Friday, December 29, 2006

Bonde la mpunga

mvua zinazoendelea kunyesha zimesababisha mafuriko huku bonde la mpunga lilipo jengo la May Fair Plaza.

Hospitali ya Temeke



Hili ndilo jengo jipya la hospitali ya Temeke linavyoonekana leo. Picha kwa hisani ya Deus Mhagale.

Mafuriko ya leo


Hivi ndivyo ilivyo huko bonde la mpunga Msasani, maji mnaona yalivyozingira. Picha ya Deus Mhagale.

Richmond mpya ni kanzu mpya, sheikh wa zamani?

KILA kona ulikuwa ukipita rat a tat!! hiyo si mitaa ya mijini, peke yake bali nchi nzima. Tatizo mgawo wa umeme au kiufupi tuseme ukosefu wa umeme umekuwa Kero!

Kero kwa sababu umesababisha wengi kukosa ajira, kiwango cha uhalifu kuongezeka, umasikini, wizi, uchumi kushuka na kila kitu kibaya unachokijua msomaji.

Wiki hii Shirika la Umeme likatangaza kuwa mgawo sasa basi, sababu kubwa la kufa kimya kimya kwa mgawo huu ni kujaa kwa mabwawa ya Mtera na Kidatu. Inasikitisha!

Inanisikitisha siyo kwa sababu maji yamejaa au kwa kuwa, eti siwatakii watanzania maisha bora na mema, bali ni kutokana na kuwa katika kiwango cha chini cha maendeleo cha kutegemea nature, wakati uwezo tunao wa kutotegemea nature. Unaweza kuendelea zaidi hapakwa kubonya hapa

Mnara wa Kigamboni


Hivi karibuni huu mnara huu wa kuongozea meli uliopo kule Kigamboni utaanza kutumika.

Dege jipya la ATC


Shirika la ndege la Tanzania ATC limeingiza nchini dege jipya lenye siti 102 aina ya boeing 737-200 (hili ni kubwa kwetu msicheke) kutoka kampuni ya Celtic Capital Corporation ya Canada linaanza kazi leo.

Tuesday, December 26, 2006

Uharibifu wa mazingira


Pichani anaonekana mwanakijiji akikusanya kuni baada ya kuzisanya katika eneo hili. Hapa ni Iringa.

Maji jamani maji!!!!


Tatizo la maji ni kerooo, sijui kama washikaji zangu kina Ulimwengu kule Houston, Juma- New York, Deogratius kule Wichita na wengine kibao mnakumbuka hali hii.

Ajira kwa watoto!!!


Nia ajenda pana sana hii, kila mmoja ana tafsiri yake na kila mwenye tafsiri ana tafsiri ndogo ndogo. Hapa watoto wako na vigunia vyao huku Masasi. Picha ya Mpoki Bukuku.

Wednesday, December 20, 2006

Rafiki arejea toka Marekani

Pichani ni rafiki yangu Mayunga Ntangalo, Mtanzania aliyeishi miaka zaidi ya saba anazo stori nyingi saana za kusimulia wabongo. Ni mtunzi wa vitabu anasifika Marekani kwa novel yake maarufu, Odd Scratches ambayo inauzwa katika maduka mbalimbali na hata kati Ebay na Amazon na ni mwalimu, mtafute.

Sunday, December 17, 2006

Solidarity forever



Wanaharakati tunaweza kuwaita wakuu wakiwa katika mstari wa mbele kabisa katika maandamano ya kudai haki watu weusi ambayo inaonekana kukandamizwa siku hadi siku hapa walikuwa wakipinga mauaji ya Sean Bell. Hakiiiiii.

Jamaa akiwa makini kazini kurekodi matukio



Mtaa wa 34 hapa akijishughulisha kuchukua matukio muhimu ya maandamano ya kupinga udhaifu uliojitokrza hadi Sean Bell kuuawa.

Maandamano New York



Wanaharakati wakiandamana wakiandamana katika barabara ya tano ya mitaa ya Manhattan, jijini hapa (New York) kupinga unyama aliofanyiwa kijana mwenye asili ya kiafrika Sean Bell ambaye alipigwa risasi hamsini.

Leo asubuhi New York ilikuwa cool sana



Amini usiamini jiji la New York leo asubuhi mpaka saa 5 hivi lilikuwa kimya saana, barabara ziokafungwa kukawa na askari kibao kwaajili ya kusubiria maandamano ya kupinga kupigea risasi 50 kinyama kwa kijana mwenye asili ya kiafrika.

Kituo cha Treni Grand Central



Pichani urembo uliopo juu kabisa ya .stesheni hii kubwa kabisa ya treni jijini New York, ingekuwa kule kwetu hapa michongo hii ni balaa

Friday, December 15, 2006

Thursday, December 14, 2006

Mnara huu uko karibu kabisa na CNN



Ipo minara mingi hapa jijini, lakini huu unasababu yake kubwa kuwekwa humu, nayo ni kwamba upo karibu na makao makuu ya CNN.

Wednesday, December 13, 2006

Washington Square kama Mnazi Mmoja

kando ya Chuo Kikuu cha New York ilipo hii bustani.

Christmass imefika



Huku mambo ya Krismasi tayari yameanza unaona kwa mbaali miti ya mikrismasi ikiwa imemwagwa mitaani.

Kituo Kipya cha televisheni

hili ni bango la kituo kipya cha televisheni cha Marekani kinachoifagilia Afrika, humo ni Isidingo, bongo music na kadhalika. Kituo kina makao makuu yake Los Angeles hapa Marekani na kitaanza kurusha matangazo hivi karibuni, stay in touch.

Tuesday, December 12, 2006

Vimbwete



Hapa washikaji wa Chuo Kikuu cha New York wakipiga buku ni katika bustani ya Washington Square, staili yao ni almost sawa na yetu pale University of Dar es Salaam wakikalia vijiwe maarufu kama vimbwete waweza pia kuwapata katika zipo opportunities kibao na ninasikia wanataka kufungua tawi bongo.

Monday, December 11, 2006

Kifungo Kikubwa

Ushawahi kuona kifungo kikubwa hivi.

Charahani

Sanamu la Fundi Charahani wa kwanza kabisa New York.

Tanzania Marekani


Wananchi Mkutanoni ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, New York.

Waheshimia Mabalozi



Balozi Augustine Mahiga, Balozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, akizungumza na Naibu wake, Tuvako Manongi, nyumbani kwake Mt. Vernon, New York.

Mkurugenzi Kijana



Bw. Edward J. Bergman, kijana mdogo wa miaka 26, Mkurugenzi wa Kampuni ya African Travel Association, kampuni hii inaitangaza Tanzania Marekani, muulize lolote kuhusu Tanzania anaifahamu kuliko wewe.

Tuesday, December 05, 2006

Eneo la kulima



Haya ndiyo maisha yetu.

Huku ni kijijini Usiulize, Meatu



Maisha haya unayakumbuka?

Kunakopikwa masuala yote duniani hapa



Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa

Balozi Mahiga

Balozi wa Tanzania UN, Dk Augustine Mahiga

Mkutanoni



Jopo la waandishi wa habari waliopo jijini New York wakimsikiliza Balozi wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa, Dk Augustine Mahiga.

Balozi Mahiga Mkutanoni



Jana Balozi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Dk Augustino Mahiga alilihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, kubwa likiwa kupiga vita biashara haramu ya almasi za damu. (Picha imepigwa na Athmani Hamisi)

Ndani ya kikao cha Baraza Kuu la Usalama la UN



Balozi Augustine Mahiga (aliyeketi) akizungumza jambo na Wasaidizi wake baada ya kumaliza kikao cha jana kilichozungumzia masuala ya ukomeshaji silah ndogo ndogo.

Saturday, December 02, 2006

Mkutano wa TED Global kufanyika Tanzania


MKUTANO mkubwa duniani wa kila mwaka wa masuala ya teknolojia, (technology, entertaiment, design) unaowashirikisha watu maarufu duniani wanaozidi 1000, utafanyika Tanzania kwa mara ya kwanza.

Akitangaza rasmi jana jijini hapa New York, Mkurugenzi wa Programu wa TED, Emeka Okafor (pichani kushoto), Emeka unaweza kumfikia kwa kubonya hapaalisema mkutano huo umeamuliwa kufanyika rasmi Tanzania kutokana na mafanikio makubwa iliyoyapata Tanzania katika nyanja mbalimbali ikiwamo uchumi na siasa.

“Hatujaichhagua Tanzania kwa bahati mbaya au kwa upendeleo tu, au eti tunataka kutazama wanyama wa mbugani, la hasha , bali ni kwasababu ya mafanikio makubwa nchi hiyo iliyoyapata kiuchumi na kisiasa,”alisema Okafor.

Kama wewe unajihusisha na masuala ya teknolojia na biashara, tuma maombi yako ili uweze kuhudhuria mkutano huu. Watu utakaokutana nao ana na mada zinazojadiliwa kwenye mikutano ya TED, utasuuzika nafsi yako.