenzake ni miongoni mwa viongozi walioshiriki katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 wakitegemea kushinda lakini walishindwa na wananchi kuichagua CCM.

Imesema wananchi wanayaona mafanikio mengi katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kwamba wanachokitafuta wale walioshindwa ni kile walichokikosa na hivyo wanajaribu kuwahadaa na kuwachanganya wananchi.

"Serikali ya Awamu ya Nne ni imara na iko makini kutekeleza ahadi zake zote ilizowaahidi wananchi wakati ilipokuwa inawaomba ridhaa ya kuingia madarakani.

"Hivyo ni vyema wananchi wakatambua kwamba wapinzani hawa hivi sasa wanatapatapa na wanataka kutuondoa katika lengo letu la kuwaletea maisha bora Watanzania," imeongeza.

Friday, September 28, 2007

Hayati Kaduma kuzikwa Iringa


Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Michuzi zinaeleza kuwa MSANII mkongwe wa sanaa za maonesho nchini, Mzee Godwin Zilaoneka Kaduma, aliyefariki dunia jana mchana kwa maradhi ya kupooza (stroke) anatarajiwa kusafirishwa leo Ijumaa kuelekea nyumbani kwake Bagamoyo na baadaye kijijini kwake Itamba, Iringa, kwa Mazishi.
Enzi za uhai wake marehemu mzee Kaduma aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Sanaa la Lugha ambayo kwa sasa imebadilishwa na kuwa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni.
Baada ya kustaafu Serikalini marehemu mzee Kaduma aliendelea na shughuli za sanaa akiwa kama kiongozi na mtendaji katika sanaa za maonesho ikiwamo ngoma na maigizo.
Alikuwa mwanzilishi wa Kituo cha Sanaa za maonesho Tanzania (TzTC) na Taasisi ya sanaa za maonesho Mashariki mwa Afrika (EATI) ambapo pia alikuwa Katibu Mtendaji wa kwanza wa asasi hizo.
Aliamua kupumzika kuzitumikia asasi hizo mwaka 2003, ambapo aliendelea na shughuli zake za kawaida za kufundisha masuala ya sanaa katika Chuo cha Sanaa Bagamoyo akiwa kama mkufunzi mwalikwa katika Idara ya tamthiliya ambapo alikuwa akifundisha somo ya uandishi wa michezo ya kuigiza kazi aliyokuwa anaedelea kuifanya hadi kifo kilipomkuta.
Marehemu Kaduma pia alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha Hakimiliki (Cosota) hadi kufa kwake, kazi ambayo aliifanya kwa ufanisi na uelewa kiasi hata kuamsha wasanii katika kuona umuhimu wa chombo hicho na kujisajili wao na kazi zao kwa wingi kuliko wakati wowote wa uhai wa Cosota.
Kwa mara ya mwisho, marehemu mzee Kaduma alifanya onesho akiwa msanii wa kujitegemea mwezi Juni mwaka huu, wakati wa semina maalum ya kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii, iliyoandaliwa na Mfuko wa Utamaduni Tanzania ambapo alitamba na shairi la 'Naililia Tanzania'.
*KWA MUJIBU WA RATIBA ILIYOTOLEWA USIKU HUU NA KAMATI YA MAZISHI INAONESHA MWILI WA MAREHEMU MZEE KADUMA UTAAGWA ASUBUHI SAA 4 KATIKA HOSPITALI YA MUHIMBILI, KABLA YA KUPELEKWA NYUMBANI KWAKE BAGAMOYO AMBAKO UTAAGWA NA WAKAZI WA HUKO NA SAA NANE SAFARI YA KUMSAFIRISHA ITAANZA SAA 8 MCHANA KUELEKEA KIJIJINI KWAKE ITAMBA, IRINGA, KWA MAZISHI
MOLA AILAZE PEMA PEPONI ROHO YA MPENDWA WETU MZEE KADUMA
AMINA

Rais Kikwete Umoja wa Mataifa





STATEMENT BY H. E. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA,
AT THE 62ND SESSION OF THE UNITED NATIONS

GENERAL ASSEMBLY, NEW YORK,
27th SEPTEMBER 2007

Your Excellency Srgjan Kerim, President of the United Nations General Assembly;
Your Excellency Ban Ki-moon, Secretary-General of the United Nations;
Excellencies Heads of State and Government;
Distinguished Representatives;
Ladies and Gentlemen.

Let me begin by congratulating you, Dr. Kerim, for your well deserved election as President of the 62nd Session of the General Assembly. You can
count on Tanzania’s full support and cooperation as you discharge your mandate. I also commend your predecessor, Madam Shaikha Haya Rashed Al Khalifa, for having skillfully presided over the 61st session.
We congratulate Mr. Ban Ki-moon for his unanimous election as the eighth Secretary General of the United Nations, which reflects his distinguished diplomatic track record, integrity and commitment to international diplomacy.
I also thank him for the honour and trust he has bestowed upon my country, by appointing an accomplished Tanzanian academic and diplomat to the post of UN Deputy Secretary General. I take this opportunity to once again congratulate Dr. Asha-Rose Migiro, for her appointment to this high office. I trust that such a combination of diligence and devoted leadership will steer this important institution towards greater heights of success.

Climate Change
Mr. President;
I highly commend the Secretary General for his decision to convene the High Level Event on Climate Change four days ago. The meeting gave us an opportunity to discuss the state of health of our common planet. It also gave us the opportunity to renew our commitment to take the necessary steps to correct the mistakes we have done.
The recent report by the Intergovernmental Panel on Climate Change (IPCC) has confirmed that warming of the earth’s climate system is indisputable and is attributable to, by and large, human activities.
Africa and many Small Island States contribute the least to the greenhouse gases that cause this phenomenon; yet, significant impact of climate change is evident on our countries. Most countries are experiencing severe floods, frequent and prolonged droughts, reduced water supply, decline in crop yields, rising sea levels, and an increase in water borne diseases. These impacts of climate change can affect African countries’ ability to achieve the Millennium Development Goals (MDGs). Climate change threatens to undo the results of decades of development efforts.
In Tanzania, for certain, the impact of global warming is real and visible. There has been a steady increase in temperature for the past 30 years, adversely affecting almost all sectors of the economy.
Severe droughts have been recurrent in the past few years. Water levels in Lake Victoria and Lake Tanganyika have dropped significantly. There has been a dramatic recession of 7 km of Lake Rukwa in the Western part of the country in the past 50 years. About 80 per cent of the glacier on Mount Kilimanjaro, the highest in Africa, has been lost since 1912.
We have prepared a National Adaptation Program of Action. There is a national programme of planting over 200 million tree seedlings per annum besides having reserved 24 percent of our territory for national parks and 38 percent for forest reserves.
We trust that countries like Tanzania, which have reserved such large tracts of land for protection of wildlife and forests, including an ambitious tree planting programme for global good, would be adequately compensated for their significant contribution to carbon sequestration.
We have prepared a National Adaptation Program of Action (NAPA) and undertaken an indepth analysis of the impact of climate change on agriculture, health, water as well as a technological needs assessment for adaptation and poverty reduction.
Tanzania hopes that the Climate Change Adaptation Fund would be successfully negotiated and concluded together with other proposed innovative sources of financing discussed during the High Level Event earlier this week.

Mr. President;
Since the causes and consequences of climate change are global, international cooperation and partnership in addressing them is imperative. Tanzania supports the Clean Development Mechanism (CDM), which assists developing countries to achieve sustainable development and requires developed countries to fulfill their commitments under the Kyoto Protocol.
So far Africa has the least number of CDM projects. Of the over 800 projects around the world, Africa has about 20 projects only. This inequitable distribution is of concern to us and must be resolved in order for it to contribute meaningfully to the sustainable development of Africa.
I wish to emphasize that international collective action is critical in developing an effective response to global warming. Indeed a review process to consider further commitment of the Parties under the Kyoto Protocol beyond 2012 is urgent and necessary. Tanzania promises to participate actively at the Bali Summit.

UN Reforms/One UN
Mr. President;
Tanzania welcomes the recent milestones in the UN reform process namely the establishment of the Peace Building Commission, the Human Rights Council and the Central Emergency Relief Fund. We attach great importance to these new initiatives and we want to contribute to their success.
In its report of November 2006 entitled, “Delivering as One”, the UN Panel on System-wide Coherence made valuable recommendations, including the establishment of a “One UN” system at the country level. For, we in Tanzania, believe that the development coordination agenda is best served when we have at the country level one programme, one budgetary framework, one leader, and one office.
Tanzania is pleased to be among the eight “One UN” pilot countries. The One UN Programme is for us a logical development from the United Nations Development Assistance Framework (UNDAF), a framework that is fully aligned with our national priorities. The efficiencies in aid delivery expected through “One UN” will certainly contribute to enhancing our capacity to attain the MDGs.
I call upon member states to give our organization, the United Nations, the resources it needs to implement this pilot project. The project should not fail for lack of resources. I also urge the Bretton Woods Institutions to take a keener interest in this initiative and join in the efforts to realize its objectives.
The need to make the UN Security Council more representative is an age old demand of all of us. Time has come to walk the talk. We need to move from rhetoric to action. Now is the time. Tanzania assures the entire UN membership our whole-hearted support and cooperation in this process.

Millennium Development Goals (MDGs)
Mr. President;
We are now halfway through the time-line of 2015 set for achieving the Millennium Development Goals. Yet we are not half-way in realizing the targets as spelt out at the Millennium Summit of 2000. We are in this unfortunate state of affairs because the additional resources expected and promised by the developed countries have not come forth. I urge this august General Assembly to renew its appeal to the developed nations to deliver on their promise.
In this regard, we welcome the initiative mentored by the Norwegian Prime Minister Mr. Jens Stoltenberg to launch a global campaign to mobilize resources for achieving the MDG 4 on reducing infant mortality rates and MDG 5 on reducing maternal mortality rates. Tanzania supports the effort and we are happy to be associated with it. I appeal to all of us to support the initiative. It is our hope that, developed nations will support the campaign by providing the required resources.
On the same vein, we commend Secretary General Ban Ki-moon for establishing the African MDG Steering Group. Africa is excited about it. We trust that it will give new impetus in assisting Africa attain all MDGs.
We also welcome the historic decision taken by the President of the General Assembly to convene a special summit of leaders to discuss the MDGs during this session. We support this wise decision of our President for we believe it will provide the needed momentum for the timely achievement of the MDGs in Africa.
Regional Issues: Africa
Mr. President;
Tanzania has played, and will continue to play, its historic role in the search for peace, security, stability and development in Great Lakes region. I thank the United Nations and the Group of Friends of the Great Lakes for their support to the processes of the International Conference on the Great Lakes. As we all know, at the Nairobi Conference held in December, 2006, an historic Pact on Peace, Security, Stability and Development in the Great Lakes Region was signed. A new era of hope, collective security and cooperation for development was ushered in. For sure, if the letter and spirit of the Pact are implemented, the Great Lakes Region will be a completely new place from the one we are used to know.
We are happy that member states have committed to ratify the Pact by the end of this year. This will enable the Pact to come into force. We look forward to continued support from the UN, friends of the Great Lakes and the international community at large as we endeavour to get durable peace, stability and sustainable development.
Mr. President;
Burundi and DRC
We are happy with the tremendous progress made in Burundi. Peace has been restored and life has come back to normal. Tanzania will continue to work with the region and South Africa to ensure the full operationalization of the peace agreement signed between the Burundi government and the FNL-Palipehutu.
We are concerned with the fluidity of the situation in North Kivu. We hope wisdom will prevail on the parties concerned to give peace a chance. The people of the DRC deserve it. We in Tanzania promise to play whatever part may be required of us.
With restored peace in Burundi and many parts of the Democratic Republic of the Congo (DRC), it is incumbent upon us in the international community to encourage and assist refugees to go back to their respective countries. This is what the Tripartite Commissions involving Tanzania, UNHCR and the respective countries of Burundi and DRC have been doing. Our joint Commissions have been encouraging repatriation of refugees on voluntary basis and we have been assisting those who came forward. The results are encouraging but things could be better. A word of encouragement from this organization could make a difference.
Mr. President;
Tanzania believes that the return of refugees to their country of origin is a sovereign right which should not be denied. It is also the ultimate testimony and guarantor of the peace so attained. It is not fair, it is not right for people to continue to live in refugee camps after peace has been restored in their countries of origin.
Situation in Darfur
Mr. President;
The current progress with regard to Darfur gives us hope. The adoption of Security Council Resolution 1769 to deploy a hybrid force of peacekeepers from the African Union and the United Nations, and the renewed political dialogue among the parties to the conflict, holds promise for the stalled peace process and the humanitarian crisis that unfortunately persists there.
Tanzania applauds the unique partnership which has evolved between the African Union and the United Nations. We stand ready to contribute troops to the hybrid force.
Somalia
Mr. President;
We are encouraged by recent developments with regard to internal political dialogue in Somalia. We are equally happy with the attention given to Somalia by the Security Council and the United Nations Secretary General. We welcome the recent Security Council resolution 1772 (2007) which supports the political process in Somalia and the role of AMISON. As member of the Somali Contact Group, Tanzania promises to continue to be pro-active and offers to contribute in the training of the Somali military.
Western Sahara
Mr. President;
The United Nations should remain seized with the issue of Western Sahara. Tanzania reaffirms its support for the inalienable right of the people of Saharawi to decide and choose the way forward. We urge the United Nations to intensify its efforts to find an honourable and just solution to this longstanding decolonization issue.
The Middle East
The crisis inside the Palestinian territories is a matter of great concern to us. Tanzania remains supportive of efforts aimed at creating two states, Israel and Palestine, living side by side, at peace with each other. This presents, in our view, the best hope for sustainable peace in the region. We applaud and welcome the renewed international interest and effort in line with the relevant UN resolutions.
Lebanese Situation
The Lebanese government and peoples need and deserve the continued support of the UN and all of us in the international community as they reconstruct and stabilize their country. In this regard, Tanzania is glad to be a party to the efforts being expended by the United Nations, through our modest contribution to the Interim Force in Lebanon (UNIFIL). We are ready to increase our contribution whenever required to do so.
Conclusion
Mr. President;
In conclusion, Mr. President, Tanzania reaffirms its belief in and commitment to multilateralism and the United Nations. You can count on Tanzania’s continued support to this organization and the ideals it stands for.
I thank you.

Thursday, September 27, 2007

Jongwe


Robert G. Mugabe, President of the Republic of Zimbabwe, addresses the general debate of the sixty-second session of the General Assembly, at UN Headquarters in New York.

Dk Migiro kazini


Deputy Secretary-General Asha-Rose Migiro (right) meets with Queen LaMbikiza of the Kingdom of Swaziland, at UN Headquarters in New York. Location: United Nations, New York

Umoja wa Mataifa



Wide-view of the Media Centre for correspondents covering the activities of the opening of the general debate of the sixty-second session of the General Assembly, at UN Headquarters in New York.
Location: United Nations, New York

Makamanda Waula

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jakaya Mrisho Kikwete amewapandisha vyeo Maafisa wa jeshi la Polisi katika ngazi za Manaibu Kamishna na Makamishna Wasaidizi Waandamizi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamishna Msaidizi wa Polisi, Essaka Mugassa, rais amewapandisha vyeo Makamishna Wasaidizi Waandamizi Peter Kivuyo wa Makao Makuu ya Upelelezi Dar es salaam, Nestory Mpembela ambaye ni Mkuu wa
Idara ya Mawasiliano Makao Makuu na Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Omary Rashid Mganga kuwa Manaibu Kamishna.

Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama amewapandisha vyeo Makamishna Wasaidizi kumi na nane kuwa Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Jeshi la Polisi Ambao ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Manyara , Luther Mbutu; Kamanda wa Polisi mkoa wa Kaskazini Unguja , Mselemu Masud Mtulia; Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Zelothe Stephen; na Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Seleman Hussein Kova.

Wengine ni Antony Joel Mwami ambaye ni Mkuu wa Kikosi cha Polisi Anga; Neven
Isaack Mashayo Mkuu wa Chuo cha Polisi Zanzibar; Juma Omary Kondia ambaye ni mkuu
wa mawasiliano Kanda Maalum ya Dar es Salaam; pamoja na Bw Kenneth Kasseke na
Faraji Kayuga wa Makao Makuu ya Polisi Zanzibar

Waliopanda vyeo na kuwa Makamishna Wasaidizi Waandamizi wengine ni Mkuu wa
Mawasiliano Msaidizi Makao Makuu Abdul Issa Nina; Mkuu wa kitengo cha Maendeleo
cha Jeshi la Polisi Zuhura Munisi, Boniface Kanyunya Mpaze na John Kimario wa
Makao Makuu ya upelelezi Dsm.

Wengine ni kutoka Makao Makuu ya Polisi Dsm ambao ni Alexander Calist Mushi, Bw.
Rashid Ally Omar, Bw, Aswegen Wilson Magambo Bw Issaya Juma Mngulu na Mkuu wa
kikosi cha Bendi Makao Makuu, Mbazi Yohana Mchomvu. Mheshimiwa Rais amewapandisha vyeo maafisa hawa wa Jeshi la Polisi kuanzia Agosti 31, 2007

Futari



Ni jioni mwanana wakati Balozi mpya wa Marekani nchini Tanzania, Mark Green, alipotembelea kijijini Misugusugu, Kibaha pamoja na kituo cha kulea watoto yatima cha Mwinyibaraka, ambacho ni sehemu ya Taasisi ya Kiislamu ya Mwinyibaraka, na kuungana na viongozi na wakazi wa eneo hilo katika ibada ya kufuturu iliyokuwa imeandaliwa na taasisi hiyo.

Wednesday, September 26, 2007

Breking News Ajali Ajaliiii

Frederick Katulanda wa Mwananchi anaripoti kuwa madiwani watatu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wamejeruhiwa baada ya msafara wa Waziri Mkuu kupata ajali na magari matatu kugongana.

Ajali hiyo imetokea majira majira ya saa 4:45 asubuhi katika barabara ya Nkirizya wakati Waziri Mkuu akitokea uwanja wa ndege kuelekea mjini Nansio.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Zelothe Steven alithibitisha kuwepo kwa ajali hiyo na kueleza kuwa chanzo ni vumbi.

Magari yaliyogongana ni Toyota Landcruiser STJ 3292 mali ya Tamesa lililokuwa likiendeshwa na Barnabas Dioniz, T 686 ANU mali ya Meneja wa TRA wilayani hapa lililokuwa likiendeshwa na Chacha Kamene pamoja na Toyota Hiace T428 AAD ambalo lilikuwa na madiwani.

Madiwani walioumia na kujeruhiwa ni Juma Mbasa wa kata ya Ilugwa, Bernard Polisi kata wa Kagunguli na Cypriani Nabigambo wa kata ya Bwiro. Madiwani hao wametibiwa na kuendelea na ziara. Chanzo ni vumbi na magari kuwa karibu karibu.

Naye Thobias Mwanakatwe wa PST, Chunya, anaripoti kuwa Msafara wa NaibuWaziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bi. Mwantum Mahiza jana ulipata ajali baada ya gari waliokuwa wakisafiria kugongwa na lori.

Msafari huo ulikuwa na maofisa wa Idara ya Ukaguzi Nyanda za Juu,waandishi wa habari na askari.Ajali hiyo ilitokea juzi 11:45 jioni katika kijiji cha Luwanjilowilayani Chunya Mkoani Mbeya wakati msafara huo ukitokea katika ziaramjini Chunya kurudi Mbeya mjini.

Lori hilo lenye namba za usajili T 683 AFK liligonga gari lenye nambaSTK 3170 ambalo lilikuwa likiongoza msafara wa Naibu Waziri huyo likiendeshwa na dereva Abel Mwakatete likiwa limewabeba maofisa hao.

Maofisa wa Idara ya Ukaguzi waliokuwa katika gari hilo lililogogwa niNaibu Mkaguzi wa Kanda, Mama Arevo, Mkuu wa shule ya Sekondari Tukuyu,Bw. Wakili Mwangoka, mwandishi wa habari wa RTD na mwandishi wa habariwa Kampuni ya The Guardian, Bw. Thobias Mwanakatwe pamoja na askari,Sajenti Seif ambao hata hivyo hawakujeruhiwa.

Tuesday, September 25, 2007

Prof Kapuya Chupu Chupu








Waziri wa ulinzi na jeshi la Kujenga Taifa, Profesa juma Othman Kapuya, amenusurika
katika ajali mbaya ya gari ambayo pia ilipoteza maisha ya walinzi wake wawili pamoja
na diwani wa kata ya Ushokola wilayani Urambo.

Kwa Mujibu wa mkuu wa mkoa wa Tabora, Bw Abeid Mwinyimsa na kamanda wa polisi
mkoani Tabora, Muhud Mshihiri, ajali hiyo ilitokea katika kijiji Usindi kata ya
Kaliua.

Taarifa hiyo imesema kuwa kijiji hicho kiko umbali wa kilomita nane kutoka katika
makao makuu ya kata hiyo mjini Kaliua, ambako ndiko nyumbani kwa Waziri Kapuya.

Watu watatu waliofariki katika ajali hiyo ni pamoja na walinzi wawili wa Profesa
Kapuya, ambao ni askari jeshi na diwani wa kata ya Ushokola wilayani Urambo, ambaye
alikuwa amfuatana na kiongozi huyo katika ziara yake ya kuhimiza maendeleo.

Mlinzi mmoja, Ramadhan Mlini, alifariki papo hapo hapo pamoja na diwani Haruna
Shamsheri, huku mlinzi mwingine Shaaban akifariki muda mfupi baada ya
kufikishwa hospitalini kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

watu wengine wanne waliokuwa kwenye gari hiyo, ambao wamepata majereha ni pamoja na
mwenyekiti wa CCM wa wilaya ya Urambo Twaha Ngosso, msaidizi wa waziri huyo Luteni
Kanali Leopald Kalima, dereva wa gari hiyo Christopher Charles mwenye namba MT 57185
na mfanyabiashara Shigela Mabula.

Taarifa za awali kuhusu ajali hiyo zinasema kuwa chanzo chake ni kupasuka kwa
gurudumu la mbele la upande wa kulia na hivyo kupinduka.

Waziri kapuya, amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Urambo mkoani Tabora, pamoja
na majeruhi wengine wanne, huku mipango ya kuhakikisha kuwa anapata tiba bora zaidi
ikiendelea kufanywa.

Waziri Kapuya, alikuwa katika ziara ya kuhamasisha maendeleo katika jimbo la Urambo
Magharibi, akitoka katika kijiji cha Kashishi kilomita zaidi ya 100 kutoka makao
makuu ya jimbo hilo mjini Kaliua.

Mudhihir atolewa Muhimbili



MBUNGE wa Mchinga, Mudhihir Mohamed Mudhihir, ameruhusiwa na madaktari kutoka Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) baada ya hali yake kuonekana inaendelea vizuri.

Akuzungumza na waandishi wa habari katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam jana, daktari wa mbunge huyo, Paul Marealle, alisema kuwa, wamemruhusu baada ya kuona anaendelea vizuri bila ya matatizo yoyote.

Daktari huyo aliongeza kuwa moja ya masharti waliyompa ni kwenda hospitali kufunga kidonda kila baada ya siku moja.

"Mbunge tumemruhusu baada ya kuona hali yake inaendelea vizuri tofauti na awali alivyoletwa. Tuna matumaini hata atakapokuwa nyumbani atakuwa anaendelea vizuri tu bila matatizo yoyote," alisema Marealle.

Wakati huo huo; Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samwel Sitta aliliambia gazeti hili kwa simu jana kuwa, Bunge lina wajibu wa kumuhudumia mbunge huyo tangu alipopata ajali hadi mwisho.

Sitta alisema kuwa, wameandaa mazingira ya kumpeleka Mudhihir nchini Ujerumani kwa ajili ya matibabu zaidi.

"Mpaka sasa hivio wabunge wote wanatambua kwamba mbunge mwenzao anaumwa na wako tayari kushirikiana naye atakapopelekwa Ujerumani kwa ajili ya matibabu zaidi.

"Katika safari hiyo ataambatana na mbunge mmoja ambaye atamsindikiza. Kwa sasa tunasubiri gharama za matibabu zitakazoletwa na madaktari kutoka Ujerumani kwa faksi ili kufahamu gharama zinazotakiwa kumuhudumia kabla ya yeye kwenda huko," alisema Sitta.

Kwa mujibu wa Sitta, Mudhihir atatarajiwa kuanza safari ya kwenda Ujerumani kwa matibabu ndani ya siku mbili zijazo. Kuanzia jana na leo, madaktari wa MOI na wa Ujerumani wanashirikiana kupata hospitali ambayo atapelekwa.

Monday, September 24, 2007

Hasara Sea Cliff zaidi ya Sh 32 bilioni






*Dk Shein atembelea kuona athari
*Asema moto huo umeathiri sekta ya uwekezaji
*Ataka watanzania kuishi kwa tahadhari

Na Kizitto Noya wa Mwananchi

MKURUGENZI Mtendaji wa Hoteli ya Sea Cliff ya jijini Dar es Salaam, Ketan Patal, amesema hasara iliyosababishwa na kuungua kwa hoteli hiyo ni sawa na thamani ya uwekezaji wa mradi huo aambayo ni zaidi ya Sh32.5 bilioni.

Akizungumza mbele ya Makamu wa Rais, Dk Mohamed Shein aliyetembelea eneo la tukio kuona athari za moto ulioteketeza hoteli hiyo, Patal alisema hata hivyo thamani ya vitu vyote vilivyoungua haijajulikana.

"Haiwezekani kukisia gharama za uharibifu huo sasa, lakini ninachoweza kusema ni kwamba kilichoharibika ni mradi ulioanzishwa miaka kumi na moja iliyopita kwa thamani ya dola za Marekani 25 milioni (sawa na Sh32.5 bilioni)," alisema Patal.

Alisema kwa sasa uongozi wa hoteli hiyo kwa kushirikiana na vikosi mbalimbali vya ulinzi na usalama, wanachunguza chanzo cha moto huo mkubwa na kutathmini gharama halisi ya uhalibifu uliotokea.

Awali, Meneja Mkuu wa hoteli hiyo, Keven Stander, alimweleza Makamu wa Rais kuwa uchunguzi umebaini kuwa hakuna mtu aliyejeruhiwa katika ajali hiyo ingawa hasara iliyopatikana ni kubwa.

Alisema karibu wageni wote waliokuwapo hotelini hapo juzi walifanikiwa kutoka wakiwa salama huku raia wa Uingereza na Ufaransa wakiwa wamechukuliwa na maafisa wa balozi zao na kupelekwa katika hoteli ya MovenPick ya jijini Dar e Salaam.

Saturday, September 22, 2007

Balozi aitaka Tanzania ijisafishe



*Ni kuhusu tuhuma za BoT na suala la madini
*Aonya isipofanya hivyo itachelewesha kupata misaada
*Ashangaa nchi kuwa maskini wakati ina rasilimali nyingi

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI ya Uholanzi imeeleza kukerwa na tuhuma za rushwa na ufisadi ambazo zinaendelea kujitokeza nchini dhidi ya viongozi mbalimbali, zikiwamo zinazoihusu Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na nyingine zinazohusisha moja kwa moja upotevu wa rasilmali za umma huku serikali ikiwa kimya

Balozi wa Uholanzi nchini Karel van Kesteren alisema hayo juzi usiku wakati akiwakaribisha maofisa wapya wa ubalozi huo nchini ambao ni Mkuu wa Idara ya Uchumi, Steef van den Berg na Mirjam Tjassing ambaye ni afisa katika idara hiyo.

"Lakini, lazima nielezwe kwanza, kwamba ninaguswa sana na tuhuma zinazotolewa mara kwa mara kuhusu ufisadi. Ninaguswa zaidi na madai mengi ya ufisadi ambayo siku za karibuni yamekuwa yakiendelea kutolewa," alisema balozi huyo.

Kauli ya Balozi huyo ni ya kwanza kutolewa na ubalozi wa kigeni nchini baada ya vyama vya upinzani vitangaze tuhuma za viongozi mbalimbali wa serikali wanaodaiwa kujihusisha na ufisadi.

Alisema licha ya hatua zinazochukuliwa na serikali ya Tanzania katika kuinua uchumi wa nchi kuwa za kuridhisha, lakini taarifa zinazohusu rushwa katika ujenzi wa Majengo pacha ya BoT, zinaichafua sifa ambayo nchi imeanza kujijengea.

"Tanzania inazidi kuingia katika nchi zenye uchumi wa kati, hilo linatia moyo, lakini ili iweze kufikia mahali hapo, inahitaji kuweka mazingira mazuri zaidi kiuchumi.

Alisema Tanzania inatakiwa kujenga mazingira ambayo sekta binafsi iweze kukua, kufanya kazi na kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa nchi na kuitaka serikali kujenga mazingira ambayo yatavutia wawekezaji kutoka nchi za nje, ikiwamo Uholanzi kuja na kufanya shughuli zao hapa.

"Tuhuma zinazohusiana na BoT (hasa Idara yake ya Malipo ya Nje, ambazo nasikia zimeanza kuchunguzwa kwa kazi inayofanywa na wakaguzi huru wa nje), pia naguswa mno na gharama halisi za ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo (BoT twin towers)," alisema balozi huyo.

Alisema majibu sahihi na kwa muda unaotakiwa kutoka serikalini, ndiyo yanayotakiwa kwani hayo ndiyo yatakayoweza kusaidia kuipa imani jamii ya wahisani wa kimataifa, serikali zao, kama ilivyo kwao Uholanzi, au hata mabunge, walipa kodi wao na hata wawekezaji hatua ambayo itaonyesha kuwa serikali (Tanzania) imekuwa makini, haina chochote cha kuficha katika hili.

Alisema kuchelewa kwa serikali kuchukua hatua kunaweza pia kuchelewesha utoaji wa ahadi na misaada mipya ambayo inatolewa na nchi wahisani, pia hili linaweza kuwakwaza wawekezaji

Balozi huyo aliongeza kuwa si rushwa kubwa kubwa tu inayoikera serikali yake, badala yake akaongeza kuwa ili kurejesha imani kwa wahisani, rushwa ya aina yoyote haina budi kuchukiwa na kisha kuchukuliwa hatua kali na za haraka.

Alionya dhidi ya maamuzi ya baadhi ya watu wenye uwezo kuelekea kupewa nafasi zaidi wakati mwingine kuliko maslahi ya maelfu ya watumishi ambao ajira zao zinahatarishwa kutokana vitendo hivyo vya rushwa au wakati mwingine ajira zao kupotea.

Balozi huyo, pia alieleza masikitiko yake kutokana na hali za maisha ya watu wengi nchini kuendelea kuwa duni huku wachache wakiendelea kuneemeka mwakati wananchi walio wengi wakiendelea kuishi katika hali ya umaskini wa kutisha.

Balozi huyo alieleza kuwa Uholanzi itaendelea kuwa mshirika mkubwa wa Tamzania katika masuala ya maendeleo na kufahamisha kuwa mwaka huu, imetoa msaada unaofikia zaidi ya Euro milioni 80 (karibu dola za Kimarekani milioni 100) ambazo alisema sehemu kubwa imechangiwa kupitia katika bajeti ya serikali.

Hata hivyo, balozi huyo alieleza kuwa si jambo la kujivunia kwa Tanzania, kuona asilimia 40 ya bajeti inachangiwa na wahisani na washirika wa maendeleo.

"Lazima mtambue kuwa jambo hili haliwezi kuendelea daima. Ninaishauri Tanzania ianze kuangalia jinsi ya kujiondoa katika mtego huu wa kutegemea misaada, hasa kwa kusaka vyanzo vyake vya mapato. Licha ya ukweli kwamba mapato yanayotokana na kodi yanaongezeka, tunaipongeza serikali kwa mafanikio hayo, lakini hiyo bado haitoshi," alisema.

Balozi huyo alisema hiyo haitoshi kwa sababu uchumi wa Tanzania bado ni wa chini mno na kwamba nchi inatakiwa kuwa na mkakati wa kukuza uchumi wake haraka, ili ukuaji wa uchumi uwe zaidi ya asilimia sita au saba za sasa.

"Ukuaji huu wa sasa unatia moyo, lakini ili kupunguza kiwango kikubwa cha umaskini, ukuaji uchumi unapaswa uwe mkubwa na unaokwenda haraka. Hiyo, inatakiwa kuwa dira ambayo Tanzania haina budi kujiwekea, pamoja na jamii na iwe ya kuiweka katika uchumi wa kiwango cha kati ifikapo mwaka 2020," alisema.

Balozi huyo alieleza pia kuwa, ili kuchangia katika kukua na kuimarika kwa uchumi, sekta binafsi haina nudi kushirikishwa na kuhusishwa kikamilifu.

Alieleza faraja ya Uholanzi kuwa miongoni mwa nchi ambazo zimewekeza kwa kiasi kikubwa katika Tanzania. Nchi nyingine ni, Uingereza, China, India na Afrika Kusini, katika sekta mbalimbali zikiwamo za kilimo cha maua, benki, utalii, mawasiliano na nishati .

Alishauri kuwa mapato yanayotokana na kodi hayana budi kuelekezwa katika sekta muhimu kama vile, elimu na afya, kuongeza na kuimarisha miundombinu. Akaongeza kuwa hilo ndilo ambalo Watanzania wanalihitaji zaidi kwa sasa.

Alifahamisha kuwa mambo hayo hayajafanyika katika Tanzania licha ya uwekezaji ambao umekuwa ukiendelea kufanyika na kushauri kuwa kuboreshwa kwa mazingira ya uwekezaji nchini ili wawekezaji wanapoingia nchini wapate nafasi ya kushiriki katika ukuaji wa uchumi wa nchi.

Alionya kuwa wanachotaka kuona wawekezaji na wahisani ni kuona matunda ya fedha zao zinazoingizwa na kuwekezwa katika Tanzania badala ya kuendelea kuwaona watu wakiwa maskini wa kutupwa.

Aliwataka viongozi wa Tanzania kuwa tayari kujifunza kutoka nchi nyingine kama Kisiwa cha Mauritius, ambacho hakina madini kama dhahabu, gesi au mafuta, lakini kimepiga hatua kubwa kimaendeleo, kiasi cha wananchi wake kuwa na kipato kinachofikia dola za kimarekani 5,000 kwa mwaka, ikilinganishwa na dola 350 kwa Watanzania. HABARI hii imetoka gazeti la Mwananchi

Thursday, September 20, 2007

Mlingotini



Mojawapo ya studio maarufu kijijini kwetu.

Pwani ya Changwahela bwagamoyo


hebu cheki ilivyo safi wanatunza mazingira yao hawa, wanalima mwani.

Mlingotini si mchezo



Hebu angalia kule Mlingotini zipo nyumba kama hizi.

Makao makuu ya kijiji kwetu Mlingotini



Nadhani bila shaka una fununu na au taarifa mbalimbali zinazohusu kijiji chetu hiki, hebu kicheki hapa ni katikati ya mji wa Mlingotini, kijiji chetu hiki kina tarafa sita. Mlingoti wenyewe sikuuona wenyeji walinieleza kuwa ulishatokomea muda mrefu, upo hapo.

Daraja la kutoka kwetu Ntwara kwenda Nchumbiji



Mafundi wakiendelea na kazi ya ujenzi wa daraja la Umoja katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji, daraja ambalo linategemewa kuwa kiungo kwa Tanzania na nchi za kusini mwa Afrika. Picha na mwanakombo Jumaa, Maelezo.

Tuesday, September 18, 2007

Mvuna chumvi kijiji Changwahela



Kama ulikuwa ukidhani uvunaji chumvi sijui ukoje hebu cheki mchakato mzima wa uvunaji chumvi na jinsi vijana wanavyochakarika

Huu ndo mwani



Dk Aviti Mmuchi akizungumza baada ya kukagua zao la mwani kijijini Mlingotini

Mama akivuna mwani



Mwanamama wa Bwagamoyo akivuna zao la mwani maarufu na lenye matumizi mengi kote dunia ingawa hapa nchi kwetu bado halijapata msukumo.

Monday, September 17, 2007

Salva Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu



RAIS Jakaya Kikwete, amemteua Mwandishi Mwandamizi nchini, Salvatory Rweyemamu (pichani) , kuwa Mkurugenzi mpya wa Idara ya Mawasiliano Ikulu.

Salvatory anachukua nafasi hiyo ambayo iliachwa wazi na Balozi Peter Kallaghe, ambaye sasa ni balozi wa Tanzania, nchini Canada.

Taarifa ya Idara ya Habari (Maelezo), iliyotolewa jijini Dar es Salaam jana, ilisema uteuzi huo ulianza tangu Septemba 11.

Kabla ya uteuzi huo, Salvatory alikuwa anafanyakazi katika Kampuni binafsi ya ushauri wa masuala ya mawasiliano ya G na S Media Consultants.

Salvatory ni miongoni mwa waandishi wandamizi nchini, ambao wanafahamika kutokana na kazi zao za kitaaluma ambazo wamekuwa wakifanya.

Mkurugenzi huyo aliwahi kuwa Mhariri katika Kampuni ya Uhuru Publications, wachapishaji wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo kabla ya kwenda kuanzisha kampuni nyingine akiwa na wanataaluma wengine waandamizi.

Kampuni hiyo ambayo aliazisha akiwa na waandishi wengine waandamizi ni Habari Corporation.

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Rais mwaka 2005, Salvatory alikuwa ni miongoni mwa waandishi waliokuwa wakiandika makala mbalimbali zinazoingia kwa undani katika kuwachambua wagombea wa kiti hicho. Picha ya Magid Mjengwa.

Tuesday, September 11, 2007

Watoto



Hivi ni ajira kwao au ni kazi kama za nyumbani hivi, au ni wanacheza sijui hebu nambie ndugu msomaji, lakini hivi ndivyo mpigapicha wetu Hassan Mndeme alivyowakuta watoto hawa wakifanya kazi zao huko kijiji cha Komtonga, wilayani Mvomero, Morogoro.

Citizen sasa iko mtandaoni



The Citizen is now a click away. To log in type www.thecitizen.co.tz on your bowser and then click "online" Ni kwamba sasa ngoma iko mtandaoni inaruka kwa masafa ya mbali na unaweza kuipata wakati wowote, saa yoyote na muda wowote.

Monday, September 10, 2007

Shenaz aaga Dunia....



Malkia wa kunengua miondoko ya Taarab na Mduara nchini, Shenazi Salum pichani ni miongoni mwa watu 27, waliokufa kwenye ajali ya basi, iliyotokea juzi kwenye Kijiji cha Majenje, Mbarali, Mbeya.

Kwa mujibu wa mdogo wa mwanamuziki huyo aitwaye Hanifa Salum, Shenazi alifariki dunia, muda mfupi baada ya kutokea ajali hiyo, iliyohusisha magari matatu....

alisema, Shenazi alipata ajali hiyo, alipokuwa akirejea nyumbani kwake Dar es Salaam na alikuwa akitoka Tunduma, Mbeya kwenye shughuli zake za muziki “Alituaga kwamba anakwenda Mbeya kufanya ‘shoo’, hatukujua kama ndiyo kifo kilikuwa kinamwita, lakini ndiyo hivyo Mungu kamchukua,” alisema Hanifa huku akitokwa na machozi.

Rafiki wa Shenazi ambaye naye ni mnenguaji maarufu, Mwajuma Thabit ‘Rose Jimama’, anasema kuwa marehemu alikwenda Mbeya na mwanamke aliyemtaja kwa jina moja la Tuki.

Rose alisema: “Nilipata taarifa kama Shenazi amepata ajali, nikapiga namba yake, ikapokelewa na polisi mmoja huko Mbeya, nikamuomba nataka kuongea na Shenazi, akanijibu, unataka kuongea na maiti? “Nilichanganyikiwa, yule polisi aliniambia rafiki yangu Shenazi amekufa na Tuki hali yake ni mbaya, nidhani utani, lakini yote ni mipango ya Mungu.”

Habari zaidi zilisema kuwa rafiki huyo wa Shenazi, Tuki, amevunjika miguu yote na alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Misheni ya Chimala, Mbarali. Shenazi alikuwa kwenye basi la SABCO aina ya Scania, T443 APF ambalo liligongana na lori pamoja na magari mawili yanayomilikiwa na Halmashauri ya Mbarali.

Ajali hiyo iliyoua watu 27, ilisababisha majeruhi 33. Shenazi alitarajiwa kuzikwa jana ambapo mwandishi wetu walifika nyumbani kwao, Ilala, Dar es Salaam na kukuta taratibu za mazishi zikiwa zimeshaanza kufanywa. Mbali na kunengua, malkia huyo atakumbukwa kama kungwi, aliyekuwa akiwafunda watu kabla ya ndoa, pia ni mwigizaji ambapo enzi za uhai wake aliwahi kucheza Filamu ya Kitchen Party ambayo ilipata umaarufu mkubwa.

Mungu Alaze Roho Za Marehemu Mahala Pema Peponi Amen...

Taarifa zaidi hebu mcheki NGOWI atakupasha ipasavyo, nemechukua taarifa hii kwake.

Hongera Mrocky Mrocky kwa kupata jiko



Father Kidevu, kidevu chako kiko wapi siku hizi. Mpiga picha mahiri wa magazeti ya Habari Leo na Daily News na pia mwanablogu, Mroki Mroki, amefunga pingu za maisha. Kila la kheri kaka maisha haya ya ndoa ni namna unavyoyacheza tu ni bomba mnoooooo hongeraaaaaaa!!!!!!!

Thursday, September 06, 2007

Haya ya Hoyce na maoni yake kwa Miss Tanzania

AdhiaHoyce.
Yamesemwa mengi jamani wengine tukaamua kukaa kimya kuhusu huyu Miss Tanzania wetu leo nimepita mtandaoni nikamkuta mdau mmoja mwenye uchungu akisema hivi: msome kidogo
"NILIDHANI walioziacha fikra za Mwalimu ni viongozi wa CCM peke yao, kwa
hakika nilikuwa nimekosea sana. Jumamosi iliyopita wakati Watanzania wengine
walikuwa wanafurahia ushindi wa Taifa Stars dhidi ya The Cranes ya Uganda,
kuna kundi la Watanzania waliokuwa wananung'unika kwanini binti mwenye asili
ya Kihindi kachaguliwa kuwa Vodacom Miss Tanzania 2007.

Kwa vile Watanzania tuna mazoea ya kusahau mambo muhimu, hasa timu yetu ya
taifa inapocheza, nimeonelea nililete jambo lililotokea Leaders Club,
Kinondoni, Dar es Salaam mapema kabla ya mechi ya marudiano na Msumbiji.

Kama nilivyosema hapo juu kuwa mwanzoni nilipokuwa naliangalia suala la
"kuziacha fikra za Mwalimu" nilikuwa naangalia kwa mtazamo wa vyama vya
kisiasa zaidi, lakini baada ya kusikia mwitikio wa watu baada ya Richa Adhia
kuwashinda warembo wengine 25 na kutwaa taji hilo maarufu zaidi la urembo
Tanzania, nimejikuta nikihitimisha kuwa si viongozi wa CCM tu walioziacha
fikra za Mwalimu bali pia wananchi wa kawaida na wengine wenye nafasi kubwa
katika jamii ambao si tu wameziasi fikra hizo, bali pia bila haya wala
kusitasita wanatangaza hadharani hoja zao mbovu na zisizo na nafasi katika
Tanzania hii.

Sijui ni makosa ya nani au ni kutokana na sababu ipi kwamba Watanzania
tumeanza kuwa wabaguzi wa rangi. Kwa taifa ambalo lilimwaga damu yake
kuupinga ubaguzi wa rangi, na kutoa rasilimali zake kuwasaidia wapigania
uhuru, inaudhi na inatisha kuona kuwa leo hii bila hata aibu, tunatangaza
hadharani kuwa sisi ni wabaguzi! Gazeti moja liliandika kwa kichwa cha
habari kikubwa kuwa kitendo cha binti huyo wa Kitanzania kuchaguliwa ni
"aibu".

Wednesday, September 05, 2007

Operesheni Okoa Richard

Hi all!



NI wiki ya nne sasa tangu lianze shindano la kumtafunta mshindi wa jumba la Big Brother ambapo tayari washiriki wawili walishatolewa safari hii wanaopigiwa kura ili hatimaye mmoja wao atoke ndani ya jumba hilo ni Meryl, Richard wetu na Maureen. Jamani hebu tuchangamkieni dili tuwapigieni kura hawa wawili Maureen na Meryl, lakini tumpigieni kura nyingi mno Meryl ili Richard na Mareen wabakie.

Ili kupiga kura, tuma ujumbe mfupi wa simu yaani, SMS ukiandika neno VOTE na jina la mshiriki unayetaka aondoke kutoka katika jumba la Big Brother Africa (Mpigie Meryl). Na utume kwenye nambari 15726

Kumbuka kuwa unampigia kura mtu ili atoke ndani ya jumba hilo, kwa hiyo usimpigie kura mshiriki umpendaye. Pia kumbuka kutumia jina la kwanza la mshiriki na siyo majina ya utani wala majina ya wazazi wao.

Pia unaweza kupiga kura kura kupitia tovuti ya www.mnetafrica.com/bigbrother.

Au piga kura kupitia nambari 27-83-900-0000

Tuesday, September 04, 2007

Wabongo si mchezo





Hebu cheki shughuli iliyofanywa na washabiki wa mechi ya juzi. Siyo kwamba haujaisha umebomolewa uwanja wetu.


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida ikiwa ndio siku ya kwanza tu kutumika kwa Uwanja Mkuu wa Taifa wa Tanzania (uwanja mpya) uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu, mashabiki wameng'oa viti pamoja na baadhi ya koki za mabomba ya maji chooni.
Mechi ya kwanza kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua mashabiki 60,000 waliokaa vitini ilichezwa Jumamosi iliyopita baina ya Taifa Stars na Uganda na ilihudhuriwa na watazamaji wanaozidi 50,000 ambato ni kubwa kutokanana mechi kuwa ya kirafiki.
Baada ya mechi hiyo imegundulika kuwa baadhi ya viti vya rangi ya bluu vimeng'olewa na baadhi ya koki za mabomba chooni pia ziling'olewa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Msimamizi Mkuu na Mtaalamu wa Ujenzi katika uwanja huo, Alloyce Mushi alisema jana walitarajia kufanya tathimini na kesho watakamilisha ukarabati huo ambao umeshaanza.
Mafundi waliongea uwanjani hapo, walidai vitu vingi vimeharibika kutokana na wingi wa mashabiki kutokujua jinsi ya kutumia vifaa vilivyopo ndani ya uwanja huo ikiwa ni pamoja na kupanda juu ya viti wakati wa kushangilia.
Baadhi ya mafundi hao walisema viti vya kukunja na kufungua ndiyo vina uimara zaidi kuliko vile ambavyo vimefungwa juu ya bomba moja.
Viti vilivyong'oka ni vya upande wa Mashariki na Magharibi ya uwanja huo baadhi vikiwa ni karibu na jukwaa la VIP.
Uwanja huo ambao bado haujafunguliwa rasmi utatumika tena katika mechi ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika Jumamosi baina ya Taifa Stars na Msumbiji.